SEMINA YA MAOMBIVQ

Bwana Yesu asifiwe Karibu tujifunze kwa Ufupi kuhusu Somo linaloitwa




MAOMBI ..

 Inawezekana si Mara nyingi umesikia habari zinazohusiana na Maombi


Umesoma Maandiko mbalimbali yanayohusu Maombi

Na umefundishwa masomo mbali mbali kuhusu Maombi

Lakini na Leo pia napenda tukumbushane pia kuhusu kipengele hiki


Tunapozungumzia habari za Maombi
Tunaweza kumanisha vitu vingi na maana tofauti tofauti kulingana na Mazingira tofauti tofauti
*Maombi* inaweza kuwa ni njia ya ...

Msaada wa kusaidiwa ..

Muunganiko wa kitu Fulani katika Eneo Fulani .


Ninaposema ni njia ya

Maana yake Maombi yanaweza kutumika kama njia ya kukuunganisha wewe ,Kuinganisha nafsi yako ,Roho yako na Eneo Fulani /Na kitu au MTU Fulani ..


Maombi ni njia ya kuunganisha /kutengeneza daraja kati yako wewe na Mungu pia

   *1 Timotheo 2:1 1 Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;*
[1/9, 15:40] ‪+255 762 450 772‬: Mtume Paulo anasema Basi (Yatosha ) kabla ya Mambo yote nataka dua ,na sala na maombezi na Shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote ...
[1/9, 15:47] ‪+255 762 450 772‬: Katika Maombi au tunapoomba siku zote tutambue kuna vitu hivyo hapo vinne vya Muhimu

✍Dua/Supplication s

✍Sala /Prayers

✍Maombezi /intercessions

Na
✍Shukrani /Thanksgiving
[1/9, 15:50] ‪+255 762 450 772‬: Kwenye Dua tunamuuliza Mungu kuhusu mahitaji yetu /Asking God na hii inapaswa kuambatana na Unyenyekevu ndani yake..
[1/9, 15:54] ‪+255 762 450 772‬: Unapokuwa unamuuliza Mungu maana yake unatafuta Msaada wake kwa ajili ya Hitaji ulilonalo

Baada ya kutafuta msaada unaingia kwenye mawasiliano /kuwasiliana naye kwa Njia ya Sala
[1/9, 15:55] ‪+255 762 450 772‬: Unapoingia kwenye kuwasiliana utaunganishwa moja kwa moja na Mungu ukiwa unawasiliana naye
[1/9, 15:59] ‪+255 762 450 772‬: *Maombezi* ni kitendo cha kupeleka mahitaji kwa Mungu /kuwasiliana na Mungu kwa niamba ya MTU mwingine ..
[1/9, 16:03] ‪+255 762 450 772‬: Unapowasiliana na Mungu moja kwa moja mwenyewe au kwa niaba ya MTU mwingine tambua kuna mambo ambayo Mungu atafanya ambayo yatakulazimu

Kutoa *Shukrani*

Shukrani ni Maombi kwa ajili ya Kumshukuru Mungu kwa kukutendea ulichokiomba
[1/9, 16:07] ‪+255 762 450 772‬: Tuangalie aina za Maombi

✍Maombi yenye IMANI ..

Maombi yote au Dua ,Sala unayompelekea Mungu au kumfanyia Mungu ni lazima yaambatane na IMANI ndani yake ..


IMANI ndio itakayomuokoa MTU atoke au utoke kati hali /mazingira ya aina yoyote ..

*Yakobo 5:15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.*
[1/9, 16:08] ‪+255 762 450 772‬: Kinachomuokoa MTU sio kuomba tu ili mradi isipokuwa *Kuomba kwa IMANI*
[1/9, 16:10] ‪+255 762 450 772‬: Nikupe mfano huu wa kutoka kitabu cha Marko 9:23 23 Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
[1/9, 16:14] ‪+255 762 450 772‬: Ukisoma kabla huu mstari hapo huu Huyu ni Yesu mwenyewe anamwambia MTU mmoja aliyeletwa na Pepo Bubu

Kwa mazingira ya kawaida watu wa mahali hapo hawakuamini kuwa Pepo litatoka

Lakini Yesu anasema *"Ukiweza! yote yanawezekana kwake aaminiye*
[1/9, 16:18] ‪+255 762 450 772‬: Kumbe IMANI Na kuamini ni  kitu cha msingi na Yakobo anasema na kule  kuomba kwa IMANI kutamwokoa mgonjwa yule .


Hapa Maombi yametokelewa kwa IMANI kwa mgonjwa ..

Akiulizwa Mungu kumponya

Tunapoomba tunapaswa kuamini nguvu na Uzuri uliopo ndani ya Mungu ( Mk 9:23)
[1/9, 16:24] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya Mapatano / Kuwa wa moja

*Matendo 1:14 Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.*

*Matendo 2:42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.Maisha ya Waumini*


   Maombi haya ni kuungana pamoja na kuomba kwa pamoja


Mnajitoa kwa Pamoja kwa ajili ya kuombea jambo Fulani
Haya *maombi yanatuhamasisha na sisi kuomba Na wengine kwa Pamoja*
[1/9, 16:31] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya kumwomba Mungu kuhusu mahitaji yetu

*Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.*


   Njia mojawapo ya Ushindi wetu ni kupigana vita ya Kiroho "Kuomba kila wakati katika Roho na Kweli

*Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;*
[1/9, 16:37] ‪+255 762 450 772‬: Maombi ya Shukrani

Rejea pia wafilipi 4:6..

Maombi haya pia yanapatikana pia Zaburi mbali mbali

✍Maombi ya kuabudu/Kumfanyia Mungu ibada

Haya ni sawa na ya Shukrani isipokuwa tofauti ya Maombi haya yanalenga kuonyesha Mungu ni nani?,Shukrani na Yaliyofanywa na Mungu


*Matendo 13:2 Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.*
*3 Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.*
[1/9, 16:42] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya kujiweka tayari kutimiza mapenzi ya Mungu ..

Haya yalifanyika na Yesu mwenyewe kabla ya kusulubiwa

*Mathayo 26:39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.*
[1/9, 16:45] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya maombezi /Sala ya maombezi

Haya yanahusu kuwaombea wengine

Ukisoma YOHANA 17 mlango wote utaona jinsi Yesu alivyoomba kwa ajili ya wanafunzi /mitume wake na Waumini wote
[1/9, 16:49] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya kuombea maadui zetu ( Kuwaombea mema)

Sisi kama Kanisa tunazingungukwa na Maadui wengi sana pamoja na hayo inatupasa kuomba kwa ajili yao pia na hatupaswi kuwaombea mabaya bali tunapaswa kuwaombea mema ..


Msaada zaidi soma

Zaburi 7 ,55 na 69
[1/9, 16:53] ‪+255 762 450 772‬: Yesu Kristo mwenyewe alitufundisha /anatufundisha tuwaombee na kuwabariki maadui zetu

Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
[1/9, 16:55] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya kutufungua kwenye  Vifungo mbali mbali


    Haya ni maombi ya kututoa katika vifungo tulivyonavyo au mambo yasiyowezekana mbele ya macho yetu ..

Zaburi 69:1 Ee Mungu, uniokoe,Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.
2 Ninazama katika matope mengi,Pasipowezekana kusimama.Nimefika penye maji ya vilindi,Mkondo wa maji unanigharikisha.
3 Nimechoka kwa kulia kwangu,Koo yangu imekauka.Macho yangu yamedhoofuKwa kumngoja Mungu wangu.
[1/9, 17:00] ‪+255 762 450 772‬: ✍Maombi ya kuleta Ulinzi katika MAISHA yetu
    Haya ni kwa ajili ya kutulinda sisi Na vyote tulivyo navyo


Yeremia 1:18Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii.
*19 Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe.*
[1/9, 17:02] ‪+255 762 450 772‬: ZIPO AINA NYINGI KWA LEO NITAISHIA HIZI CHACHE ...

MWISHO NIKUPE BAADHI YA VIZUIZI VYA MAOMBI

1⃣Dhambi

 Dhambi inafanya maombi yetu yasisikilizwe na Mungu wetu
Isaya 59:1 Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
*2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.*
[1/9, 17:05] ‪+255 762 450 772‬: 2⃣Kuomba vibaya

Yakobo 4:3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.
[1/9, 17:07] ‪+255 762 450 772‬: 3⃣Kutokuwa na IMANI  *1Timotheo 1:19 uwe mwenye imani na dhamiri njema, ambayo wengine wameisukumia mbali, wakaangamia kwa habari ya Imani.*
[1/9, 17:09] ‪+255 762 450 772‬: 4⃣Kutokushukuru

Luka Mtakatifu 17:11 Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
[1/9, 17:12] ‪+255 762 450 772‬: Kutokumshukuru Mungu baada ya kukutendea ya mwanzo inaweza kusabisha usijibiwe yajayo ..


Hitimisho

Maombi ni agizo la Mungu ndio maana anasema *Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.*
[1/9, 17:21] ‪+255 762 450 772‬: Hivyo tukeshe katika maombi siku zote

Na Biblia inasema tuombe katika Roho na kweli

Maombi ni mawasiliano au majibizano na Mungu ambayo hayapaswi Kuwa na kikomo

1Thesalonike 5:16-18 ,Tukue katika UPENDO wa Yesu Kristo na tutakuwa hamu ya kuzungumza naye Daima .


*Bwana ninakushukuru kwa kunipa kibali kusema na Kanisa lako mahali hapa

Ahsante kwa kusema na Roho zetu ,nafsi zetu ns mioyo yetu na MAISHA yetu pia .

Endelea Bwana kutuhudumia mchana na usiku ,Tuhudumie kwa NENO lako daima ,tufundishe na kutuonya na k
NENO lako zaidi ya ya yote tujalie kuitumia NEEMA hii uliyotupa kwa ajili ya kukutumikia na kuutafuta USO wako

Ongoza MAISHA yetu ,njia zetu na mipango yetu

Tawala fikra zetu ,fahamu zetu na mawazo yetu ili Bwana tuyatende mapenzi yako daima .

Tunajikabidhi mikononi mwako  tembea nasi siku zote na kuishi pamoja nasi .

✍KWA NIABA YA WASIONIFAHAMU


NAITWA

Mr ZAWADI NGAILO

Nipo Sikonge TABORA

Kikazi ni

Mwalimu ( IGIGWA secondary )

Mungu amenipa neema ya Kumtumikia Mungu kwa njia ya mitandao hii ya kijamii

N.k nje ya huku ..

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*