GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA 🌐

🌐GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA 🌐




SIKU YA SABA





Mwl. Peter Francis Masanja


0679392829



The Voice of God Ministry


πŸ’» 9 Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? 

Mwanzo 4 :9

10 Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. 

Mwanzo 4 :10

11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; 

Mwanzo 4 :11

12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. 

Mwanzo 4 :12






Bwana Yesu apewe sifa.



πŸ’« Kumekuwa na mambo mengi yanayomfanya mtu asifikie maisha ambayo Mungu anataka aishi .


πŸ’« Katika siku ya kwanza mpaka ya sita tumejifunza mambo mengi ambayo yamekuwa ni giza linalomzuia mtu asione baraka za Mungu .


πŸ’« Katika siku hii ya saba na ya kuhitimisha somo hili tutaangalia jambo lingine linalomzuia mtu asione baraka za Mungu .



 _🌐 UMWAGAJI WA DAMU ISIYOKUWA NA HATIA_


πŸ’« Hakuna jambo linalomfanya mtu asifanikiwe kama kumwaga damu isiyokuwa na hatia .


πŸ’» 9 Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? 

Mwanzo 4 :9

10 Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. 

Mwanzo 4 :10

11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; 

Mwanzo 4 :11

12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. 

Mwanzo 4 :12





πŸ’«. Tukimwangalia Kaini alivyomwua ndugu yake , tunaona jinsi damu ya ndugu yake ilivyokuwa ikidai haki kutoka kwenye ardhi .



πŸ’« Ardhi inaweza kufunga maisha ya mtu asifanikiwe , hii ni kwasababu ardhi ni lango linalopitisha laana au baraka kwa mtu .




πŸ’«Kaini  alipomwaga damu ya ndugu yake tunaona ardhi haikumzalia matunda ( kumletea mafanikio) .




➡ Jambo lingine ni utoaji wa mimba




πŸ‘‰πŸ» kutoa mimba pia ni umwagaji wa damu isiyokuwa na hatia na pia ni uuaji wa kiumbe cha Mungu kisichokuwa na hatia .


πŸ’« Umwagaji wa damu unamfanya mtu asiuone ufalme wa Mungu ( uzima wa milele ) .


πŸ’« Ukitoa mimba na ukanyamazia hiyo hali uendelee nayo bila kuitubia inatakuletea shida sana katika maisha yako .


πŸ‘‰πŸ»Ukitoa mimba unaweza kusababisha yafuatayo maishani mwako na kizazi chako


1⃣ roho ya kuharibu mimba


2⃣ roho ya utasa



3⃣ roho ya kutokuolewa.


πŸ‘‰πŸ»  utashangaa binti zako hawaolewi kumbe damu uliyoimwaga imewafunga wanao .

4⃣ Kushindwa kuurithi ufalme wa mbinguni .


πŸ‘‰πŸ» Usipotubu utawekwa hukumuni kutolea hesabu ya damu ya mtoto uliyoimwaga siku ulipotoa mimba .


πŸ’« Damu pekee iliyona kibali cha kumwagika ni damu ya Yesu pekee ndyo iliyopata kibali iyafuye makosa yetu.


Lakini kumwaga damu ya mtu ni kujiandalia makao ya jehanamu.


➡ Lakini usiogope maana Mungu anasamehe kila dhambi isipokuwa ya kumkufuru roho Mtakatifu .


πŸ’» 28 Amin, nawaambia, Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote;

Marko 3 :28

29 bali mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hana msamaha hata milele; ila atakuwa ana dhambi ya milele,

Marko 3 :29



πŸ’« Umeua au umetoa mimba usikae na hiyo dhambi itakuzuia kufanikiwa tubu .


πŸ’» Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

Mithali 28:13


πŸ’«.Kwahiyo bado kuna nafasi ya kufanya toba mbele za Mungu na kurudisha uhusiano wako na Mungu kupitia damu ya Yesu .

πŸ‘‰πŸ» usiiangalie hiyo dhambi ukakosa amani mwangalie Mungu afutaye dhambi .


πŸ’» 18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. 

Isaya 1 :18

19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi; 

Isaya 1 :19


πŸ’« Mungu ni mwenye rehema kubali kutubia dhambi ya umwagaji wa damu isiyokuwa na hatia ili ufanikiwe .




πŸ’» 1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. 

Zaburi 51 :1

2 Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. 
Zaburi 51 :2

3 Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. 

Zaburi 51 :3

4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu. 

Zaburi 51 :4

5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani. 

Zaburi 51 :5

6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; Nawe utanijulisha hekima kwa siri, 
Zaburi 51 :6

7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji 


Zaburi 51 :7

8 Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi. 

Zaburi 51 :8


➡ HITIMISHO

Umwagaji wa damu ni giza linaloweza likamfanya Mungu asifanikish
e njia zako .


Mungu akubariki sana



https:/peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*