CHANGAMOTO NA MAJARIBU KATIKA UONGOZI πŸ’’*


 *πŸ’« CHANGAMOTO NA MAJARIBU KATIKA UONGOZI πŸ’’*




SIKU YA KWANZA


Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829
0744056901


πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’


SAUTI YA MUNGU MINISTRY


πŸ’« _UTANGULIZI_ 🌐



✍🏻 Changamoto ni nini ❓


✍🏻 Majaribu ni nini ❓



πŸ’« Changamaoto ni kikwazo kinachomzuia mtu asifikie malengo fulani au kinachomfanya mtu aahirishe kufanya jambo fulani.

πŸ’« Changamoto ni upinzani au kipingamizi kinachomfanya mtu asifikie malengo yake kwa mahangaiko au akate tamaa.



πŸ’« Changamoto katika kila kazi lazima ziwepo .



πŸ’« Changamoto zinamfanya mtu aweze kufikiri na kupambanua mambo ili aweze kufanya vizuri maishani mwake



πŸ’« Changamoto huzaa maamuzi ya nini mtu afanye na kwa namna gani .




🌐 Katika uongozi wowote duniani kuna changamoto nyingi sana .


✍🏻 Kama nilivyotangulia kusema changamoto ni kikwazo au kitu chochote kinachokuzuia usifikie malengo uliyoyakusudia , basi katika uongozi kuna changamoto nyingi sana.



πŸ’« Watu wanaokuzunguka wanaweza wakawa ni changamoto katika uongozi wako .



πŸ’« Hata ukiwafanyia mema kiasi gani lakini wapo watakusema vibaya yaani watakuchukia bila hata sababu.



πŸ’« Wengine watakuchukia kwa sababu ya kutenda haki .

Utasikia wanasema oooh ametubania .

Nini ulichowabania ❓

πŸ‘‰πŸ» Umewazibia mipango yao mibaya ndyo maana wanakuchukia .



πŸ’« Katika uongizi wa kiroho


πŸ‘‰πŸ» Kiongozi anayesema ile kweli ya Mungu huchukiwa sana na kizazi cha leo kinachohalalisha usasa ( kila tamaduni zisizo na maadili yanayomtukuza Mungu ).



πŸ’« Changamoto katika uongozi hazijaanza hivi karibuni , zilianza kipindi cha Musa .


πŸ’« Wana wa Israeli walikuwa walalamikaji sana wlikuwa wanamlalamikia Musa pamoja na Mungu .


πŸ’« Ilifikia hatua Musa mwenyewe akataka kukata tamaa kuwaongoza kwa sababu ya maneno ya wana wa Israeli .



πŸ’» 11 Wakamwambia Musa, Je! Kwa sababu hapakuwa na makaburi katika Misri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona umetutendea haya, kututoa katika nchi ya Misri?

Kutoka 14:11

12 Neno hili silo tulilokuambia huko Misri, tukisema, Tuache tuwatumikie Wamisri? Maana ni afadhali kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani.

Kutoka 14:12


 πŸ’«Katika uongozi huwezi kuepuka malalamiko


πŸ’«usiyaangalie malalamiko yakiwa ni kinyume na mpango wa Mungu wewe simamia ni nini Mungu anasema .

πŸ’«Kwa leo naomba utafakari ni marangapi umekata tamaa katika uongozi ❓


πŸ‘‰πŸ» Kukata tamaa ni kushindwa ,

πŸ’« Nakuomba sana usikate tamaa katika kazi yoyote uifanyayo .

πŸ’« Usiyasikilize maneno ya kukatisha tamaa .


πŸ’« Fanya kazi ya Mungu usiangalie kusemwa na watu .


 Musa angeangalia maneno ya watu asingeweza kuongoza lakini kwa kuwa aliangalia Mungu anasema nini alifanikiwa kuongoza vizuri .




Mungu akubariki sana
[Endelea kufuatilia somo hili utajifunza mengi sana




https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

  1. Tumeona ufumirifu wamsa na hatimayake kwa watu ariokua akiwaongoza je kunautofauti gani kitiyauongozi wasasa nauongozi wamsa kwaviongozi wariopo?

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*