BWANA AONGOZE HATUA ZAKO

🌐 BWANA AKUFUNDISHE NA AONGOZE HATUA ZAKO🌐

Mwlm.Peter Francis Masanja

0679392829

The Voice of God Ministry

💻 8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

Zaburi 32 :8

💫 Uamkapo asbh hii kuelekea kazini , masomoni , na katika huduma , mwambie Mungu aongoze hatua zako

💫 Mwambie Mungu nifundishe na uniongoze katika kila jambo nilifanyalo kwa utukufu wako .

💫Mwambie Mungu aitazame kazi yako , ailinde na kupitia kazi hiyo ukuu wake ukaonekane.

💫Ahadi za Mungu ni za kweli akisema atafanya jambo maishani mwako anafanya kwelikweli.



*💒TUOMBE* 💒

Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu , baba wa mbinguni , Bwana wa majeshi , Mungu wa miungu .

Tunaliinua jina lako na kushukuru tukisema asante kwa kutujalia afya na uzima na kutupa zawadi kuu ya kuiona siku nyingine iitwayo leo .

Mungu ,ahadi zako ni za haki na kweli ukiahidi utatenda jambo maishani mwetu wewe unafanya .

Na sasa tunakuja mbele zako asbh hii tukikuomba utufundishe , utuongoze na ututazame katika kila jambo tutakalolifanya .Maana umeahidi utafanya .

Watazame wasafiri na watu wenye shida mbalimbali ukawaongoze ee Mungu .

Zitazame nchi mbalimbali katika dunia hii ukaachilie amani na kuondoa roho za madaraka na umwagaji wa damu zisizokuwa na hatia .

Katika jina lipitalo majina yote la Bwana Yesu Kristo tunaomba yote haya tukiamini utayafanya .

Amen


https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*