MAOMBI BILA NENO LA MUNGU NI SAWA NA GARI BILA MAFUTA


📖 MAOMBI BILA NENO LA MUNGU NI SAWA NA GARI BILA MAFUTA 📙


Mwl.Peter Francis Masanja

0744056901

📖📖📖📖📖📖📖📖📖
Kumshinda shetani siyo kazi nyepesi kama huna neno la Mungu ndani yako .
Neno la Mungu ndiyo kweli na hii kweli humweka mtu huru kabisa kutoka kwenye mitego ya ibilisi.
📖 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

Ufunuo wa Yohana 12:11
Neno la Mungu na damu ya YESU ni silaha kuu ya kumshinda shetani .

Bila neno maombi yako yatakuwa kama kusoma gazeti tu .
: Kama unadesturi ya kuanza maombi bila neno nakushauri acha kabisa na uanze kusoma neno la kusimamia mahitaji yako unayompelekea Mungu .
Maombi yakikosa neno yanachosha na hayawi na nguvu ndani yake .
Umefunga na kuomba na umeorodhesha mahitaji ya kuombea , pia usisahau kuweka neno la Mungu litakalosimamia kila hitaji .
Baraka za Mungu zinaletwa na neno la Mungu pekee , ukilisimamia vizuri na kulitendea kazi utafanikiwa .
: Neno la Mungu ni silaha ya kumpigia shetani kwahiyo litumie katika maombi
Usipambane na watoto wako kwa fimbo , bali weka msingi mzuri wa kumjua Mungu
Watakapoingia kwenye maombi wafundishe kutumia neno wawe waombaji mashujaa .
Jiwekee ratiba ya kutafakari neno kila siku , ili mwovu akikujia umchape vizuri .
Huwezi kumshinda shetani kama huna ushirika na neno la Kristo .
Halleluya 🎤🎤


Neno la Mungu likuongoze katika maombi , ujiepushe na maombi ambayo hayatumii neno maana ni dhaifu .
Mungu akubariki sana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*