URAFIKI UCHUMBA NA NDOA

*👫URAFIKI , UCHUMBA NA NDOA* 💍

MWL. Peter Francis Masanja

francispeter424@gmail.com

👉🏼Hatua ya kwanza katika
mahusiano ni

1⃣ URAFIKI

📖Katika urafiki kila mtu atataka kumfahamu mwenzake

👉🏼Anapenda nini

👉🏼Anachukia nini

👉🏼Hali yake ya kiroho ikoje

🅰 Ameimarika

🅱Hajaimarika

👉🏼Anaishi wapi


👉🏼Ana wazazi

👉🏼Anamchumba


👉🏼 Umri wake

👉🏼 Elimu yake

👉🏼 Anajishughulisha na nini



HAYA NI MASWALI YA KUULIZANA KIPINDI CHA URAFIKI

📖Kipindi cha urafiki ndicho kipindi cha kumsoma mwenzako kabla ya kufanya maamuzi ya kumwambia ukweli unampenda na unatamani muingie hatua ya pili ya mahusiano

Ambayo ni

👉🏼UCHUMBA

📖Kijana ukiruka hatua ya kwanza ya mahusiano ukakimbilia ya pili utaacha wengi sana

📖Usiharakie kisa umeona sura tu ukaamua kuanzisha uchumba

Mfanye rafiki kwanza ili upate nafasi ya kumfahamu zaidi

Ukifanya hivyo utapata mke mwema kabisa.

📖 Ukishamfahamu tabia na mwenendo wake sasa unaweza kuingia hatua ya pili ya mahusiano , yaani UCHUMBA

📖 Naongezea katika kipindi cha urafiki

👉🏼 mjue anavaaje akiwa kanisani na mtaani

🅰Anavaa nguo zisizomstiri

Je unapenda kumuoa mtu wa namna hiyo ❓

🅱 Jitahidi ujue aina ya marafiki zake

Ukishajiridhisha ingia hatua ya pili

👇👇👇👇👇👇👇

2⃣UCHUMBA

Katika uchumba unatakiwa uzingatie yafuatayo :

📖📖📖📖📖📖📖🖍

HATUA YA PILI YA MAHUSIANO*


📖UCHUMBA

Uchumba ni nini ❓

📖Uchumba ni makubaliano ya hiari  ya watu wawili wanaotarajia kuishi pamoja kama mke na mume .

📖 Ndani ya uchumba kuna neno hiari.Hiari maana yake bila kulazimishwa

📖 Uchumba siyo ndoa

📖Hivyo msifanye mambo ya wanandoa kabla ya ndoa

📖KANUNI ZA UCHUMBA

👉🏼Zingatieni utakatifu

🅰 Msizini

👉🏼zungatieni kuwa tendo la ndoa ni kwa wanandoa tu

📖🖍 Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.

Mithali 22:3
Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.

Mithali 27:12


📖Nimekupa hayo maandiko ujue kuwa ukiona ubaya usilazimishe usije ukaendelea ukaumia

📖Kwa tamaa za mwili kila mwanaume anafaa kuwa mume

Lakini kwa kuangalia  kanuni za Mungu siyo kila mwanaume anakufaa haijalishi ameokoka 📖📖📖📖📖📖

📖 Kama nilivyosema mwanzoni kuwa uchumba ni jambo la kujichunga sana ili msiende kinyume na mpango wa Mungu

📖HASARA ZA KULALA PAMOJA ( KUJUANA KIMWILI KABLA YA NDOA

1⃣ Binti lazima utachukiwa NA kuonwa mchafu

📖🖍 14 Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.
2 Samweli 13 :14

15 Kisha Amnoni

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
akamchukia machukio makuu sana; kwa kuwa machukio aliyomchukia yakawa makuu kuliko yale mapenzi aliyokuwa amempenda kwanza. Amnoni akamwambia, Ondoka, nenda zako.
2 Samweli 13 :15

📖Mwone Tamari alipokubali kulala na Amnoni alichukiwa sana

📖🖍 8 Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.
Maombolezo 1 :8
👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
9 Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza.
Maombolezo 1 :9

10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako.
Maombolezo 1 :10

ASOMAYE NA AJIFUNZE

⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪

Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*