RAFIKI MWEMA

⛪ *RAFIKI MWEMA* ⛪


Mwlm.Peter Francis


SERHEMU YA PILI


πŸ‘‰πŸΌKosea rafiki ufe


Rafiki mwema lazima mfanane tabia na vitu mpendavyo


πŸ‘‰πŸΌ Rafiki mwema lazima mfanane kimisimamo

πŸ‘‰πŸΌ misimamo ya imani

πŸ‘‰πŸΌkusimamia kweli

πŸ‘‰πŸΌKusimamia utakatifu



Musa aliambatana na haruni


πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂


πŸ‘‰πŸΌ Kwanini Musa aliambatana na haruni ❓ kwasababu walifanana katika eneo la utumishi πŸ‘‰πŸΌπŸ˜€πŸ˜€


πŸ“–πŸ– Bwana akanena na Musa na Haruni, akawaagiza wawaendee wana wa Israeli, na Farao, mfalme wa Misri, ili awatoe hao wana wa Israeli katika nchi ya Misri.

Kutoka 6:13



πŸ‘‰πŸΌMusa na Haruni wote walikuwa wanamcha MUNGU na kumpenda


πŸ‘‰πŸΌ HAO VIJANA WALISHIKAMANA MPAKA WAKATUPWA KWENYE TANURU YA MOTO KWA KUISIMAMIA KWELI YA MUNGU



πŸ“–πŸ– 12 Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
Danieli 3 :12

13 Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme.
Danieli 3 :13

14 Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
Danieli 3 :14

16 Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.
Danieli 3 :16

17 Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme.
Danieli 3 :17

18 Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
Danieli 3 :18

19 Ndipo Nebukadreza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto.
Danieli 3 :19

20 Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
Danieli 3 :20

23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.
Danieli 3 :23

24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
Danieli 3 :24


πŸ‘‰πŸΌπŸ‘‰πŸΌRafiki mwema hatakuacha katika wakati wa shida na raha


πŸ“–ANGALIA HAWA VIJANA WALIOISIMAMIA KWELI YA MUNGU NAO WALIKUWA MARAFIKI




πŸ“– DANIELI

πŸ“–SHADRACK , MESHACK NA ABEDINEGO .



πŸ–πŸ“– 6 Basi katika hao walikuwapo baadhi ya wana wa Yuda, Danielii, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria.
Danieli 1 :6

7 Mkuu wa matowashi akawapa majina; alimwita Danielii, Belteshaza; na Hanania akamwita Shadraka; na Mishaeli akamwita Meshaki; na Azaria akamwita Abednego.
Danieli 1 :7

8 Lakini Danielii aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa; basi akamwomba yule mkuu wa matowashi ampe ruhusa asijitie unajisi.
Danieli 1 :8

9 Basi Mungu alimjalia Danielii kupata kibali na huruma machoni pa huyo mkuu wa matowashi.
Danieli 1 :9

11 Ndipo Danielii akamwambia yule msimamizi, ambaye mkuu wa matowashi amemweka juu ya Danielii, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria,
Danieli 1 :11


πŸ‘‰πŸΌYESU ALIAMBATANA NA PETRO

πŸ“–Rafiki mwema


πŸ“–πŸ– Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka.

Mathayo 26:37



πŸ“–Petro alikuwa mwanafunzi wa karibu sana aliyempenda Yesu



πŸ“–πŸ– 7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.
Yohana 21 :7

8 Na hao wanafunzi wengine wakaja katika mashua; maana hawakuwa mbali na nchi kavu; ila yapata dhiraa mia mbili; huku wakilikokota lile jarife lenye samaki.
Yohana 21 :8

11 Basi Simoni Petro akapanda chomboni, akalivuta jarife pwani, limejaa samaki wakubwa, mia hamsini na watatu; na ijapokuwa ni wengi namna hiyo, jarife halikupasuka.
Yohana 21 :11

12 Yesu akawaambia, Njoni mfungue kinywa. Wala hakuna mtu katika wale wanafunzi aliyethubutu kumwuliza, U nani wewe? Wakijua ya kuwa ni Bwana.
Yohana 21 :12

15 Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu.
Yohana 21 :15

16 Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu.
Yohana 21 :16

17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.
Yohana 21 :17

18 Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.
Yohana 21 :18

19 Akasema neno hilo kwa kuonyesha ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu. Naye akiisha kusema hayo akamwambia, Nifuate.
Yohana 21 :19

20 Petro akageuka akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu anafuata; (ndiye huyo aliyeegama kifuani pake wakati wa kula chakula cha jioni, akasema, Bwana, ni nani akusalitiye?)
Yohana 21 :20

21 Basi Petro akamwona huyo, akamwambia Yesu, Bwana, na huyu je?
Yohana 21 :21

22 Yesu akamwambia, Ikiwa nataka huyu akae hata nijapo, imekupasaje wewe? Wewe unifuate mimi.
Yohana 21 :22



πŸ‘‰πŸΌYESU ALIKUWA ANAANZA KUMWITA PETRO KWANZA KATI YA WANAFUNZI WAKE KWASABABU ALIMPENDA


πŸ‘‰πŸΌMTUME PAULO ALIAMBATANA NA TIMOTHEO

Rafiki wa kweli ni rafiki anayekuweka vizuri kiroho na kimwili




πŸ“–πŸ– Paulo na Timotheo, watumwa wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu, walioko Filipi, pamoja na maaskofu na mashemasi.

Wafilipi 1:1


πŸ‘‰πŸΌIli umjue rafiki mwema jiulize maswali matano yafuatayo πŸ‘‰πŸΌπŸ˜€πŸ˜€



πŸ‘‰πŸΌ Anapenda gani❓

Anachokipenda Mungu anakirihusu ❓


πŸ‘‰πŸΌ Anafaida gani kwako ❓
Au anakuja kukuangamiza


πŸ‘‰πŸΌ Anamarafiki wa aina gani❓


πŸ‘‰πŸΌAtakufanya ukue kweli kiroho na kimwili ❓


πŸ‘‰πŸΌ Je mnaendana ❓
.

πŸ‘‰πŸΌKama unarafiki ukipata mshahara anakwambia mkajiachie bar , au huyo mpendwa hakufai


πŸ‘‰πŸΌ Kama kuna rafiki simu yake imejaa Video chafu , bongo fleva na picha chafu halafu wewe umeokoka

Rafiki yangu umepotea sana
Mkimbie


πŸ‘‰πŸΌ Rafiki siku nzima anakimbilia kwenye mpira wa miguu anaangalia ratiba za mechi tu πŸ˜€πŸ˜€

Akitoka hapo anafungulia redio tena nyimbo bongo fleva .


Ukiishika simu yake angalia makundi ya what's app utakuta kajiunga na makundi ya ajabu


Biblia anaikumbuka jumapili tu πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€


Mkimbie huyo rafiki ni Yuda πŸ˜€πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂


HITIMISHO*



 *πŸ“–πŸ– 3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana* ?

Amosi 3 :3



πŸ‘‰πŸΌ Mpendwa ukiambatana na mvutabangi mtaani watu watasema umeanza kuvuta bangi

Hii ni kwa sababu dhambi inanguvu sana kuliko haki .



πŸ‘‰πŸΌ Ndyo maana Paulo alisema tujitenge na ubaya


πŸ“–πŸ– 6 Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi.
Waefeso 5 :6

8 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru,
Waefeso 5 :8

9 kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;
Waefeso 5 :9

11 Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;
Waefeso 5 :11

12 kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena.
Waefeso 5 :12





HATA KAMA UNARAFIKI AMEOKOKA KAMA ANAIKANA KWELI YA MUNGU KIMBIA KABISA UTAANGUKA πŸ‘‰πŸΌπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€


NAKUMBUKA SIKU MOJA KUNA KIJANA ALIULIZA SWALI AKANIPA USHAURI MPAKA NIKACHEKA NA KUMBLOCK πŸ˜€



Je Mtumishi unamchumba ❓


Nikamwambia ndiyo


Akaniambia unajua hawa wanawake siyo waaminifu Mimi nakushauri ahidi dada wa pili ili uliyenaye akizingua usiumie πŸ˜€πŸ˜€



Nikamwambia namwamini , namthamini, namjali, nampenda, na sipotayari kumfanyia hivyo mchumba Wangu


πŸ“–πŸ– Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

Mathayo 6:24



πŸ‘‰πŸΌHUWEZI KUPENDA WANAWAKE WAWILI HUO NI UNAFIKI KAMA SIO UNAFIKI NI UASHERATI AU UZINZI




πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂πŸƒ‍♂

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*