WEWE NI NANI MPAKA UMFANYE MUNGU WA ZIADA

💫 WEWE NI NANI MPAKA UMFANYE MUNGU WA ZIADA ❓*






Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829


SAUTI YA MUNGU MINISTRY



💫 Huna mda hata wa kumtunikia Mungu unasingizia biashara na chaajabu biashara yako haiingizi hata 50000 kwa siku tayari umeringa na kumsahau Mungu .




💫 Wewe ni muuza chakula tu gengeni unaacha kwenda ibadani .Eti upo busy unatafta pesa mambo ya Mungu badae hivi unajua kuwa hata kwenye hicho kibanda amekuweka Mungu ❓



💫 Wapo watu wakubwa sana makanisani wamefanikiwa na hawajaacha kumtumikia Mungu kwa sababu ya mali zao wewe umepata kazi mda mfupi tu umemdharau Mungu na kumfanya wa ziada .


� Vipi kuhusu wanasheria na madaktari wapiga vinanda makanisani , je huwaoni hao ❓


Mbona hawajamfanya Mungu wa ziada ❓



Wewe ni nani mpaka umfanye Mungu wa ziada ❓




 💫 Kwanini unasoma neno siku ya ibada hadi siku ya ibada tu ❓

Au huoni kuwa umemfanya Mungu ni wa ziada ❓




💫 Je haujui kuwa imeandikwa ufalme wa Mungu utatekwa na wenye nguvu ❓


👉🏻 Sizungumzii nguvu za kimwili nazungumzia nguvu za kiroho yaani wale wafanyao kazi ya Mungu kwa bidii watauteka ufalme wa mbinguni .



💻 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

Mathayo 11:12



💫 Kazi ya Mungu ni ya kwanza kabisa tena ipangie mda wa kutosha maishani mwako .


💫 Jifunze kumwomba Mungu kwa kila ufanyalo na kumshukuru pia naye atakubariki zaidi .



 💫 Wapo watu watakufa maskini kwa sababu hawamtii Mungu wamemfanya kuwa wa ziada .



💫 Mungu anawaangalia na kusema ,


👉🏻 Mtu huyu nimemfanikisha kidogo tu kanisahau nikimpa utajiri si ataniasi huyu

Simpi utajiri wangu huyu

🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂




 💫 Saivi tu umeanza kuacha kanisani ukidai kazi nyingi miradi yako itasimama , nakwambia hiyo miradi itakufa mpendwa kama hutamtii Mungu .

✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻



 💫 Mungu anakanuni za kumfanya mtu awe tajiri .


1⃣ Anataka umtii

👉🏻 Umtumikie ndiyo akuzidishie mali zako


Usipo mtumikia kwa bidii utakuwa hupigi hatua kiuchumi kila siku wewe kukicha unakula matembele tu

🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂



 💫 Mwangalie Ibrahimu jinsi alivyokuwa mtii hakumwacha Mungu kwa sababu ya vitu alivyonavyo .



 💻 1 Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu.
Mwanzo 17:1

2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana.
Mwanzo 17:2

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.

Mwanzo 17:6



💫 Mtumikie Mungu kwa bidii na kutenda mema



💫 Mungu anakuangalia je , umejitoa kwake ❓

Kama hutaki kumtumikia na kumheshimu kukupa utajiri sahau kabisa .


✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻




 💻 1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

Kumbukumbu la Torati 28:1

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.

Kumbukumbu la Torati 28:2

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

Kumbukumbu la Torati 28:3

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

Kumbukumbu la Torati 28:4

5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.

Kumbukumbu la Torati 28:5

6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.

Kumbukumbu la Torati 28:6

7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

Kumbukumbu la Torati 28:7

8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.

Kumbukumbu la Torati 28:8



 💫 Usipomtumikia na kumheshimu atakuacha kwenye maisha ya tabu sana , anakubakiza kiwango ulichonacho hakuzidishi mpaka utakapoamua kutii ndyo atakupandisha zaidi .



 💻 34 Hata mwisho wa siku hizo, mimi, Nebukadreza, nikainua macho yangu kuelekea mbingu, fahamu zangu zikanirudia; nikamhimidi Yeye aliye juu, nikamsifu na kumheshimu Yeye aishiye milele; kwa maana mamlaka yake ni mamlaka ya milele, na ufalme wake hudumu toka kizazi hata kizazi;
Danieli 4:34

36 Basi wakati uo huo fahamu zangu zikanirudia, na kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu, enzi yangu na fahari yangu zikanirudia; na mawaziri wangu, na madiwani wangu, wakaja kunitafuta; nami nikathibitika katika ufalme wangu, nikaongezewa enzi kupita kiasi.

Danieli 4:36




2⃣ Utoaji


👉🏻 Hii ni kanuni nyingine ambayo inamfanya Mungu akuinue kiuchumi



💫 Utoaji siyo sadaka tu , hata kuwasaidia wasiojiweza , yatima na wajane ni sehemu ya utoaji pia .



👉🏻 Kuna watu wamebakia maisha ya mateso kwasababu siyo watoaji

Katika

✍🏻 Zaka

✍🏻 Kusaidia yatima na wajane

✍🏻 kusaidia wagonjwa


Hivi vitu ni vizuizi kwako usiinuliwe kiuchumi .




💫 Mungu anaangalia na kusema

Hivi tu nilivyomfanikisha amesahau watu na kuwapita hawajali
Nikimzidisha si atanyanyasa watu huyu ❓


Simpi utajiri nimwache ahangaike na umaskini asiniasi .

✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻




💻 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Malaki 3:10

11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi.

Malaki 3:11

12 Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema Bwana wa majeshi.

Malaki 3:12



💫 Kama nilivyosema mwanzo kuwa utoaji wako mbele za Mungu uambatane pia na kusaidia watu wenye shida mbalimbali ambao hawajiwezi .



💻 1 Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

Matendo ya Mitume 10:1

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.

Matendo ya Mitume 10:2

4 Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.

Matendo ya Mitume 10:4



 💫 mwangalie Kornelio jinsi Mungu alivyombariki na kumkuza kiuchumi kwa sababu tatu .


1⃣ Kumcha Mungu

2⃣ Kumtolea Mungu

3⃣ kusaidia watu

👉🏻 Hata kumwambia mtu fanya hiki ni kumsaidia pia .


Mungu akubariki sana



Tutaendelea siku nyingine

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*