MUNGU NDIYE MLINZI WAKO

📖 MUNGU NDIYE MLINZI WAKO

Mwlm.Peter Francis Masanja

Mtwara _ Tanzania

📖💻 7 Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
Zaburi 121 :7

8 Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Zaburi 121 :8

👉Kuna watu tuna walinzi wetu tumewaweka lakini hawawezi kulinda roho zetu

👉 Mwanadamu hawezi kulinda roho yako ila Mungu analinda roho yako.

👉unatakiwa umtegemee sana Mungu akulinde kuliko kuwategemea wanadamu ambao hawawezi kukulinda na magonjwa wala hawawezi kukuepusha na ajali.

👉Ni jambo la aibu kumsahau Mungu na kutegemea ulinzi wa wanadamu tena ni laana .

📖💻 5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.

Yeremia 17 :5

👉Mtegemee Mungu katika kila jambo ili uwe salama.

👉 Utategemea mganga wa kienyeji ambaye anakufa mpaka lini ❓

Yupo Mungu aliye hai milele ndye mlinzi wako .

📖📖📖📖📖📖📖📖📖📖📖

Mungu akubariki sana

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*