IJUE THAMANI YA ZAWADI
*ITUNZE NA KUIPENDA ZAWADI ULIYOPEWA*
Mwl.Peter Francis Masanja .
067392829
The Voice of God Ministry
*Bwana Yesu asifiwe*
Leo napenda tujifunze kuhusu thamani ya zawadi katika maisha yetu .
Zawadi ni kitu chochote ambacho utakipokea kutoka kwa mtu kama sehemu ya kujenga mahusiano maziri .
Zawadi ni zawadi tu hata iwe ndogo ni zawadi tu
Unapopewa zawadi maana yake ni kwamba huyo akupaye zawadi anakupenda , anakujali , na anakuthamini sana.
Zufuatazo ni zawadi ambazo Mungu alitupatia
1⃣ *UUMBAJI*
24 Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo.
Mwanzo 1 :24
25 Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Mwanzo 1 :25
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mwanzo 1 :26
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
Mwanzo 1 :27
28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
Mwanzo 1 :28
29 Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;
Mwanzo 1 :29
30 na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.
Mwanzo 1 :30
Mungu alituubia vitu vyote kama zawadi kwetu ili tuvitumie.
Hata kumwumba mwanadamu ilikuwa ni zawadi kwake Mungu .
Kwahyo uumbaji ni zawadi tosha kabisa , ulivyoumbwa na Mungu jithamini sana.
13 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu.
Zaburi 139 :13
14 Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana,
Zaburi 139 :14
15 Mifupa yangu haikusitirika kwako, Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi;
Zaburi 139 :15
16 Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.
Zaburi 139 :16
2⃣ *MAISHA*
Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Mwanzo 2:7
Pumzi tuliyopewa ni zawadi tosha kabisa .
3⃣ *MAHUSIANO NA WATU WENGINE*
3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?
Amosi 3 :3
Watu unaosaidiana nao ni zawadi toka kwa Mungu .
Mke uliyenaye au mime uliye naye ni zawadi ambayo Mungu kakupa mtunze , mpende , mjali na kumwona mzuri kila Siku.
4⃣ *YESU KRISTO NA KIFO CHAKE MSALABANI*
hii ni zawadi kubwa kuliko zote ambayo Mungu alitupatia maana kufa kwake msalabani tumepokea uzima wa milele
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Yohana 3 :16
Pia kufa kwake msalabani tumefanyika wana wa Mungu .
32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?
Warumi 8 :32
Kwahyo zawadi yoyote upewayo ni ya thamani sana .
Mungu akubariki sana .
https://peterfrancismasanja.blogspot.com
Maoni
Chapisha Maoni