GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA

🌐GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA 🌐

SIKU YA TANO

Mwlm. Peter Francis Masanja

0679392829

The Voice of God Ministry

💫Bwana Yesu asifiwe .

Karibu sana katika mwendelezo wa somo letu nakukaribisha tuendelee kujifunza katika jina la Baba , mwana na Roho Mtakatifu .Amen

💫 Lifuatalo ni giza lingine linalomzuia mtu kupata baraka kutoka kwa Mungu .



🌐 KUTOKUKAA NDANI YA YESU 💫


💻 Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;

Yohana 8:31

➡ Ukikaa ndani ya Yesu kunafaida kubwa sana .

➡ Maana kuu ya kukaa ndani ya Yesu ni kuyavaa matendo yake na kutii neno la Mungu kwa uaminifu huku ukilifanyia kazi .

💻 22 Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.

Yakobo 1 :22

23 Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo.

Yakobo 1 :23

➡ Neno la Kristo likikaa ndani yako utapokea mambo mengi sana kutoka kwa Mungu .

➡. Siyo tu neno likae kwa wingi pia inabidi neno lilokaa ndani yako ulifanyie kazi ili lilete mabadiliko .

💻 4 Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

Yohana 15 :4

5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

Yohana 15 :5

6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.

Yohana 15 :6

7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Yohana 15 :7


➡ Ili Mungu akustawishe katika huduma yako au utumishi wako pamoja na mambo yako yote , anakutaka ukae ndani ya Yesu kwanza .


➡ Ukikaa ndani ya Yesu umekaa katika neno na hilo neno litakaa ndani yako na neno hilohilo litaruhusu baraka za Mungu kukufikia kwa wingi.


💻 16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

Wakolosai 3 :16

17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

Wakolosai 3 :17


➡ Kukaa ndani ya Yesu pia inamaanisha kuishi maisha matakatifu .

💻 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;

1 Petro 1:15

➡ Maisha ambayo Mungu anamtaka mkristo aishi ni maisha matakatifu  maana yeye ni mtakatifu .

➡.    Na utakatifu ni kudhirisha kuwa Kristo anakaa ndani yako.


➡Tukikaa ndani ya Yesu tutakuwa tumekaa nuruni na siyo gizani tena.


💻 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.

1 Yohana 1:7

➡.  Tukikaa nuruni yaani ndani ya Yesu tutakuwa tumeliondoa giza linalotuzuia kupata baraka za Mungu .

Mungu akubariki sana


https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*