URAFIKI UCHUMBA NA NDOA

*πŸ‘«URAFIKI , UCHUMBA NA NDOA* πŸ’

MWL. Peter Francis Masanja

francispeter424@gmail.com

πŸ‘‰πŸΌHatua ya kwanza katika
mahusiano ni

1⃣ URAFIKI

πŸ“–Katika urafiki kila mtu atataka kumfahamu mwenzake

πŸ‘‰πŸΌAnapenda nini

πŸ‘‰πŸΌAnachukia nini

πŸ‘‰πŸΌHali yake ya kiroho ikoje

πŸ…° Ameimarika

πŸ…±Hajaimarika

πŸ‘‰πŸΌAnaishi wapi


πŸ‘‰πŸΌAna wazazi

πŸ‘‰πŸΌAnamchumba


πŸ‘‰πŸΌ Umri wake

πŸ‘‰πŸΌ Elimu yake

πŸ‘‰πŸΌ Anajishughulisha na nini



HAYA NI MASWALI YA KUULIZANA KIPINDI CHA URAFIKI

πŸ“–Kipindi cha urafiki ndicho kipindi cha kumsoma mwenzako kabla ya kufanya maamuzi ya kumwambia ukweli unampenda na unatamani muingie hatua ya pili ya mahusiano

Ambayo ni

πŸ‘‰πŸΌUCHUMBA

πŸ“–Kijana ukiruka hatua ya kwanza ya mahusiano ukakimbilia ya pili utaacha wengi sana

πŸ“–Usiharakie kisa umeona sura tu ukaamua kuanzisha uchumba

Mfanye rafiki kwanza ili upate nafasi ya kumfahamu zaidi

Ukifanya hivyo utapata mke mwema kabisa.

πŸ“– Ukishamfahamu tabia na mwenendo wake sasa unaweza kuingia hatua ya pili ya mahusiano , yaani UCHUMBA

πŸ“– Naongezea katika kipindi cha urafiki

πŸ‘‰πŸΌ mjue anavaaje akiwa kanisani na mtaani

πŸ…°Anavaa nguo zisizomstiri

Je unapenda kumuoa mtu wa namna hiyo ❓

πŸ…± Jitahidi ujue aina ya marafiki zake

Ukishajiridhisha ingia hatua ya pili

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

2⃣UCHUMBA

Katika uchumba unatakiwa uzingatie yafuatayo :

πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ–

HATUA YA PILI YA MAHUSIANO*


πŸ“–UCHUMBA

Uchumba ni nini ❓

πŸ“–Uchumba ni makubaliano ya hiari  ya watu wawili wanaotarajia kuishi pamoja kama mke na mume .

πŸ“– Ndani ya uchumba kuna neno hiari.Hiari maana yake bila kulazimishwa

πŸ“– Uchumba siyo ndoa

πŸ“–Hivyo msifanye mambo ya wanandoa kabla ya ndoa

πŸ“–KANUNI ZA UCHUMBA

πŸ‘‰πŸΌZingatieni utakatifu

πŸ…° Msizini

πŸ‘‰πŸΌzungatieni kuwa tendo la ndoa ni kwa wanandoa tu

πŸ“–πŸ– Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.

Mithali 22:3
Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.

Mithali 27:12


πŸ“–Nimekupa hayo maandiko ujue kuwa ukiona ubaya usilazimishe usije ukaendelea ukaumia

πŸ“–Kwa tamaa za mwili kila mwanaume anafaa kuwa mume

Lakini kwa kuangalia  kanuni za Mungu siyo kila mwanaume anakufaa haijalishi ameokoka πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–πŸ“–

πŸ“– Kama nilivyosema mwanzoni kuwa uchumba ni jambo la kujichunga sana ili msiende kinyume na mpango wa Mungu

πŸ“–HASARA ZA KULALA PAMOJA ( KUJUANA KIMWILI KABLA YA NDOA

1⃣ Binti lazima utachukiwa NA kuonwa mchafu

πŸ“–πŸ– 14 Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.
2 Samweli 13 :14

15 Kisha Amnoni

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡
akamchukia machukio makuu sana; kwa kuwa machukio aliyomchukia yakawa makuu kuliko yale mapenzi aliyokuwa amempenda kwanza. Amnoni akamwambia, Ondoka, nenda zako.
2 Samweli 13 :15

πŸ“–Mwone Tamari alipokubali kulala na Amnoni alichukiwa sana

πŸ“–πŸ– 8 Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.
Maombolezo 1 :8
πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡
9 Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza.
Maombolezo 1 :9

10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako.
Maombolezo 1 :10

ASOMAYE NA AJIFUNZE

β›ͺβ›ͺβ›ͺβ›ͺβ›ͺβ›ͺβ›ͺβ›ͺ

Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*