π KIJANA NA MAISHA YA KIROHO ✍π»*
π KIJANA NA MAISHA YA KIROHO ✍π»*
Mwl.Peter Francis Masanja .
0679392829
Sauti Ya Mungu Ministry
Swali : NIFANYE NINI ILI NIKUE KIROHO ❓
π» 22 wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.
Matendo ya Mitume 14:22
π« Inawezekana kuna watu huwa wanajiuliza hawapati majibu kuhusu nini wafanye ili wawe imara kiroho .
π« Lakini leo Mungu anakuonyesha mambo ya kufanya ili mtu fulani ambaye wa kwanza ni mimi , wewe na yule .
π« Kuna kila sababu ya kujifunza mbinu zitakazokusaidia kiroho .
π« Katika kujifunza mbinu za kiroho , kuna mambo mawili ya kuzingatia .
1⃣ Kuachana na mambo fulani ili ukue kiroho .
✍π» Kuna baadhi ya mambo lazima kijana ayaache ili akue kiroho .
π« Baadhi ya mambo hayo ni kama vile ; mambo ya mizaha, tamaa za dunia kama vile ulevi , uzinzi, uasherati , n.k
Kuacha kutumikia miungu ya kigeni ,
π« Acha kutumia mda mwingi kwenye mambo yasiyo na maana tafta kujadili mambo ya kiMungu .
π« Acha kupoteza muda wako kwenye movie ( filamu ) masaa mengi
2⃣ FANYA YAFUATAYO ILI UKUE KIROHO
✍π»✍π»✍π»✍π»✍π»✍π»✍π»✍π»✍π»
π« DUMU KATIKA KUSOMA NENO
✍π» Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya usomaji wa neno na ukuaji wa kiroho wa kijana .
π» 16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
Wakolosai 3:16
π« Kadri unavyozidi kusoma neno na kulifanyia kazi ndivyo unazidi kukua kiroho.
π« Neno la Mungu likikaa kwa wingi ndani ya moyo wako linahalalisha ukuaji wa kiroho .
π» Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
Yohana 8:31
π« Baada ya kumwamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako unakazi ya kusoma neno
π«Ndyo maana utaona anawaambia wale Wayahudi waliomwamini wakae katika neno .
Kukaa katika neno maana yake ni kulisoma neno na kulitendea kazi .
π« Mtu asomaye neno ni mwanafunzi wa Yesu kwelikweli
ππ» Kwa maana hiyo mtu ambaye hasomi neno bado hajakuwa mwanafunzi wa Yesu kweli kweli ( hajakua kiroho ) .
π« KAA KARIBU NA MLEZI WAKO WA KIROHO
ππ» Vijana wengi wakiokoka wanajisahau kukaa karibu na walezi wao wa kiroho kitu ambacho kinawafanya wapoteze dira ya kiroho .
✍π» baba yako wa kiroho ni mtu muhimu wa kukufanya wewe ukue kiroho ,
Ukiwa karibu naye utajifunza mbinu nyingi za kiroho
π« TAFTA MARAFIKI WA IMANI
Haruni alijifunzia utumishi kwa Musa
ππ»Je wewe unarafiki gani ambaye anakufanya ukue kiroho ( anakuweka karibu na Mungu )
ππ» usikubali kuwa na marafiki ambao watakufanya ufe kiroho .
ππ» Petro alikuwa karibu sana na Yesu ndyo maana alimpenda .
ππ»Je rafiki yako wa karibu sana anakufanya umtafakari Mungu ❓
Kama ni hapana huo urafiki unafaida gani ❓
π« Rafiki uliye naye anaweza akaawa mchango kwa wewe kuanguka au kukua kiroho
π« waangalie wa kina Shadrak , Meshack na Abedinego hawa vijana waliimarishana kiroho .Nawewe tafta watu ambao watakufanya ukue kiroho
Naomba niishie hapo kwa leo
Mungu akubariki sana
https://peterfrancismasanja.blogspot.com
Karibu siki nyingine tuendelee na somo letu

Maoni
Chapisha Maoni