JE, UNA MHURI WA MUNGU ?
📙
JE, UNA MHURI WA MUNGU ?
Mwl.Peter Francis Masanja
0744056901
BWANA YESU ASIFIWE
KARIBU TUJIFUNZE KWA PAMOJA SOMO HILI
1 Baada
ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia
pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya
mti wo wote.
Ufunuo
wa Yohana 7:1
2
Nikaona malaika mwingine, akipanda kutoka maawio ya jua, mwenye muhuri ya Mungu
aliye hai; akawapigia kelele kwa sauti kuu wale malaika wanne waliopewa
kuidhuru nchi na bahari,
Ufunuo
wa Yohana 7:2
3
akisema, Msiidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia
muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao.
Ufunuo
wa Yohana 7:3
Ø Muhuri
ni uthibitisho wa umiliki wa kitu fulani , ni alama ya ambayo inatambulisha
kitu fulani kipo chini ya mamlaka fulani.
Ø Mhuri
pia ni alama inayofanya kitu fulani kikubaliwe kuwa halali .Bila mhuri kitu
hicho hakiwezi kupokelewa .
Ø Mhuri
pia unasemekana kama chapa au alama ya utambulisho .
Ø Mhuri
ni kadi au kitambulisho au cheti kinachoweza kumruhusu mtu aingie mahali
fulani.
Ø Wewe
mtu wa Mungu umewekwa mhuri ambao utakufanya uingie katika ufalme wa mbinguni.
Mhuri huu
tunaouzunguzia ni mhuri ambao siku ya mwisho utakupatia uhalali wa kuurithi
ufalme wa Mungu ( mbinguni).
Biblia
inasema , si kila mtu aniambiye Bwana , Bwana ataurithi ufalme wa mbinguni .
Maadamu upo duniani hapa wewe mtu wa Mungu napenda
Mungu akujiulize maswali yafuatayo:
Ø Ninaombea
watu pepo wanatoka lakini ninao mhuri wa Mungu ?
Ø Ninaombea wagonjwa wanapona je,ninao mhuri wa
Mungu ?
Ø Ninaonyesha ishara na matendo ya miujiza
je,ninao mhuri wa Mungu?
Ø Ninahubiri sana injili na kumwimbia Mungu na
kumpigia vinanda je,ninao mhuri wa Mungu?
Mwulize rafiki
yako je, unao mhuri wa Mungu ?
21 Si kila
mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni
yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Mathayo 7:21
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana,
hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako
kufanya miujiza mingi?
Mathayo 7:22
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe;
ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Mathayo 7:23
Kwanini si kila mtu aliitaye jina la BWANA ataingia
katika ufalme wa mbinguni ?
Ø Kwasababu
si kila aliitaye jina la BWANA ana mhuri wa Mungu.
Mhuri wa
Mungu unathibitishwa na matendo ya haki , hiki ndyo kigezo cha msimgi cha
kumfanya mtu awe na mhuri wa Mungu.
Wanaotiwa
mhuri wanatoka katika kila.
👉🏻Taifa
👉🏻
Kabila
👉🏻
Jamaa
👉🏻
Lugha n.k
Kama mtu
anasali na anaishi maisha ya dhambi , hatawekwa mhuri wa Mungu.
Na kama
hatawekwa mhuri wa Mungu anakazi gani kanisani , maana anafanya kazi haitazaa
matunda kwake .
9 Baada ya
hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye
kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele
ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana
matawi ya mitende mikononi mwao;
Ufunuo wa Yohana 7:9
Ø Tunawekwa
mhuri kama saini ya kwenda mbinguni .
12 Tena naliwapa sabato zangu, ziwe ishara kati ya
mimi na wao, wapate kujua ya kuwa mimi, Bwana, ndimi niwatakasaye.
Ezekieli 20:12
20 zitakaseni sabato zangu; zitakuwa ishara kati ya
mimi na ninyi, mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Ezekieli 20:20
Unapodumu
katika kujitakasa kwa damu ya Yesu ili uwekwe mhuri wa Mungu.
Sote tuliompokea YESU na wanaotarajia kumpokea kama
Bwana na mwokozi wa maisha yetu tumealikwa kwenda mbinguni tukiwa tumewekwa
mhuri wa Mungu katika vipaji vya nyuso zetu.
📙
HITIMISHO
✍
Kuuingia ufalme wa mbinguni lazima tutiwe mhuri wa Mungu.Tuvae matendo mema.
✍
Kama ilivyo kwenye sherehe au harusi bila kadi huingii ndivyo ilivyo na
kuuingia ufalme wa Mungu .
✍
Matendo mema ndiyo utambulisho wa kuingia katika ufalme wa mbinguni.
Mungu akubariki sana
KWA MASWALI
Piga simu namba: 0679392829 au 0744056901
Waweza kunipata whats app kwa namba hizo.
Maoni
Chapisha Maoni