πŸ’« ROHO YA UASI 🌐*

πŸ’« ROHO YA UASI 🌐*




Mwl. Peter Francis Masanja



0679392829




SAUTI YA MUNGU MINISTRY



roho ya uasi ni roho isiyotaka toba





πŸ’«mtu mwenye roho ya uasi hataki kukemewa .




 πŸ’«mtu mwenye roho ya uasi ukimkemea umemtukana .




 πŸ’« mtu mwenye roho ya uasi anapinga kweli ya Mungu anahalalisha dhambi.



πŸ’« Imekuwa kawaida kwa vijana wa kike kuvaa mavazi ya aibu wakiita fasheni bila kujua kuwa wanamwasi Mwenyezi Mungu .



 πŸ’« Imekuwa jambo la kawaida kwa Vijana wa kike wakiwa na kazi basi hawatii waume zao tena wala kuomba samahani kwao hakuna kabisa .


Hii ni roho ya uasi



 πŸ’« Hii roho ya uasi iliyoingia kwa vijana wa kike inawafanya wengi wao kuzeekea makanisani bila kuolewa kabisa .



πŸ’« Imekuwa ni desturi ya kawaida hata kwa vijana wa kiume kubebesha mimba na kutelekeza wanawake

Hii ni roho ya uasi .



πŸ’« Hii roho ya uasi inaukataa ukweli inafuata tamaa za mwili ikisingizia kufanya mapenzi kabla ya ndoa ni burudani .



πŸ’« Hii roho ya uasi inawafanya wakristo wafungishe ndoa huku wanamimba



πŸ’» 13 Ushuhuda huo ni kweli. Kwa sababu hiyo uwakemee kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani;


Tito 1:13


14 wasisikilize hadithi za Kiyahudi, wala maagizo ya watu wajiepushao na yaliyo kweli.


Tito 1:14


15 Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia.


Tito 1:15


16 Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.


Tito 1:16



πŸ’« mtu mwenye roho ya uasi hataki kuthamini mawazo ya wenzake .



πŸ’« mtu mwenye roho ya uasi hawezi kujishusha hata kama kakosea



πŸ’«mtu mwenye roho ya uasi anakufanya wewe wa ziada kwenye mahusiano hana mda na wewe .



πŸ’» 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,


2 Timotheo 3:2


3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,


2 Timotheo 3:3


4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;


2 Timotheo 3:4




 πŸ’« mtu mwenye roho ya uasi anakiburi .



πŸ’« mtu mwenye roho ya uasi anapenda maisha ya anasa kuliko kumpenda Mungu .



Ukimwambia twende kwenye mkesha wa maombi hataki lakini anaenda kuangalia mechi za mpira usiku au anaangalia filamu akidai anajifunza kumbe ajitengenezea njia ya kwenda kuzimu .




 πŸ’« mtu mwenye roho ya uasi hataki kuchangamana na wanaishika kweli ya Mungu


Yeye marafiki zake wengi hawajaokoka yaani watenda dhambi



πŸ’«Mkemee hata kama hataki kukemewa mkemee



πŸ’» 1 Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;


2 Timotheo 4:1


2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.


2 Timotheo 4:2



πŸ’«Nimeagizwa kukaripia na kukemea kwa mafundisho ya uzima sitaki mzaha



πŸ’« nichukie nichukie nitukane lakini ukweli umeupata



πŸ’« upo kanisani unasema Mungu haangalii mavazi wewe unaroho ya uasi .



πŸ’« Leo tunasafisha kanisa , tunatoa uchafu kanisani


πŸ’« wamekaa kanisani huku ni waasi wanaikataa kweli kwa kuhalalisha ujinga ( maovu).



πŸ’» Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.


1 Yohana 2:19



πŸ’«Anajiita mpendwa lakini matendo yake hayanatofauti na wasioamini .


πŸ’« Wakristo feki ,Wakristo photocopy .



 πŸ’« wanapenda nyimbo za dunia kuliko nyimbo zinazomtukuza Mungu   , yaani ni waasi .



 πŸ’« Hawasomi hata neno kazi kukaa yao ni  kuleta mizaha kwenye neno la Mungu kwa kutaka kuingiza habari za dunia .



πŸ’« Waache kiburi watubu wamrudie Mungu



: πŸ’» 1 Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; Uwahubiri watu wangu kosa lao, Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.


Isaya 58:1


Mungu akubariki sana

Nakutakia siku njema


https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*