KUMTAMBUA ALIYE NA VITA YA UKOO

*KUMTAMBUA MTU MWENYE VITA YA KIUKOO *

Mwlm.Peter Francis Masanja

Mtwara _Tanzania

francispeter424@gmail.com



Inawezekana kuna mpendwa ameokoka peke yake katika ukoo wake au familia yake

Mtu ambaye kaokoka kutoka kwenye familia za wasiookoka huwa na vita kali sana .

Mtu huyo hufuatiliwa sana na mashambulizi ya miungu ya ukoo na wakati mwingine kutafta kumuua kabsa

 Kamba za mauti zilinizunguka, Shida za kuzimu zilinipata. Naliona taabu na huzuni;

Zaburi 116:3

mtu aliyeokoka kwenye familia ambazo wanaabudu mizimu anahitaji asimame sana katika maombi ili anusurike na miungu ya ukoo

Lazima atambue kuwa kama alishawahi kuchanjwa chale na kula chakula cha matambiko ajue kuwa hizo ni kamba amefungiwa na inabidi azikate ( azifungue ) na kuzitupa

Kamba hizo lazima zifunguliwe kwa njia ya toba na maombi .

 Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.

Isaya 10:27

Elewa pia kuwa mtu huyo amefungiwa nira na miungu ya ukoo hivyo basi inabidi iondolewe na njia pekee ya kuiondoa ni maombi .

_DALILI ZA MTU ALIYE KWENYE VITA YA UKOO

1⃣ Kuota ndoto unafanyishwa kazi nyumbani ulikozaliwa .

2⃣Kutokuelewana na ndugu zako

3⃣ Kudhihakiwa na ndugu zako

4⃣ Kuota unakimbizwa na nyoka au unatumbukia shimoni

5⃣ kuota ndugu zako wanatambika

6⃣Kuota unagombana na ndugu zako

 Hizi ni baadhi ya viashiria vya kuwa mtu yupo kwenye vita na miungu ya ukoo .

Watu ambao nyumbani kwao au katika ukoo wao kuna mbuzi au ng'ombe wamepewa majina ya watu na kufungwa kengele huwa wanapata tabu sana kiroho .

Utakuta jina la ukoo unaloitwa kuna mbuzi au ng'ombe anaitwa jina hilo hilo na wamemfanya huyo mnyama kama njia ya kufikisha maombi yao kwa miungu ya ukoo .

SULUHISHO JUU YA VITA VYA UKOO

1⃣ MAOMBI YA TOBA.

Toba kwaajili yako mwenyewe

*SOMA SALA HII*

‍BWANA YESU asante kwa damu yako iliyomwagika msalabani kwaajili yangu .

‍Nimekuja mbele yako Mungu mwenye enzi yote na mamlaka yote , ninatubu dhambi zangu zote nilizozitenda kwa makusudi na pasipo makusudi .

‍Kwa damu ya Yesu naomba unioshe na kunisafisha na kila uovu nilioutenda katika maisha yangu eeh Mungu utakasaye ( Jehovah maccadeshem ).

‍Nakusihi ulifute jina langu kwenye kitabu cha hukumu nakuliandika jina langu kwenye kitabu cha uzima wa milele.

‍Lifute jina langu kwenye kitabu cha laana na uliandike kwenye kitabu cha baraka kwa jina la Yesu.

‍Kuanzia leo ninatoa mwili wangu ,nafsi yangu na roho kwako ee Bwana Yesu.

‍ Roho Mtakatifu karibu ndani yangu na uweza wako unipe nguvu za kushinda dhambi kwa jina la Yesu .AMEN

 Toba kwa ajli ya waliokutangulia ( wazazi , babu na bibi )

Kumbuka toba hii ni pande mbili yaani ukoo wa baba na ukoo wa mama yako

‍ 29 Huoni jinsi Ahabu alivyojidhili mbele yangu? Basi kwa sababu amejidhili mbele yangu, sitayaleta yale mabaya katika siku zake; ila katika siku za mwanawe nitayaleta mabaya hayo juu ya nyumba yake.

1 Wafalme 21 :29

 Mwangalie Ahabu alipotubu utajifunza kitu kizuri sana kuhusiana na toba

Unapotubu unapangua mabaya yasikupate

 Unapotubu juu ya waliokutangulia unapangua mabaya ya kurithi yasikupate kabisa

Ikiwa ni magonjwa , mikosi na kila aina ya laana mfano kutokuolewa au kutokukaa kwenye ndoa ukafurahia
Haya yote ni mabaya yanahitaji toba .

Inawezekana ndoa yako inasumbua au uchumi wako unasumbua sana kumbe tatzo ni waliokutangulia na cha ajabu umeyarithi mabaya yao .

‍ 7 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.

Maombolezo 5 :7

Lazima ujitenge na uovu wa baba zako na mababu zako pia ili uweze kufanikiwa
[3/9, 11:53] Rev.Peter Francis: *SOMA SALA HII

‍BWANA YESU ninakuja mbele zako masihi .

‍Ninazileta mbele zako  dhambi za baba yangu na mama yangu pamoja babu zangu wa upande wa baba na mama yangu.

‍Ninatubu na kuziungama dhambi zao , kwa maana walikutenda dhambi .

‍Naziungama dhambi zao zote za kuua binadamu wezao , kuabudu sanamu, kuuza na kununua wanadamu, kutoa kafara za watu kwa miungu ya sanamu, kula nyama za watu , uasherati, uzinzi na kila matendo ya giza waliyoyafanya .

‍ Nakusihi uwarehemu na kuwahurumia juu ya uovu walioutenda .

‍Ninawasamehe makosa yote waliyonitendea kwa kujua na kutokujua katika jina la Yesu .
Ninaomba uzisahau dhambi yao yote katika kizazi changu .

‍Baba siyapendelei makosa na uovu wao wote , kwahiyo ninajitenga mwenyewe kutoka kwenye adhabu ya makosa hayo ee Bwana kama ilivyoandikwa :

✍ 20 Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.

Zaburi 68 :20

Nakuomba Mungu unitoe kwenye mauti ya dhambi zao katika jina la Yesu.AMEN

Toba kwa ajili ya watoto wako na uzao wako

‍ 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu;

✍✍✍✍✍✍✍✍
nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

Kutoka 20 :5

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Kutoka 20 :6

 Tubu juu ya watoto wako na uzao wako ili uwe na kizazi kizuri

https://peterfrancismasanja.blogspot.com


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*