URAFIKI,UCHUMBA NA NDOA

*🌹🌹MFANYE AWE WAKO PEKE YAKO TU👫😘*


Mwl.Peter Francis Masanja


The Voice of God Ministry

0679392829

🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹🌹

Bwana Yesu asifiwe

🌹kuna mwimbaji aliimba tumeagizwa upendo

🌹mwimbaji huyo hajakosea kabisa.

🌹👫 25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

Waefeso 5 :25

26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

Waefeso 5 :26

27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

Waefeso 5 :27

28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.

Waefeso 5 :28

29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.

Waefeso 5 :29

🌹Mwanamke anahitaji kuonyeshwa upendo.

🌹Mwanamke anahitaji kusifiwa .

👉Msifu mkeo mwambie ni mzuri unafrahi ukimwona .

👉Mwambie yeye ni mzuri kuliko wanawake wote duniani .

🌹👫 29 Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.

Mithali 31 :29

👉Msifu mkeo ili akufrahie.

🌹Mwite majina matamu huku ukimwambia unampenda sana na  kumwaminisha kuwa yeye ni wa thamani sana maishani mwako.

Mfano :

Mpenzi , wewe ni wa thamani sana maishani mwangu  , nikikukumbuka huko kazini natabasamu tu  , uzuri wako wanifanya nizidi kukuona mpya kila iitwapo leo , nakupendaa baby .

🌹Mwanamke anapenda kiss ( busu )

👉Jitahidi kumpatia kiss mkeo siyo mpaka akwambie unaweza kumfanyia kama surprise huku unaonyesha tabasamu .

Hapo ndoa yako au uchumba wako utadumu sana.

🌹Kuwa na mazoea ya kukaa na mke wako siti moja au kaa karibu naye ongea naye na ikibidi mshike mkono , mtizame hata usoni.

Hii humfanya mwanamke akufrahie sana .

🌹Uwe na mazoea ya kumkumbatia mkeo huku ukisema wampenda .

🌹Mfanye mkeo acheke , mwanamke anahitaji kuchekeshwa , yaani utani huku ukimsifu ikibidi mshikeshike nywele zake.

🌹Cheza na mkeo , na wakati mwingine mbebe 👫

🌹👫 Ikawa alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, akachungulia dirishani,
✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻

*akamwona Isaka anacheza-cheza na Rebeka mkewe.*

Mwanzo 26:8

👉Shetani hupiga vita ndoa za waliookoka , kwahyo msipokaa vizuri kwenye maombi hayo hutokea .

✍🏻✍🏻 4 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.
Ufunuo wa Yohana 2 :4

5 Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu.

Ufunuo wa Yohana 2 :5

🌹Mke mjue anapendelea nini au anavaa size gani nguo za ndani 👙

Anavaa kiatu namba ngapi 👠

✍🏻hivyo vitu mletee hivi vitu kama surprise.

🌹Usisubiri eti akwambie , hata kama anauwezo wa kujinunulia nguo mletee atakuona wewe unampenda na kumjali sana.

👉Tatizo mnashindwa kuwasoma wake zenu wanapenda nini hii itawaumiza

👉Mwanaume hujui hata mkeo anavaa chupi namba ngapi kazi kumfunua tu 😨😨😨

✍🏻Unashindwa kujua mkeo anavaa size gani kiunoni mmmmh aiseeee ✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻

👉Umejua anapendelea rangi gani ❓👫🌹🌹

📖💻 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao,

.✍🏻📖 *wasio na shukrani* ,

wasio safi,

2 Timotheo 3 :2

3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,

2 Timotheo 3 :3

4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;

2 Timotheo 3 :4

5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

2 Timotheo 3 :5

🌹mke asiye na shukurani huyo siyo mke anaweza kuwanyima chakula hata ndugu zako .

🌹Mwachie mkeo pesa ya matumizi

👉Hii pia humfanya mke atulie kwako daima

👉Haijalishi mkeo anakazi wewe acha hela ya matumizi

✍🏻kuna vitu vingne mletee bila yeye kumtaarifu ,

👉Af ndoa ni tamu mkiwa mnacheka na mkeo.

Ubarikiwe sana

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*