HISTORIA YA MAKANISA SABA


                       HISTORIA YA MAKANISA SABA.

MWL.LAMECK KIJALO
+255 656 824 479:
JESUS CO-WORKERS MINISTRY


Ø  Makanisa haya yanapatikana katika kitabu cha UFUNUO sura ya 2&3
Ø  Hivyo kwa wenye Biblia ni vizuri mkafungua hizo sura na kuzipitia wakati Somo linaendelea
 Makanisa saba hayo ni:-
1)Kanisa la Efeso. Ufunuo 2:1-7
2)Kanisa la Smirna
Ufunuo 2:8-11
3)Kanisa la Pergamo.
Ufunuo 2:12-17
4)Kanisa la Thiatira.
Ufunuo 2:18-29
5)Kanisa la Sardi.
Ufunuo 3:1-6
6)Kanisa la Filadelfia
Ufunuo 3:7-13
7)Kanisa la Laodikia.
Ufunuo 3:14-22.



Kanisa ni nini?
Ø  Kanisa ni mtu, au kusanyiko la watu pamoja na Jengo wanalotumia, mtu au watu wanaomwamini Mungu na kufanya taratibu zote za Ibada, kama vile kuabudu, kufanya maombi, kusifu, kujifunza maneno ya Mungu n.k.

Ø  Makanisa saba(7) huonyesha historia ya Kanisa iliyopitia vipindi saba ambapo Leo hii tupo kwenye Kanisa la kipindi cha saba liitwalo Laodikia.


Ø  Vipindi hivi vya Kanisa vilianza pale Yesu alipopaa kwenda mbinguni, ambapo tunaona kuwa Kanisa la kwanza Kabisa kuanzishwa ni Kanisa la Efeso. Kanisa lililoanzishwa na Mitume.

Ø  Ikumbukwe kuwa  Kiini cha kuwepo kwa Kanisa ni Yesu Kristo mwenyewe. Na katika vipindi hivi saba suala la majina ya madhehebu kama Roman Catholics kuwa ndiyo Kanisa la kwanza hayana ukweli wowote kwani kama tulivyo Leo hii kwenye kipindi cha Kanisa la Laodikia basi madhehebu yote humezwa humo. Na yamkini kwenye kipindi cha Kanisa la Waefeso yalikuwepo Madhehebu mengi tu yanayounda Kanisa.


Ø  Tambua kuwa kila kipindi cha Kanisa kina msimamizi wake ambaye ni Malaika.

Ø  Ndiyo maana Biblia inasema; Na kwa Malaika wa Kanisa lililoko...... Andika.


Ø  Hivyo Malaika alikuwepo wa Kanisa la kwanza akamaliza kazi yake, na wa pili,..., mpaka leo tunaye Malaika wa Mwisho katika hili Kanisa.

Ø  Tambua kuwa vipindi saba vya Kanisa, ni ukamilifu wa uumbaji, kama ambavyo Mungu aliumba dunia kwa SIKU sita, SIKU ya saba ambayo ni ukamilifu wa kila kitu akapumzika.


Ø  Hii inamaana tupo kwenye kipindi cha mwisho Kabisa na sifa zote za Kanisa la Laodikia ndizo tunazo sasa.

Ø  Katika hivi vipindi kuna makanisa yalitiwa Moyo, kuna makanisa yalionywa, na kushauriwa. Hivyo vipindi hatutaviingia kwa undani sana kwani muda wangu ni mdogo.
Hivyo twende haraka kuangalia mapito ya Kanisa katika hivi vipindi saba.


KANISA LA EFESO.
Ø  Hili ni Kanisa la kwanza Kabisa.

Ø  Ni Kanisa lililopitia taabu nyingi sana. Hiki ndicho kipindi ambacho Paulo alihusika kuwaua wakristo na mmoja wa Wakristo aliyeuliwa ni Stephano. Wengi wa mitume walifungwa jela. Hakika mwanzo SIKU zote huwa mgumu sana. Lakini licha ya mateso na kuuliwa kwa baadhi ya wateule wa Mungu, bado Imani iliendelea kuenea na kushika hatamu.


Ø  Pia kuna watu walijifanya ni watumishi wa Mungu kumbe ni waongo, lakini walijaribiwa na kuonekana ni waongo, ndiyo maana imeandikwa Ijaribuni kila roho ili kujua kama yatokana na Mungu au la. Kina Mtume Petro kipindi hiki walikuwa si watu wa kuchezea imani zao.
Lakini mwisho hili Kanisa lilikosa Upendo,
Ø  Hivyo likaonywa likumbuke ni wapi lilipoupoteza huo Upendo na kuuanzisha upya.
Lilisifiwa kwa kuyachukia matendo ya Wanikolai ambao wao walikuwa ni waabudu sanamu.
Hivyo watu Hawa waliahidiwa kuwa ikiwa watashinda yote hayo na kutekeleza maagizo waliyoagizwa basi watakula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu

 KANISA LA SMIRNA.
Ø  Hili ni Kanisa ambalo ni la kipindi cha pili.

Ø  Waamini wa kipindi hiki walipitia dhiki kubwa na walipitia hali ya umaskini sana. Walikuwa wakitukanwa, na wengine walionekana ni waumini wazuri lakini kumbe walikuwa ni wa Shetani.


Ø  Waumini Hawa walitiwa Moyo kuwa wasijione ni maskini bali wao ni matajiri, pia waliambiwa wasiogope japo watatiwa magerezani. Lakini walitakiwa wawe waaminifu hata kufa. Na wakaahidiwa taji ya uzima.

Ø  Naomba niishie kwa Leo kwenye makanisa haya mawili, next wiki nitamalizia mengine matano.

Ø  Katika haya makanisa mawili, vitu vya kujifunza ni kuwa mpaka Leo tunatakiwa kujifunza juu ya suala la:-
1) Kuishi kwa Upendo.
2) Kuyapinga matendo mabaya ambayo ni machukizo kwa Mungu kama vile kuabudu sanamu, uzinzi, anasa, n.k.
3) Kuzijaribu kila roho zinazojidai kuwa zatokana na Mungu, yaani tuwajaribu wachungaji, manabii, wainjilisti, mitume, walimu, waimbaji n.k. kama je ni kweli wanamtumikia Mungu?
5) Tusiogope kufa wala kufungwa magerezani tunapoitetea imani yetu.
 6) Hata kama unaishi maisha ya umaskini lakini kwa sababu ya kuwa mwaminifu mbele za Mungu, jione kuwa Wewe ni Tajiri sana
 7) Lakini tunajifunza kuwa tunapokosea ni sharti tujue ni wapi tumekosea au kutenda dhambi kisha tutubu, la sivyo tutahukumiwa
8) Tambua kuwa ahadi zote za Mungu juu ya wanaomtumikia ni njema sana mfano kula mti wa uzima. Kupewa taji ya uzima.
Je nani hapendi uzima?
Mungu awabariki sana.

KARIBU TENA

Maoni

  1. Kanisa la sardi maana halis

    JibuFuta
  2. Nimebarikiwa sana maana nilikua sijui maana ya hili kanusa la saba

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*