MUNGU AKUONGOZE

*📖💻MUNGU AKUONGOZE 📖📖*

Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829

The Voice of God Ministry





📖 Bwana, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.

Isaya 48:17

👉Siku zote bila Mungu huwezi kuwa na dira nzuri ya maisha .

👉Utakuwa unatembea bila kujua unaelekea wapi

👉 Utakuwa hupati faida yoyote ya uumbaji ambao Mungu alikupatia ili uishi hapa duniani .

💫 Nakuombea kwa Mungu ili maisha yako yamtegemee yeye katika kila jambo ulifanyalo.

👉Unataka upate faida katika jambo fulani ? Anza na Mungu kwanza ili aachilie kibali .

💫 Unataka utajiri ?

Mwangalie Mungu katika miradi yako yote ili akupe nguvu ya kuupata huo utajiri .

📖💻 17 Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.
Kumbukumbu la Torati 8 :17

18 Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Kumbukumbu la Torati 8 :18

👉nguvu ya kupata utajiri ipo kwa Mungu peke yake

👉Utajiri unaopewa na Mungu ni wa kudumu .

👉Utajiri kutoka kwa shetani siyo wa kudumu .

📖💻 8 Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu, asema Bwana wa majeshi.

Hagai 2 :8

👉Mungu amekuandalia kila kitu lakini anahitaji umtumikie ili akupe .

Mungu akubariki sana

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*