KUIJENGA IMANI




.*πŸ“–KUIJENGA IMANI πŸ“–*



MWL.Peter Francis Masanja 



πŸ“–πŸ– 2 Tukamtuma Timotheo ndugu yetu, mtumishi wa Mungu katika Injili ya Kristo, ili kuwafanya ninyi imara na kuwafariji kwa habari ya imani yenu; 

1 Wathesalonike 3 :2



πŸ‘‰πŸΌkuana wakati haitoshi kukaa peke yako na kuyatafakari maandiko 

Hii inakulazimu ujifunze kwa walio juu zaidi yako ili imani yako izidi kukua zaidi 


πŸ‘‰πŸΌIpo faida kubwa kutaka kujifunza zaidi ili  ukue zaidi kiimani 



ZIFUATAZO NI FAIDA AMBAZO LEO NATAKA TUZIONE 


πŸ“—KUKUZA UWEZO WA KUMTAFAKARI MUNGU 



πŸ“—KUONGEZA KIWANGO CHA IMANI 


πŸ“– Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.

Luka 17:5


πŸ‘‰πŸΌ Kumbuka hili jambo , ili imani ijengeke ndani yako lazima uondoe mashaka ndani yako kwanza 


πŸ“– 23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. 
Marko 11 :23

24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu. 
Marko 11 :24


πŸ‘‰πŸΌIli imani ijengeke ndani yako epuka kusikia mafundisho yoyote yatakayokufanya uiache imani yako 


πŸ“– 8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani. 
Matendo ya Mitume 13 :8

9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho, 
Matendo ya Mitume 13 :9

10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka? 
Matendo ya Mitume 13 :10

11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza. 
Matendo ya Mitume 13 :11

12 Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana. 
Matendo ya Mitume 13 :12


πŸ‘‰πŸΌepuka mafundisho yoyote yenye asili ya kuzimu yanayolenga kukuangusha kiroho 




https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*