*MAOMBI YA UPONYAJI

*MAOMBI YA UPONYAJI* πŸ”₯






BWANA Yesu asifiwe sana



πŸ‘‰inawezekana umeomba miaka mingi lakini bado unahangaika na tatzo

πŸ‘‰ siyo kwamba hujii kuomba lakini kuna roho ya mauti imefunga maisha yako bila wewe kujua .


πŸ‘‰ Umefungwa wapi sasa ❓

Tuone hapa


πŸ”₯ kila mchumba anayekuja kwako anakuacha ujue umefungwa


πŸ”₯ kila unapoanzisha biashara inakufa au unataka kuanzisha unaogopa utapata hasara hyo ni mauti iloyofunga uchumi wako .



πŸ”₯ Kila unapotaka kusoma neno la Mungu unapata usingizi ,ukiona hali hyo ujue kuna mauti imeshikilia maisha yako usimjue Mungu zaidi


 *Tuombe*




Baba katika jina la Yesu ,ninakuja kinyume dhidi ya nguvu zote za giza zilizoshikilia maisha ya watu wako ninasambaratisha nguvu za kaburi na kila roho za mauti zilizoshikilia maisha ya watu wako kwenye afya ,kwenye uchumi,kwenye,ndoa,na kwenye elimu katika jina la Yesu  .Kama ilivyoandikwa katika HOSEA 13:14 kusema


14 Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Kujuta kutafichwa na macho yangu.
Hosea 13 :14

Ninasimama juu ya neno hilo kusambaratisha na kuhatibu na kuzing'oa nguvu za kaburi na mauti katika jina la Yesu




πŸ”₯ Ninakuja kinyume na kila madhabahu inayopitisha magonjwa na laana na mikosi na kila roho za ajali naziharibu na kuzisambaratisha  katika jina la Yesu
Maana imeandikwa



2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;
Kumbukumbu la Torati 12 :2

3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.
Kumbukumbu la Torati 12 :3


Ninavunja kila madhabahu ipitishayo roho za uchawi na uganga ziletazo laana na mateso katika maisha ya watu wako


πŸ”₯Ninaamuru kila roho chafu ,roho ya magonjwa,roho ya umaskini ,roho ya mateso ,na roho ya uharibifu katika biashara ,uchumi, familia n.k kutoka katika jina la Yesu kila ubaya uliotumwa kwa watu wa Mungu ninauamuru kurudi kwa walio utuma kuanzia sasa katika jina la Yesu


5 Atawarudishia adui zangu ubaya wao; Uwaangamize kwa uaminifu wako.
Zaburi 54 :5

Ninaenda kinyume na kila nguvu za giza na mapepo na majini na roho za magonjwa katika jina la Yesu.ninatumia mamlaka yake Yesu kuharibu kila ubaya


1 Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
Mathayo 10 :1


Amen.


Bwana Yesu ninakushukuru kwa haya Maombi naamini kwamba wewe ndye ngome na mwamba wa wokovu Wangu na tukiomba jambo lolote kwa jina lako twapata na huu ndyo ujasiri uliotupa

Asante Yesu maana wewe unatenda makuu ndani ya maisha ya watu wako naamini hata Leo utafanya jambo jipya katika maisha ya watu wako

Katika jina la Baba , Mwana na Roho Mtakatifu .Amen





πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»πŸ™πŸ»


CATHERINEπŸ’’πŸ‘—πŸ‘‘

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*