SABABU ZINAZOFANYA MAOMBI YAKO YAKOSE MAJIBU

πŸ“– *SABABU ZINAZOFANYA MAOMBI YAKO YAKOSE MAJIBU* πŸ“–

_SEHEMU YA TANO_

Mwlm. Peter Francis

https://peterfrancismasanja.blogspot.com


Karubu tena katika mwendelezo wa somo tuendelee kujifunza

Nakuombea kwa Mungu uweze kujifunza kitu hapa na roho wa Mungu akupe ujuzi kupitia somo hili .Amen


πŸ‘‰ZIFUATAZO NI SABABU ZINAZOWEZA KUFANYA MAOMBI YAKO YAKOSE MAJIBU




πŸ“–πŸ‘¨πŸ»β€πŸ’» _KUSHINDWA KUTUMIA MAMLAKA_

πŸ‘‰Mamlaka tunayo izungumzia hapa ni ya kiroho ambayo tumepewa na Mungu .

Watu wengi walijikuta hawaoni matokeo chanya ya Maombi yao kwa sababu walishindwa kuitumia mamlaka waliyopewa na Mungu

πŸ“– 19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Luka 10 :19

πŸ‘‰Wengi walijikuta shetani anawanasa kwa kushindwa kutumia mamlaka vizuri .

πŸ‘‰Ukiitumia mamlaka uliyopewa na Mungu utayaona matendo makuu ya Mungu yanajidhihirisha kwako .

πŸ“– 23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake.
Marko 11 :23

24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.

Marko 11 :24

πŸ‘‰ ukiitumia mamlaka ya kiroho uliyopewa na Mungu hata mapepo utayatoa na wagonjwa pia watapona kabsa .

πŸ“– 1 Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
Mathayo 10 :1

8 Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

Mathayo 10 :8



πŸ‘‰Ukiitumia vizuri mamlaka utaona mambo makuu maishani mwako yanatendeka

Hata wanaokuzunguka utawashangaza sana kwa jinsi Mungu anavyozidi kukutendea mema .

πŸ“– wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?

Luka 20:2


πŸ‘‰Ukiitumia mamlaka hata watu wataona jinsi Mungu anavyojidhihirisha kwako kupitia imani uliyonayo .

πŸ“–πŸ‘¨πŸ»β€πŸ’» _KUACHA KUTUBU DHAMBI_


πŸ“– 8 Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.

1 Yohana 1 :8

πŸ‘‰Mungu anataka tutubu dhambi zetu ili atusikie kuomba kwetu.

πŸ“– Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

Isaya 1:18

πŸ‘‰ Mungu mwenyewe tunamkosea sana na tunamkasirisha sana kwahyo tunapomwendea lazima tutubu dhambi zetu bila toba tutakuwa mbali na Mungu

πŸ“– 1 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
Isaya 59 :1

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.
Isaya 59 :2

3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong'ona ubaya.

Isaya 59 :3

πŸ‘‰Tunaona jinsi gani Mungu anahitaji tutubu ili atujibu maombo yetu .

πŸ“– Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.

2 Petro 3:9


πŸ‘‰Ahadi za Mungu ndani ya maisha yako zinahitaji toba ili zitimie maishani mwako .



✍✍✍✍✍✍✍✍✍✍

Katibu tena katika sehemu ya sita .


MUNGU AKUBARIKI SANA

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*