GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA

🌐GIZA LINALOZUIA BARAKA ZA MUNGU KUKUFIKIA 🌐

SIKU YA SITA

Mwlm. Peter Francis Masanja

0679392829

The Voice of God Ministry

Bwana Yesu asifiwe.

Karibu tena katika mwendelezo wa somo letu .

💫kama tulivyotangulia kusema kuna mambo ambayo yanamfanya mtu asione matokeo ya kile ambacho Mungu kakusaidia ndani yake.

➡Giza lingine linalomzuia mtu asione baraka za Mungu maishani mwake ni ;

🌐KUJITAMKIA AU KUTAMKIWA MANENO MABAYA

💻 2 Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,

Mithali 6 :2

👉🏻 kujitamkia maneno ya kushindwa jambo fulani kulifanya kunamfanya mtu aishi maisha ya kushindwa kufanikiwa kwa sababu amejifungia kufanikiwa .

👉🏻 Maneno mabaya yanakamata mfumo wa maisha ya mtu na kumfanya aishi kulingana na alivyotamka.

💫 Leo kuna changamoto nyingi sana na matatizo mengi kwenye ndoa kwa sababu vijana wengi wamejitamkia maneno mabaya kabla ya ndoa.

👉🏻 Utasikia kijana anasema naolewa tu ili nitoe aibu lakini ndoa ni ngumu sana , mpendwa kama unaingia kwenye ndoa na wazo la kuwa ndoa ni ngumu ndoa yako itakuwa ngumu .

👉🏻 Neno lolote unalojinenea ni mbegu inayoota maishani mwako na mwisho wake utakuja uvune ulichokipanda

Ukipanda kushindwa utavuna kushindwa .

💫 Wengine walijitamkia sitakaa niolewe lakini wakaolewa ,na sasa ndoa zao zipo kwenye hatari ya kuvunjika kwa sababu ya maneno mabaya waliyojitamkia .

💻 20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake.

Mithali 18 :20

21 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.

Mithali 18 :21

👉🏻 Unaona jinsi gani maisha ya mtu yanabebwa na neno analojitamkia .

💫Vijana wengi walishindwa kufanikiwa kwa sababu ya maneno yao mabaya

Anajitamkia Mimi ni maskini , mimi siwezi , mimi wa hivyohivyo , n.k

Sasa haya matamko yanamzuia Mungu kumbariki kwasababu tayari huyu mtu amejitia vifungoni mwenyewe na roho ya kushindwa .

💻 4 Je! Umetamka maneno kwa nani? Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako?

Ayubu 26 :4

👉🏻 neno ni roho , na mtu akijitamkia kushindwa atakuwa amekamatwa na roho ya kushindwa .

👉🏻  Ukumbuke kuwa vitu vyote viliumbwa kwa neno ,.

💻 1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

Yohana 1 :1

2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
Yohana 1 :2

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

Yohana 1 :3

4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.

Yohana 1 :4

5 Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.

Yohana 1 :5

👉🏻 Kwahiyo epuka kujitamkia maneno  mabaya ili Mungu akufungulie milango ya baraka.

💻 29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.

Yeremia 22 :29

30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.

Yeremia 22 :30

👉🏻 Pia tunaona mtu anaweza kutamkiwa maneno ya kutokufanikiwa ikawa ni chanzo cha mateso maishani mwake .

💫.   Kupitia kutamkiwa maneno mabaya watu wengi wamejikuta wanakwama katika maisha yao .

👉🏻 Futa maneno yote mabaya uliyojitamkia au kutamkiwa

💻 10 Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi.

Isaya 8 :10

👉🏻 maneno yote uliyotamkiwa hayatasimama yafute maishani mwako .

💻. 7 Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa.

Isaya 7 :7

Neno lolote baya haliwezi kusimama katika maisha yako ukilifuta.

💫maneno mabaya ni giza linalozuia baraka za Mungu kukufikia .

Popote ulipojitamkia kushindwa au ulitamkiwa kushindwa tamka kufanikiwa .

💻 9 Maana Yeye alisema, ikawa; Na Yeye aliamuru, ikasimama.

Zaburi 33 :9

10 Bwana huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huyatangua makusudi ya watu.

Zaburi 33 :10

👉🏻Futa maneno ya kushindwa na uweke neno la kufanikiwa lisimamie maisha yako ili Mungu akubariki .

Mungu akubariki sana.

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*