NGUVU YA MSAMAHA 2
NGUVU
YA MSAMAHA
Mwl.Peter Francis Masanja
0744056901
Somo letu lililopita tuliangalia faida ya
msamaha kiroho .
Leo
tuangalie faida hasara za kutokusamehe kiroho na kiafya.
1.
Kutokusamehe husababisha ugonjwa wa
hasira.
✍🏻
mtu wa Mungu tambua kuwa hasira miongoni wa magonjwa ambayo yanatesa vijana
katika maisha yao .
Usiposamehe
itakuwa kila unapomwona aliyekukwaza au kukukosea hasira zinapanda tena .
Usiposamehe
utakuwa mwepesi wa hasira ukikwazwa jambo dogo tu hasira kali inakupanda .
Kuna vijana walijikuta wamepoteza dira ya
maisha kwa sababu ya hasira .
Kutokusamehe hupansikiza mbegu ya wepesi wa
hasira .
Tafiti
zinaonyesha vijana wengi walioumizwa kwenye mahusiano wengi ni wepesi wa hasira
.
Hii
ni kwasababu ya kutunza kumbukumbu za wapenzi wao .
Mtu
wa hasira huchochea ugomvi;
Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza
mashindano.
Mithali
15:18
2.
Kutokusamehe huzeesha mapema .
Mtu
wa Mungu unaposamehe maana yake unamwondoa kabisa mtu aliyekukosea moyoni mwako
.
Ukikaa
na mtu umemchukia hutaki kumsamehe unaweza ukakwama kiafya.Watakuona kila siku
unakonda tu .
Hali hii ya kuzeeka mapema hujidhihirisha kwa
wanandoa .
Utaona
binti ameolewa alikuwa na ngozi nyororo na umbo zuri lakini walipopishana
kidogo tu kila siku huzuni ukimwuliza anasema haifurahii ndoa yake .
Kila
siku utamwona anakonda kama ukuni mkavu
Binti
kaolewa lakini miaka mitatu amezeeka na yupo na mumewe anakula vizuri kabisa ,
tafakari.
3.
Kutokusamehe huleta magonjwa ya moyo
.
Mtu wa Mungu unatakiwa uepuke sana hali ya
kutokusamehe .
Usiposamehe maana yake ukimwona aliyekukosea
mapigo ya moyo yanapanda .
Mishipa
ya moyo inatanuka , presha na stress zinakuua uzeeni .
Kuna mama mmoja alikosana na mume wake alipata
stress akalazwa .Mama hakutaka kabisa kuonana na mumewe ilikuwa kila akimwona
ugonjwa unaanza upya .
Mama yule alikataa mpaka kula chakula anaomba
afe tu .
Yule mama alipotoka hospitali alirudishwa
nyumbani kwao lakini haukuisha mwaka akafariki.
4. Kutokusamehe
hupandikiza roho ya mauti
Maana yake ukishindwa kusamehe kifo
kinakunyemelea wewe mwenyewe .
Ukijisikia huna ule moyo wa kusamehe jua
shetani yupo kazini anataka akumalize.
5. Kutokusamehe
husababisha roho ya kisasi ( kulipiza kisasi ) pamoja na Roho ya uuaji(
umwagaji damu ) .
Kuua siyo lazima uchukue upanga au silaha
yoyote ,
Hata kumchukia mtu ni kuua mbele za Mungu .
21 Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue,
na mtu akiua, itampasa hukumu.
Mathayo
5:21
22
Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu
akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya
moto.
Mathayo
5:22
Chuki nyingi za ndugu zimeleta uuaji na
wengine kuua undugu kwa kutangaziana kabisa kwamba fulani siyo ndugu yangu
kuanzia leo
Tatizo ni kutokusamehe .
6.
Kutokusamehe humfanya mtu asisamehewe
dhambi zake mbele za Mungu.
15
Bali
msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
Mathayo
6:15
25
Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na
Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Marko
11:25
26
Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi
makosa yenu.]
Marko
11:26
Samehe
ili Mungu akusamehe dhambi zako.
7
Heri
waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao.
Warumi
4:7
8
Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.
Warumi
4:8
7.Kutokusamehe Husababisha Maombi Yako
Yasijibiwe.
25
Nanyi,
kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu
aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Marko
11:25
26
Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi
makosa yenu.]
Marko
11:26
Kwanini usiposamehe Mungu hawezi kujibu maombi
yako.
Kwa
sababu moyo wako umebeba
📙
UCHUNGU
📙
KINYONGO
📙
CHUKI
📙
UNAFIKI
📙
UONGO
n.k
Moyo
wa mtu asiyesamehe ni mchafu .
Mungu
anataka ufanye maombi ukiwa na moyo safi .
Bila kuwa na moyo safi huwezi kumwona Mungu(
maombi yako hayatajibiwa )
8 Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona
Mungu.
Mathayo
5:8
8.
Kutokusamehe Humleta Mtu Hukumuni
35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni
atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.
Mathayo
18:35
Mtu wa Mungu kutokusamehe ni dhambi kwahiyo
usipoiacha inaweza ikakuzuia kuurithi ufalme wa mbinguni .
Mungu
akubariki sana leo naishia hapa
Karibu
tena siku nyingine
francispeter424@gmail.com
Maoni
Chapisha Maoni