HAKI , SHERIA , NA NEEMA
HAKI , SHERIA , NA NEEMA
Mwl.Peter Francis Masanja
0744056901
Bwana YESU asifiwe
✍ Kuna wakati mtu
wa Mungu unaweza ukakaa mda mrefu sana huoni matunda ya kile ambacho umemwomba
Mungu .
✍ Kitu chochote
ambacho unakiomba ndani yake lazima kuwe na neno imani ili uweze kukipokea .
✍ Imani inazaa
haki yaani kitu unachostahili kukipokea .
Ibrahimu alihesabiwa haki kwa imani
Maana yake alipokea kile alichostahili sawasawa na
kile alichokiamini .
π» 17 Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa,
akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa
mwanawe, mzaliwa pekee;
Waebrania
11:17
18
naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa,
Waebrania
11:18
19
akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka
huko kwa mfano.
Waebrania
11:19
✍ Ibrahimu
hakusita alipoambiwa na BWANA amtoe mwanaye , Isaka
Aliamini kuwa Mungu atamfufua Isaka akatii sauti ya Mungu .
✍ Huyu Ibrahimu kupitia imani hiyo kuna ahadi
aliipokea kwa Mungu .
π» 1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu
Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
Mwanzo
22:1
2
Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako
mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo
nitakaokuambia.
Mwanzo
22:2
9
Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko,
akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya
madhabahu, juu ya zile kuni.
Mwanzo
22:9
10
Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.
Mwanzo
22:10
11
Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu!
Naye akasema, Mimi hapa.
Mwanzo
22:11
12
Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa
ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.
Mwanzo
22:12
14
Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika
mlima wa BWANA itapatikana.
Mwanzo
22:14
15
Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
Mwanzo
22:15
16
akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala
hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
Mwanzo
22:16
17
katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama
nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango
wa adui zao;
Mwanzo
22:17
18
na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii
sauti yangu.
Mwanzo
22:18
✍ Ibrahimu alikuja kupokea vitu vingi sana vizuri
toka kwa Mungu kwa sababu ya ile imani . Aliamini kuwa Mungu ni msaada wake
pekee .
✍ Mtu wa Mungu
lazima utambue kuwa imani inanguvu katika kupokea kile unachokiomba.
✍ Imani lazima iambatane na matendo ndani yake kile
unachokiamini lazima ukitendee kazi ili kionekane.
Maana
kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo
imekufa.
Yakobo
2:26
✍ Ibrahimu aliitendea kazi ile imani akaitwa mwenye
haki, akabarikiwa sana .
π» 17 Kwa maana
haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama
ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.
Warumi
1:17
✍ Maisha yako ya imani yaambatane na utii .✍ Mtu wa Mungu palipo na sheria kuna dhambi .
✍ Dhambi ilipoingia ndipo Mungu akaleta sheria yaani
amri ambazo mwanadamu anatakiwa azifuate .
✍ Pamoja na
sheria za Mungu kuletwa bado hazikumzuia mwanadamu kuzivunja .
✍ Sheria ambazo Mungu alizitoa pale Sina kwa mkono wa
Musa hazikutosha kumwokoa mwanadamu.
✍ Sheria
haikutosha kumfanya mwanadamu awe mbali na dhambi .
✍ Mungu akaona ni
vema sheria zake aziandike kwenye moyo wa kila mwanadamu.
✍ Mungu akamtoa YESU Kristo afe kwaajili ya dhambi
zetu ili tuwekwe huru tutengwe mbali na dhambi.
✍ Ndipo tulipoingizwa katika kipindi cha neema mpaka
sasa tupo huru mbali na dhambi .
✍ Mpaka sasa
hakuna amwaminiye Yesu asiyezijua sheria za Mungu .
Sheria haiwezi kumtenga mtu mbali na dhambi bali
neema ya Kristo .
16 Hili
ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria
zangu mioyoni mwao, Na katika nia zao nitaziandika; ndipo anenapo,
Waebrania
10:16
Mtu wa Mungu , huyu Yesu kupitia neema yake
ametuzawadia vitu vingi sana .
v Tumepokea
wokovu .
v Uzima
wa milele.
v Neema
imetupa mamlaka ya kuishinda dhambi
14 Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa
sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema.
Warumi
6:14
v Katika
kipindi hiki cha neema , sisi ni watumwa wa haki ( matendo mema ).
18 na
mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki.
Warumi
6:18
v Dhambi
haina mamlaka ya kututawala tena bali sisi tunayo mamlaka ya kuitawala (
kuishinda).
12 Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu
ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake;
Warumi
6:12
v Neema
imetupa mamlaka ya kushinda dhambi .
Ili mamlaka
ya kuishinda dhambi ikae ndani yetu tunatakiwa kukaa ndani ya Yesu , tusiende
mbali.
ΓΌ Tudumu katika sala.
ΓΌ Tusome
neno
ΓΌ Tulifanyie kazi neno .
Bila kukaa
ndani ya YESU imani yetu katika yeye haiwezi kuzaa matunda.
v Bila
kukaa ndani ya YESU vizuri imani yetu itakuwa ya kutiana faraja kuwa mwenye
haki ajapo anguka mara saba atasimama tena.
v Mtu
wa Mungu kamwe usiamini katika kuanguka na kusimama tena maana huwezi kujua
siku unaanguka ndyo mwisho wako .
v Mungu hajakuleta duniani uangukeanguke
alikuleta usimame imara kabisa kama neema inavyotufundisha kukataa ubaya
wowote.
π» Kesheni,
simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari.
1
Wakorintho 16:13
Mtu wa Mungu usiruhusu mbengu ya kuanguka na
kusimama tena
Ruhusu mbegu ya kusimama imara katika imani bila
kuanguka .
v Neema
imetupa ujasiri wa kuonya .
v Neema
imetukataza kutenda dhambi za kujitakia ( za kujua ).
π» 47 Na
mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda
mapenzi yake, atapigwa sana.
Luka
12:47
Hakuna kitu
kibaya kama kufanya jambo ukijua kuwa ni katazo .
v Mtu
wa Mungu hii neema tuliipokea kwa ajili ya kutenda mema .
Γ Tumeokolewa
kwa neema.
Γ Tunaishi
kwa neema .
Γ Tumechaguliwa
kwa neema.
Γ Tumepokea
mamlaka ya kumuliki na kutawala kwa neema.
Γ Tumeuona
utukufu wa Mungu ndani yetu kwa neema .
Γ Tumepokea
karama , vipawa, na huduma mbalimbali kwa neema .
Γ Tumempokea
Roho Mtakatifu kwa neema .
Γ Tumefanyika
wana wa Mungu kwa neema .
Γ Tunawashangaza wakuu wa dunia kwa neema.
Neema ya
Mungu inafaida sana kwetu .
Mungu
akubariki sana .
Neema ya Mungu iangaze maisha yako popote ulipo .
Neema ya Mungu izuie kila mabaya yasikupate .
Neema ya Mungu iambatane na kila ulichonacho
kifanikiwe .
Neema ya Mungu ifufue miradi yako iliyokufa .
Nakutakia
jioni njema .
Maoni
Chapisha Maoni