UKWELI KUHUSU NDOA



UKWELI KUHUSU NDOA


SWALI: JE NI HALALI KUVUNJA NDOA IKIWA MUME HANA NGUVU ZA KIUME ?


Majibu :

Pastor Peter Sponga A.

From Bahi _ Dodoma



JESUS CO_WORKERS MINISTRY



Hiyo inavunjwa  ndoa ni tendo kwanza mengine ni mbwembwe



 Kanisa linakaa na kuvunja



Tatizo likimpata akiwa kwenye ndoa huo ni msalaba wako inabidi uubebe



Japo ni nguvu ya kanisa kuamua maana tokea zamani wasioweza tendo la ndoa walijulikana mapema na hawakuruhusiwa kuoa



 Kwahiyo Biblia iko kimya sasa kama huwezi kumpa binti haki yake na ulizaliwa hivyo haiwezekani



 Umeonja vya moto vyabaridi vyenye chachu vikavu vibichi halafu kisaikolojia uwe fiti labda uwe umepondwa pondwa na huyu Yesu vinginevyo utaona ndoa ni PINGU PINGUA NA WOKOVU JOKOFU


Kweli na shida leo madhehebu wachungaji vijana

Group wengi vijana

Mtu anazaliwa mpaka anakua anaishi na vijana

Mengi ya mambo ya chumbani nguvu za kiume yalimalizwa na mababu zamani



Mnafundishana kwa video za ngono

Unataka ujifunze mpira wa Miguu kwa kuangalia mechi Messi akiwa anawapita mabeki??

Unajua chenga hiyo kajifunza kwa miaka mingapi??



Vijana ukiwaambia unaswali hawana

Kuna tatizo wanakuambia pambana na hali yako



Binti anaingia kwenye ndoa anafikili ndoa ninvicheko tu akinuniwa siku moja anapost whataap jamani nisaidieni baby kanuna



Anapost video analia baby hajanichumu leo si nivituko hivi



 Watu tunachati nanyi tunaomba tuna hudumu kumbe usiku nilipigwa kipepsi lakini tulifundwa



Tumebahatika wwnzenu kukaa na wazee vijijini na mijini wazee ndio rafiki zetu

Leo vijana wanaamini kila mzee ni mchawi



Leo mnaingia kwenye ndoa kila mtu anabullet proof kwenye akili ndoa umeambiwa ni uwanja wakujaribisha silaha ulizo nazo



 Ndoa ni paradiso ndogo ndio maana ulipewa raha huwa unasahau shida zako na kupitiwa na usingizi mwororo


Kila kabila lina ubora mitindo na udhaifu katika mambo ya familia na katika ubora wa tendo la ndoa


Kuna makabila tendo ndio muhimili wa ndoa lakini makabila mengine ni kiburudisho tu sawa na juice baada ya kula  hata kama hakuna ni sawa tu


Kuna kabila ukienda kuoa utaomba pooo lakini mengine kila ukitaka mpaka upige magoti au uandike barua ya maombi uambatanishe na zawadi na picha



Kunamakabila baba mkwe alitaka lazima umpe maana mke ni mali ya ukoo


Kuna makabila baba akioakabinti saizi yako unaruhusiwa kuingia mara moja moja na mtoto akizaliwa anakuwa mdogo wako



Sasa ktika mazingira haya ambayo watu tumekutana kanisani usione kila anayenena kwa lugha ni mkristo wengine bado mila hawajaacha




FANYA YAFUATAYO

1.Amin Mungu anaweza kukupatia mwenza mwema

2.omba Mungu akupe wa kwako , wamaisha yako, unayemmudu, atakaye kupa raha hadi uzee

3.tulia mngoje Bwana maana hakawii wala hawahi

4. Kuwa mtii kufuata maelekezo kuelekea kwenye ndoa

5. Kuwa tayari kurekebisha vigezo vya mwenza uliyemtaka linapokuja swala la kumsubiri Bwana

6. Kumbuka wakati wakuanza familia ulishapangwa ukifika usijizuie anza Bwana ameshaweka tayari unavyoviona na visivyoonekana kwajili ya familia hiyo.

Ukiwahi au ukichelewa utajipigania mwenyewe

7. Ndoa ni shule kamili hatakama ulikuwa mwalimu wa wanandoa kabla ya kuoa ulishaanza ndoa kubali kuanza CHEKECHEA

KUMBUKA NDOA



1+1=1 ni jibu linaloweza kutolewa na mwanafunzi wa chekechea pekee

Mwisho

KUMBUKA SIKU ZOTE KUJITOLEA KWAAJILI YA MWENZIO NA KUTAMANI KUJUA HISIA ZA MWENZA WAKO JUU YAKO


 Kama huamini kuwa ndoa ni hatma yako usiolewe utajinajisi tu


Wanaume tujenge mazingira ya kusikiliza wachumba wetu na tuwatoe mashaka yote yanayowasibu kabla ya kuingia katika ndoa



Mwanamke ni ngumu kuishi mpk uzee bila kuolewa wala kupata mtoto kuliko mwanaume. Kwa nn.?



 Tafadhali wakaka tuache tabia ya kuwateka wasichana

Unamkuta mkaka anatawala mawazo ya msichana na kumfanya zezeta unamfanya kama simu hutaki kusikia mawazo yake

Kumbuka unaweza kudanganya na kutawala kila mara lakini hutoweza kutawala na kudanganya siku zote



 Wadada acheni mawazo hasi kuhusu ndoa bado mabikira wapo kuanzia wamwili hadi wa fikra



Mpokeee mtu ambaye unadhani anastahili kuwa mfalme wako ili akufanye kuwa malkia



Kumbuka ndoa inalenga kujenga himaya ukoo siyo eneo la pikiniki au kujirusha.


Usipowekeza vya kutosha katika ndoa yako hakuna atakaye kusaidia


Unaporuhusu mtu asiyehusika kuwa muhimili wa ndoa yenu hata kama unaona leo anawafaa sana au anakufaa sana tambua kuwa ndoa yako haitadumu




Jitahidi kuwa na muda wa kutosha wa mijadala na mwenza wako ili mjenge mifumo yenu katika mambo haya.

1. Mtafunga ndoa ya aina gani

2.mtaishi maisha kwa mfumo gani wa kiroho kimila au kisayansi

3.mtaishi wapi

4.mnawategemezi wangapi na mtawasaidiaje

5. Mtazaa watoto wangapi na majina yao yatapatikanaje

6. Ajira itakuwaje ,kiuchumi mtashirikianaje, uhifadhi wa mali.

7. Anataka zaidi ya kuwa mwenza uwe nani wake, mwalimu ,mzazi, mlezi ,mshauri nk

8.kubalianeni namna ya kupeana raha zenu. Mf. Ukinikwaza omba radhi .

Au usiku ukiona sina nguo ujue nataka😁😁😁😁

Tutasali wapi??


Kumbuka mawazo na milengo tofauti katika ndoa ndio uharibifu wenu wamali na wawatoto

Mungu awabariki siwezi kumaliza

Nawapenda

Pastor Sponga Peter A.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*