GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA

🌐 GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA 🌐



SIKU YA TATU

Mwlm.Peter Francis Masanja


The Voice of God Ministry

Bwana Yesu asifiwe

Karibu tuendelee tena na somo letu hili ikiwa leo ni siku ya tatu .

👉 Kuna mambo ambayo waliookoka yamekuwa giza kwao hata yamewafanya wasione baraka za  Mungu maishani mwao .

👉 Matendo yanayokuzuia Mungu asikujibu maombi au asikubariki ni giza kwako linalokuzuia usipokee baraka kwa Mungu .


✍🏻Leo tuangalie giza lingine linalowazuia watu kuzipata baraka za Mungu .

*KUTOKUSAMEHE

💻 25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.

Marko 11 :25

26 Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]

Marko 11 :26

💫 Naomba nikukumbushe kuwa msamaha ni jambo kuu sana ambalo Mungu analiangalia katika maisha ya mwanadamu.

💫Kama yeye Mungu alivyo na tabia ya kusamehe na kusahau ndivyo ilivyo na kwa mtu

💫 Kutokusamehe ni dhambi mbele za Mungu dhambi hii inakufanya wewe ukose baraka za Mungu maishani mwako .

💫 Hata hivyo napenda kugusia juu ya sala ambayo wakristo wengi tunakiri tukisema .


" utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe waliotukosea "


Jiulize mpendwa je , nimesamehe walionikosea ❓
Ndipo mwambie Mungu , " unisamehe makosa yangu kama ninavyowasamehe wanaonikosea "


💻 12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

Mathayo 6 :12


💫Katika huu mstari tunajifunza kusamehe kwanza ili Mungu atusamehe .


💻 14 Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.

Mathayo 6 :14

15 Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

Mathayo 6 :15


💫 Ni nini basi leo nataka ujifunze , nataka ujifunze kuwa usiposamehe Mungu hawezi kukubariki kirahisi rahisi .

💻 4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu].

Luka 11 :4

💫 Tujifunze kwamba mtu yeyote asiyesamehe bado yupo mikononi mwa shetani kwahyo inabidi aing'oe roho ya kutokusamehe ili Mungu amsamehe na kumrejesha kwake .

💫 Imekuwaje basi kutokusamehe liwe ni Giza linalozuia baraka za Mungu kukufikia ❓

Jibu ni kwamba kazi ya giza ni kumzuia mtu asione anachokitafta .Au ni nani aliyewahi kutafta sindano gizani akaiona ?

Kwahiyo kutokusamehe kunamfanya mtu asione baraka za Mungu .Hii ni kwa sababu kutokusamehe ni dhambi na dhambi ndiyo giza .

💻 3 Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.

Luka 17 :3

4 Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.

Luka 17 :4

💫. Jifunze kusamehe na kusahau ili Mungu akubariki .

✍🏻 Msamaha ni jambo la msingi sana maishani mwako na kama uliapa kutokumsamehe mtu basi futa maneno yako na uachilie msamaha ili Mungu akusamehe pia .

💫 Kusamehe ni njia inayomfanya mtu aone baraka za  Mungu haraka sana .

💫 Anayesamehe ana furaha , amani na upendo moyoni mwake .Na ijulikane kuwa Mungu anapenda moyo wenye furaha .


💫Wengine ni wapendwa wanasali kanisa moja lakini walikwazana na hawataki kusalimiana kabisa na ibadani hushikana mikono kwa unafiki , watu kama hao hawawezi kuona baraka za Mungu maishani mwao mpaka wasameheane .Na hata hivyo ijapokuwa wanatoa sadaka sadaka yao ni uchafu mbele za Mungu maana inanena dhambi .

💻 23 Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,

Mathayo 5 :23

24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako.

Mathayo 5 :24

25 Patana na mshitaki wako upesi, wakati uwapo pamoja naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi, na kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani.

Mathayo 5 :25

💫Liondoe giza la kutokusamehe ili uone baraka za Mungu .

Mungu akubariki sana

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*