NGUVU YA KUISHINDA DHAMBI

*πŸ”₯NGUVU YA KUISHINDA DHAMBI πŸ”₯*

πŸ’«DAY ONE πŸ”₯

Mwlm.Peter Francis Masanja

0679392829

The Voice of God Ministry

πŸ“–πŸ’» Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake;

Warumi 6:12

πŸ‘‰Mpendwa ili mtu aweze kuishinda dhambi lazima atambue kuwa amepewa mamlaka ya kuishinda dhambi

πŸ‘‰Na mamlaka ya kuishinda dhambi yamo ndani ya Yesu .

πŸ“–πŸ’» 5 Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake.
1 Yohana 3 :5

6 Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua.
1 Yohana 3 :6

πŸ‘‰ Kanuni kuu ya kushinda dhambi ni kukaa ndani ya Yesu .

πŸ‘‰Yesu alikuja duniani kuzivunja hila zote za shetani maana shetani ndiye mwanzilishi wa dhambi na baba wa uovu wote duniani .

πŸ’»πŸ“– 8 atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.

1 Yohana 3 :8

πŸ‘‰Kwahiyo inakupasa umkaribishe Yesu akae ndani yako ili usitende dhambi .

πŸ‘‰Ukikaa ndani ya Yesu kuna uzima na unafanyika kuwa mwana wa Mungu.

πŸ’»πŸ“– 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.

1 Yohana 3 :9

10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

1 Yohana 3 :10

πŸ‘‰Mpendwa dumu sana katika kusoma neno na kulifanyia kazi ili uweze kufanikiwa kumshinda shetani na kazi zake

Mungu akubariki sana

Nitaendelea siku nyingine .

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*