🌐VITU MUHIMU VINAVYOWEZA KUMSAIDIA KIJANA KUISAFISHA NJIA YAKE 🌐

🌐VITU MUHIMU VINAVYOWEZA KUMSAIDIA KIJANA KUISAFISHA NJIA YAKE 🌐







Mwlm.Peter Francis Masanja





0679392829

Kutoka: The Voice of God Ministry




Anafundisha

JESUS CO_ WORKERS MINISTRY



πŸ’» Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.

Mhubiri 11:9


πŸ’« Ninaposema vijana nawagawanya katika makundi mawili makuu


1⃣ Wa kiume na

2⃣ wa kike

Hawa wote ni vijana .



πŸ’« Pia nitawagawa vijana katika umri utajifunza kuwa sifa za mtu kuitwa kijana lazima awe na umri wa miaka 18 hadi 45


πŸ’« Vijana pia naweza kuwagawa makundi mawili

1⃣ Ambao bado hawajaoa au hawajaolewa .


2⃣ Waliooa au kuolewa



πŸ’« Nilitaka kwanza ujitambue upo kundi gani kijana.



 πŸ’«kila kundi la vijana lina mapito mema ya kupendeza na yasiyopendeza.


πŸ’« Kijana hakuletwa duniani kihasara  , ameletwa duniani atambue nini cha kufanya ili mwisho wake uwe mzuri.


 πŸ’«Kijana yeyote ameletwa duniani ili  kutumika kwa kazi ya Mungu.


πŸ’« Kijana laziwa awe na maono

Unatoka wapi ? Upo wapi? na Unaelekea wapi ?


πŸ’» Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.

Mhubiri 11:9


πŸ’« lazima kijana atambue , hiyo njia apitayo inampeleka wapi ❓


πŸ‘‰πŸ» kuitambua njia ni wapi inampeleka kijana inahitaji maono .


πŸ’» Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;

Yoeli 2:28


πŸ‘‰πŸ» Kijana akibeba maono njia yake itampendeza Mungu na mwisho wake utakuwa ni uzima wa milele .


🌐 Tuangalie mambo muhimu yanayomfanya kijana aiweke njia yake iwe safi .



1⃣ URAFIKI ( USHIRIKA )


πŸ’» Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.

Zaburi 119:63


πŸ’«Marafiki wanamchango mkubwa sana katika kuifanya njia ya kijana iwe safi .


➡Pia marafiki wanaweza kuifanya njia ya kijana iwe mbaya kwa kumwingiza katika tamaa za dunia


πŸ’« Ili njia ya kijana iwe safi anatakiwa ajitenge marafiki ambao hawana ushirika na Mungu


πŸ’» Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.

Mithali 18:24


➡ Sisemi kijana usiwe na marafiki lakini unatakiwa kujua hao marafiki wanakuweka karibu na Mungu ❓



➡ Kama hawakuweki karibu na Mungu wakimbie .πŸƒπŸ»‍♂πŸƒπŸ»‍♂πŸƒπŸ»‍♂πŸƒπŸ»‍♂


πŸ’» 3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?

Amosi 3 :3


πŸ’« Kijana huwezi kuwa rafiki na watenda mabaya ukabaki huna kovu la mabaya.


πŸ’« Kijana aliyeokoka awe na marafiki wa imani



πŸ‘‰πŸ» Waangalie Shadrach ,Meshach na Abednego hawa walikuwa marafiki wa imani


πŸ‘‰πŸ» Waangalie Musa na Haruni walikuwa marafiki wa imani.


πŸ‘‰πŸ» Mwangalie Petro aliambatana na Yesu ,


πŸ‘‰πŸ» Je , wewe unarafiki yupi wa imani ❓


 πŸ‘‰πŸ»Jiulize maswali yafuatayo:


1⃣ Ananifanya nikue kiroho au nife kiroho ❓
.
2⃣ Anaamini katika  utakatifu ❓

πŸ‘‰πŸ» kama haamini katika utakatifu hakufai .


3⃣ Anampenda Mungu au anaigiza kumpenda huku anashiriki matendo ya giza ❓

πŸ‘‰πŸ» lazima uwe na rafiki ambaye anampenda Mungu na kutii maagizo yake .➡ hili eneo la urafiki limebeba maisha yote ya kijana katika dunia hii


 2⃣ Kudumu katika neno


 πŸ’» 8 Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.

Yoshua 1 :8



πŸ‘‰πŸ»Maisha ya kijana bila kusoma neno la Mungu yanakuwa kwenye hatari ya kumsahau Mungu na kumilikiwa na adui ( shetani ) .


πŸ‘‰πŸ» Kijana aliyeokoka njia yake inaongozwa na neno la Mungu , kwa maana hii basi njia ya kijana inasafishwa na neno la Mungu.


πŸ‘‰πŸ» Ili njia ya kijana iwe safi lazima neno la Mungu likae ndani yake na alifanyie kazi .


 πŸ’» Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

Zaburi 119:11


πŸ‘‰πŸ» Njia ya kijana imeshikiliwa na neno la Mungu


πŸ‘‰πŸ» Kijana bila neno la Mungu ni rahisi sana kuchafua njia yake kwa kutenda dhambi .


πŸ‘‰πŸ»Lazima kijana atambue kuwa mafanikio yake ya kiroho na kimwili yameshikiliwa na utii neno la Mungu


 πŸ’» Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.

Ayubu 22:21



πŸ‘‰πŸ»Kadri kijana anavyozidi kumjua Mungu ndivyo Mungu anavyozidi kumpa kibali cha kumiliki na kutawala .


πŸ‘‰πŸ» Mwangalie Ibrahimu , Isaka , Yakobo , na Yusufu hawa walipata kibali kwasababu walienda katika njia za Bwana.na walitii kile Mungu alichowaambia .


πŸ‘‰πŸ» Mwangalie Nuhu alivyoitii sauti ya Mungu na kutenda aliyomwagiza aliokoka na gharika .



πŸ‘‰πŸ»Mwangalie Selemani alivyotii sauti ya Mungu jinsi alivyofanikiwa na kupewa uwezo wa juu sana na akawa mtawala mzuri sana.



πŸ’» 22 Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.

Yakobo 1 :22


πŸ‘‰πŸ»Neno la Mungu linalokaa ndani ya kijana linatakiwa alitendee kazi yaani liongoze njia zake.


πŸ’» Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Zaburi 119:105


3⃣ Kuwa na ushirika na roho Mtakatifu .


πŸ’» Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;

Waefeso 5:18


 πŸ‘‰πŸ» Kijana ili njia yako iwe safi lazima ufanye ushirika na roho mtakatifu


πŸ‘‰πŸ» Roho Mtakatifu ni mwalimu , Mshauri , Kiongozi ,na anatufunulia yatakayotukia .


πŸ‘‰πŸ» Kijana akiwa na ushirika na roho wa Mungu njia yake itakuwa safi .


πŸ’» kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.

Warumi 8:13


 πŸ‘‰πŸ»Njia ya kijana ikiwa chafu tambua yupo mwilini


πŸ‘‰πŸ»Kijana akiwa mwilini lazima njia yake itakuwa chafu na mwisho wake utakuwa ni mauti .

πŸ’» Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

Wagalatia 5:5


Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.

Wagalatia 5:25


πŸ‘‰πŸ» Usafi wa njia ya kijana umebebwa na roho wa Mungu .


 πŸ’» Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.

Wagalatia 6:8


πŸ‘‰πŸ»Kijana lazima utambue tamaa za mwili zinakuvutia kuzimu lakini ukienenda kwa roho njia yako itakuwa safi na utaurithi uzima wa milele .



πŸ’» Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

Wagalatia 5:16


Mungu awabariki sana


Leo naishia katika mambo hayo matatu

: Hitimisho


Jifunze ,



πŸ’« misingi mikuu inayofanya njia ya kijana iwe safi ni .


1⃣ Marafiki Wa imani wanaoitii kweli ya Mungu .


2⃣  Neno la Mungu


3⃣Ushirika na Roho Mtakatifu .



https://peterfrancismasanja.blogspot.com


πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’

Maoni

  1. Nimebarikiwa asante kwa ujumbe mzuri Mungu akubariki.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*