JE ,KUNA TOFAUTI GANI KATI YA HEKALU,SINAGOGI NA KANISA?


JE ,KUNA TOFAUTI GANI KATI  YA HEKALU,SINAGOGI NA KANISA?

                                             Mwl.Elias Mgallah
                                          ( 0768 645 718)
                               Jesus Co-Workers Ministry

BWANA YESU APEWE SIFA

Ø  Ipo tofauti kati ya Hekalu,Sinagogi na kanisa ingawa tofauti yenyewe si kubwa sana na ndio maana unaweza ukadhani vyote ni sawa lakini kumbe si sawa kwa sababu ya utofauti wao.

Ø  Si wengi wenye kuweza kuelezea maana kamili ya matatu hayo yaani hekalu,sinagogi na kanisa. Tofauti ya kila moja imejificha kiasi kwamba kuonekana ni vigumu,kama vile tofauti iliyojificha kati ya maneno haya mawili;
 Agano na Mkataba.
Ingawa ipo tofauti kati ya agano na ,mkataba.

Ø  Basi siku ya leo napenda nikueleze maana ya hekalu,sinagogi na kanisa kwa ufupi kidogo,nami ninatumaini kwamba utapokea jambo kubwa siku ya leo.

 TUANZE KUZUNGUMZIA

01.HEKALU.
Ø  Ilikuwa ni sehemu takatifu ya kwa Waisraeli,hivyo hekalu lilikuwa na sehemu tatu muhimu;
1.Ukumbi wa nje.
2.Hekalu au patakatifu.
3.Sehemu ya juu/patakatifu pa patakatifu.
Ø  Kulikuwa na utofauti kati ya hekalu/patakatifu na sehemu ya patakatifu pa patakatifu,tofauti ya kwanza ni kwamba sehemu ya patakatifu pa patakatifu ilikuwa ni sehemu ya juu zaidi wakati katika hekalu palikuwa chini yake.sijui kama unanielewa.

Ø  Tofauti nyingine ni kwamba patakatifu pa patakatifu ndio ilikuwa sehemu hasa ya kulihifadhi sanduku la  agano,na palitenganishwa na pazia kati ya patakatifu na hekalu ( Soma 1 Wafalme sura ya 6 yote). Kuhani mkuu ndiye aliingia patakatifu pa patakatifu mara moja kwa mwaka ( Walawi 16:15-17).

v  Hekalu ni nyumba kubwa ya ibada ya jamii ya Wayahudi.Hekalu hukusanya watu wenye kunia mamoja katika kumfanyia ibada BWANA.).

v  Patakatifu pa patakatifu ni mahali ambapo panaaminika kuwa ndipo Bwana Mungu hushuka na kuigusa dunia.


Ø  Panaaminika ndipo mahali ambapo Mungu huketi,hivyo kuhuni huingia mara moja kwa mwaka kwa ajili ya kupeleka mahitaji ya watu wake waliopo chini.

Ø  Kwa sababu kuhani anakwenda kukutana na Mungu,hivyo ilimbidi kwanza ajitakase yeye kwanza kabla ya kuachilia utakaso kwa wengine ambapo watu wote wakimsubilia chini.

Ø  Jambo hili tunaliona likitendeka kwa kuhani Zekaria wa zamu wa Abiya pale kura ilipomwangukia
” Basi ikawa, alipokuwa akifanya kazi ya ukuhani katika taratibu ya zamu yake mbele za Mungu, kama ilivyokuwa desturi ya ukuhani, kura ilimwangukia kuingia katika hekalu la Bwana ili kufukiza uvumba. Na makutano yote ya watu walikuwa wakisali nje saa ya kufukiza uvumba. ” Luka 1:8-10
Ø  Katika biblia yetu tuisomayo kila siku,inaeleza kuwa Hekalu   lilianzia tangu agano la kale. Mara ya kwanza tunasoma habari za hekalu kupitia kuhani Eli ambaye alikuwa akiketi hekaluni siku zote.( 1 Samweli 1:9 )
Ø   
 ( i ) Hekalu katika Jerusalemu ( hekalu katika Uyahudi )
Kwa mujibu wa historia ya Waisraeli,kulipatwa kujengwa mahekalu matatu yaliyojengwa katika nyakati tofauti tofauti na watu tofauti tofauti ndani ya Yerusalemu
 1.Hekalu la Sulemani ~ Mwaka 950 kabla ya Kristo,ambapo hapo baadae hekalu hili liliteketezwa na Wababuloni katika mfalme wake Nebukadreza II mnamo 586 kabla ya Kristo.
 2.Hekalu lingine dogo ~ Hekalu hili lilijengwa mahali hapo hapo mnamo mwaka wa 515 kabla ya Kristo,katika kipindi cha Ezra ndani ya utawala wake mfalme Dario ( Ezra 6:15-16).
3.Hekalu lililojengwa upya na Herode mkubwa ~ Lilijengwa mnamo kuanzia mwaka wa 19 kabla Kristo baada ya uhamisho wa Babeli

Ø  ( Uhamisho wa Babeli ni kipindi ambacho Wayahudi walilazimishwa kuishi Babuloni. kwa lugha nyingine ni kwamba Wayahudi walilazimishwa kuishi Babeli,ambayo kwa sasa tunaweza kusema

Ø  walipelekwa Iraq,sababu magofu ya Babeli yapo katika mji wa kisasa wa Al-Hillah,kando ya mto flati kama 90km kusini mwa Baghdadi). Hekalu hili liliteketezwa (baada ya uvamizi ) na Warumi katika mwaka 70 baada ya Kristo.

Ø  Hata hivyo baadhi ya Wayahudi wanaamini kuwa na hekalu jingine pale Yerusalemu kitu ambacho wataalamu wa mambo ya historia wametilia shaka kwamba inaweza kutokea mapigano makubwa baina ya wenye kutaka na wasiotaka hali hiyo sababu katika eneo ambapo hekalu lilipokuwapo kwanza,sasa wapo wenye imani tofauti na Kikristo.
( ii ) Hekalu katika ujio wa Kristo Yesu.
Ø  Ujio wa Bwana Yesu,ulihamisha hekalu la kujengwa kwa mikono hata kila aaminie anakuwa ni hekalu ambapo Roho mtakatifu hukaa ndani yake. ( 1 Wakorintho 6:19). Yeye Yesu Kristo ametununua kwa damu yake ya thamani,na sasa tu mahekalu ya Roho mtakatifu.

 02.SINAGOGI

Ø  Neno hili limetoka katika lugha ya kigiriki ” Sinagoge ” lenye maana ya “ Mkutano” ni tafsiri ya kiebrania ni beit knesset lenye maana ‘“ Nyumba ya mkutano”
           1 Wakorinto:6.19

Ø  Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
Ø  Katika lugha ya kiebrania neno “ beit ”  linamaana “ nyumba” ndio maana hata ukisoma bethsaida “ Nyumba ya mvuvi” au bethsania-Nyumba ya masikini. (Soma injili imetajwa sana majina haya ).

TOFAUTI KATI YA HEKALU NA SINAGOGI
Ø  Hekalu huwa ni jengo kubwa lenye sehemu mbali mbali za ibada,wakati sinagogi huwa ni mkutano tu wa watu katika jengo lisilokuwa na mgawanyo mkubwa.

Ø  Hekalu lina sehemu ya patakatifu pa patakatifu,sinagogi halina sehemu hiyo.

Ø  Hekalu lilikuwa kuanzia agano la kale mpaka agano jipya mfano kuanzia kitabu cha 1 Samweli 1:9,mpaka Ufunuo 21:22- Wakati Sinagogi lenyewe halitajwi katika agano la kale bali agano jipya tu.

Ø  Hekalu hukusanya jamii ya watu wenye kuamini,wenye kunia mamoja katika ibada wakati Sinagogi huchukua wanye kuamini na wasioamini,Sinagogi huchukua watu safi na hata watu ovyo.


Ø  Ukiwa ni mfuatiliaji mzuri wa neno la Mungu,utaona kipindi ambacho Bwana Yesu au hata mtume Paulo alipoingia katika Sinagogi kuhubiri,mara nyingi sana alishindana nao. Sababu ya kuwa na watu wenye kuamini na wengine wasioamini. Mfano mdogo waweza soma Matendo 17:1-5.
Ø  Mara baada ya uhamisho wa Babeli na kuvunjwa kwa hekalu la pili mwaka 70 tunaona sinagogi likishamili sana.
          Matendo ya Mitume:17.1

Ø  Wakiisha kupita kati ya Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambapo palikuwa na sinagogi la Wayahudi.

    Matendo ya Mitume:17.2

Ø  Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu,
             Matendo ya Mitume:17.3
 akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na         ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo.
Matendo ya Mitume:17.4
Ø  Wengine miongoni mwao wakaamini, wakashikamana na Paulo na Sila; na Wayunani waliomcha Mungu, wengi sana, na wanawake wenye cheo si wachache.
             Matendo ya Mitume:17.5
Ø  Na Wayahudi wakaona wivu, wakajitwalia watu kadha wa kadha katika watu ovyo wasio na sifa njema, nao wakakutanisha mkutano, wakafanya ghasia mjini, wakawaendea watu wa nyumba ya Yasoni, wakataka kuwapeleka mbele ya watu wa mji;

03.KANISA.
Kanisa ni nini?
Ø  Kwa mujibu wa neno la Mungu zifuatazo ni tafsiri tano tafsiri sahihi za maana ya neno hili “kanisa“.

Ø  Awali ya yote neno hili “kanisa” tunalolitumia leo,lenye chimbuko la lugha ya kiyunani kwa jina la “ Kuriakon” yenye maana ya “ mali ya Bwana ” ndio maana katika Mathayo 16:18 Yesu anasema “ nitalijenga kanisa langu,”  ikiwa na maana kanisa ni mali ya Bwana

Ø  Lakini ikumbukwe ya kwamba katika agano neno hili lilitafsiriwa kwa jina la Kiyahudi “ ekklesia” yaani “ watu fulani walioitwa na Bwana,au watu waliotengwa na Bwana”

1.Kanisa ni mwili wa Kristo
“ akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.” Waefeso 1:22-23.

Ø  Biblia inaeleza ya kwamba Yeye Kristo ndie kichwa cha kanisa,lakini kanisa ni mwili wake. Neno “kichwa cha kanisa ” lina maana ya “ kiongozi mkuu wa kanisa” .

Ø  Katika tafsiri hii ya kwanza ni vyema kufahamu kuwa tu viungo vya Kristo kwa kuwa tu mwili wa Kristo.

Ø  Ni jambo la aibu ikiwa kanisa linaitwa kwa mwili wa Kristo lakini limekumbatia dhambi,Je mwili wa Kristo waweza ukashiriki dhambi? Hapana hauwezi kushiriki dhambi yoyote ile.
2. Kanisa ni kusanyiko la waaminio katika Kristo Yesu.
Ø  Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.” Yoh.10:1
Ø  Ikumbukwe kwamba kusanyiko hili la waaminio limepewa jina kondoo waliokusanyika kama kundi pa moja na mchungaji wao. Kupitia andiko hili,Yesu anasema analo kundi jingine ambalo anapaswa kulileta pamoja na kwa kuwa ni mali ya Bwana basi,watamsikia.
3.Kanisa ni hekalu/jengo/nyumba ya kuabudia.
Ø  Tafsiri hii ni moja ya tafsiri ambayo watu wengi wameijua,kwa maana watu wanapotamka kuhusu kanisa humaanisha kwamba kanisa ni jengo fulani hivi. Kupitia fasiri hii;wanakuwa hawajakosea. Biblia inaeleza pia kwamba;20 Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.

Ø  Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika Bwana.Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.


Ø  Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika Bwana.Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.” Waefeso 2:21-22.
4.Kanisa ni bibi harusi wa Kristo;
Ø  Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa.” Waefeso 5:31-32.

Ø  Ikumbukwe kwamba katika ulimwengu wa roho,kila aliyeokoka na kumfuata Kristo Yesu amefanyika kama bibi harusi.

Ø  Kwa lugha nyepesi tumefunga naye agano;na ndio maana mtu akimuacha Kristo Yesu kisha akaigeukia miungu mingine basi anaitwa ni mzinzi/amezini.


Ø  Umewahi kujiuliza kwa nini uitwe mzinzi hali hujazini katika mwili?  ( ufunuo 2:14). Hivyo tumuonapo bibi harusi basi ni dhahiri yupo bwana harusi na pia kuna harusi yao.

Ø  Katika ulimwengu wa roho KristoYeye mwana-kondoo ndiye Bwana harusi kwa maana kuna harusi ya mwana-kondoo huko mbinguni ( soma Ufunuo 19:7)
 Ufunuo:2.14

Ø  Lakini ninayo maneno machache juu yako, kwa kuwa unao huko watu washikao mafundisho ya Balaamu, yeye aliyemfundisha Balaki atie ukwazo mbele ya Waisraeli, kwamba wavile vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na kuzini.

 Ufunuo:19.7

Ø  Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.
5.Kanisa ni hekalu la Roho mtakatifu.
Ø  Tafsiri hii inalenga hekalu za namna mbili. Hekalu la kwanza ambapo Roho mtakatifu anapokaa ni ndani yako ya moyo na hiyo ndiyo madhabahu ya kwanza ya mwamini ( 1 Wakorintho 3:16).

Ø  Pia hekalu la pili ni katika madhabahu sehemu fulani ya kanisa iliyotengwa kwa ajili ya kazi ya Bwana. Madhabahuni pa Bwana,mahali ambapo dhabihu zinapotolewa..

 1 Wakorinto:3.16

Ø  Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Ø  Hivyo tafsiri hii inamlenga mwamini mmoja mmoja kuwa ni kanisa ( mwamini ametengwa kwa ajili ya Bwana,huitwa pia ni sehemu ya kanisa kwa sababu moyo wake u madhabahu). Kigezo kikubwa cha kanisa ni uwepo wa madhabahu mahali ashukapo na akaapo Bwana Mungu.
Mkazo mkubwa wa kanisa kama mwili wa Kristo.

Kwa kuwa tumeona maana ya kanisa kiundani,basi hatuna budi kuweka mkazo juu ya kanisa kwamba Yesu mwenyewe ndio kichwa cha kanisa sisi tu viungo kila mmoja wetu. (Wakolosai 1:18)
TOFAUTI YA KANISA NA HEKALU NA SINAGOGI
Wakolosai:1.18

Ø  Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.

Ø  Katika kanisa huzungumzia mtu moja tu, pasipo kuleta maana halisi ya jengo,wakati hekalu muda mwingine huonesha jengo,na sinagogi huonesha kusanyiko la watu.

Ø  Katika kanisa sisi tu viungo vya Kristo,hii inaonesha kuwa sote tunahitajiana kuukamilisha mwili wa Bwana tofauti kabisa na hekalu na sinagogi.
 Nakupongeza kwa kujifunza fundisho hili,Mungu akubariki sana

Maoni

  1. Mungu akubariki sana mtumishi wa Bwana Yesu, nimejifunza hakika nilikuwa sijui baadhi ya mambo lakini sasa nimejua barikiwa sana.

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*