MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MAOMBI π
π« MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MAOMBI π
Mwl.Peter Francis Masanja
0679392829
SAUTI YA MUNGU MINISTRY
π» 11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
Waefeso 6:11
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
Waefeso 6:12
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
Waefeso 6:13
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
Waefeso 6:14
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
Waefeso 6:15
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
Waefeso 6:16
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
Waefeso 6:17
π« Kama askari aendavyo vitani , vivyo hivyo na mtu aingiapo katika maombi anatakiwa kujua kuwa maombi ni vita.
π« Ili mtu aingie kwenye maombi anatakiwa ajipange kwanza , maana anakwenda vitani kupambana na shetani na jeshi lake .
π« Mtu aendapo vitani huchukua silaha yake na kuiweka tayari kwa kuanza vita .
Mfano , ataandaa bunduki na risasi nyingi kwaajili ya kumpiga adui.
π« Kwa mtu mwombaji , anapomwendea Mungu anatakiwa ajipange na kuhakikisha kuwa moyo wake wote upo kwa BWA
π« Baada ya kujipanga anatakiwa kujua kwamba kutangaza vita na shetani vita kwelikweli .
π« Unatakiwa kufahamu kwamba silaha kuu ya kumshinda shetani ni neno la Kristo pekee.
π« Shetani hupingwa kwa neno , bila neno huwezi kumshinda shetani na hila zake.
π« Neno la Kristo linamfanya shetani akimbie .
π» Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
Yakobo 4:7
π«Shetani anapingwa kwa neno
π« Unasisitizwa sana kabla ya kuanza maombi hakikisha unaomba ulinzi.
π« Tubu pale uponkosea Mungu
π« Mkaribishe roho Mtakatifu awe mwalimu wako katika maombi yako .
π» 26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Warumi 8:26
π« Lialike jeshi kutoka mbinguni likulinde
Pia jifunike na damu ya Yesu .
π» Mmoja angefukuzaje watu elfu, Wawili wangekimbizaje elfu kumi, Kama Mwamba wao asingaliwauza, Kama Bwana asingaliwatoa?
Kumbukumbu la Torati 32:30
π« Ni kazi ngumu kumfanya shetani akukimbie , mpaka uite msaada kutoka mbinguni.
π Ualike jeshi la malaika kutoka mbinguni liwe pamoja na wewe katika maombi .
π« Vita ya kiroho unayopigana siyo yako ni vita ya Mungu na adui zako
π« Mungu ni adui wa adui zako wanaokusumbua katika ulimwengu wa roho na ulimwengu wa macho .
π« Ili Mungu aingilie hiyo vita lazima umwite yeye maana ukinyamaza hawezi kuwaondosha adui zako.
π» 6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;
Isaya 62:6
π«Hutakiwi kunyamaza kimya wewe mwana wa Mungu maana Mungu mwenyewe anasisitiza usinyamaze mkumbushe mahitaji yako .
π« Maombi yako yatafaa zaidi ukianza na kumsifu Mungu .
π« Kumwimbia Mungu sifa na kuabudu kunamfanya Mungu aachilie nguvu ya ajabu ndani yako .
π« Maombi ya mtu anayeanza na kumsifu Mungu yana nguvu sana kuliko maombi makavu yaani maombi bila kumsifu Mungu .
βπ»βπ»βπ»βπ»βπ»βπ»βπ»βπ»
Mungu akubariki sana nahitimisha kwa kuaema hivi.
π« Katika maombi zingatia
1β£ Sifa na kuabudu ili maombi yako yawe ya ushindi .
2β£ Hakikisha unamwalika Roho Mtakatifu akufundishe vita .
3β£ Alika jeshi la malaika kutoka mbinguni likuzingire ili shetani asipate nafasi ya kukudhuru.
4β£ Jifunike na damu ya YESU wewe na vitu vyote ulivyonavyo ili shetani asipate nafasi ya kukudhuru wewe na vitu vyako.
5β£ Hakikisha unatumia neno la Mungu katika maombi yako maana neno ndyo silaha kuu ya kumharibu shetani .
https://peterfrancismasanja.blogspot.com
Maoni
Chapisha Maoni