SIRI KATIKA MAOMBI 🛐

 SIRI KATIKA MAOMBI 🛐



Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829


SAUTI YA MUNGU MINISTRY



✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻




 *🛐 KWANINI BAADHI YA WATU HUSHINDWA KUOMBA KWA MUDA MREFU ❓*


✍🏻 Kutokukaa ndani ya YESU kunamfanya mtu ashindwe kuomba kwa muda mrefu .


 📙 7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Yohana 15:7


✍🏻 Kutokusoma neno kunamfanya mtu aombe kwa mda mfupi akose cha kuongea .


💻 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

Wakolosai 3:16



✍🏻 Dhambi usipoitubia vizuri ni kikwazo cha wewe kuomba muda mrefu


Dhambi inakusababisha uombe maombi ya kuchoka .


 ✍🏻 Na katika toba hawaingii na neno.

Toba kavu haina manufaa .


✍🏻 Fanya toba inayoambatana na neno .


Mfano :


💻 14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.

2 Mambo ya Nyakati 7:14

15 Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.

2 Mambo ya Nyakati 7:15

16 Maana sasa nimeichagua nyumba hii na kuitakasa, ili kwamba jina langu lipate kuwako huko milele; yatakuwako na macho yangu, na moyo wangu daima.
2 Mambo ya Nyakati 7:16

17 Nawe, ukienda mbele yangu kama alivyokwenda Daudi baba yako, ufanye sawasawa na yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu;

2 Mambo ya Nyakati 7:17

18 ndipo nitakithibitisha kiti cha enzi cha ufalme wako, kama nilivyoagana na Daudi baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kutawala katika Israeli.

2 Mambo ya Nyakati 7:18


💻 16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;


Isaya 1:16

18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

Isaya 1:18


Mwambie Mungu


🛐 Eee Mungu unasema tujioshe , tujitakase , tuondoe uovu na tuache kutenda mabaya .

🛐 Ninakuja mbele zako sawasawa na neno lako lilivyoandikwa katika

Isaya 1:16,19

Nionye Bwana , nioshe dhambi zangu kwa damu ya YESU .


Pia neno lako linasema katika zaburi 51



💻 1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.

Zaburi 51:1

2 Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu.

Zaburi 51:2

3 Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima.
Zaburi 51:3

4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu.

Zaburi 51:4

5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.

Zaburi 51:5

6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; Nawe utanijulisha hekima kwa siri,

Zaburi 51:6

7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji

Zaburi 51:7

8 Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi.

Zaburi 51:8

9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; Uzifute hatia zangu zote.

Zaburi 51:9

10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu

Zaburi 51:10

11 Usinitenge na uso wako, Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.

Zaburi 51:11

12 Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi.

Zaburi 51:12



 Hii ndio toba ya kweli lazima iambatane na neno

Usifanye toba kavu yaani toba isiyo na neno .


 Hii itakufanya uombe mda mrefu na Mungu atakujibu maombi yako


 ✍🏻 Kukosa umoja katika maombi kunasababisha upungukiwe maombi .


✍🏻 Tafuta marafiki mwe mnaomba nao kama kikundi .Hii itakuimarisha katika maombi .



✍🏻 Ukiona ulikuwa mwombaji sana halafu umepungukiwa kuna sababu mbili .



✍🏻 Umeanza maisha ya dhambi .


✍🏻 Unaishi na maeneo yasiyosalama wewe kuishi ( unaishi na wana wa uasi ) .
[


📙 UFANYAJE ILI UOMBE KWA MUDA MREFU ❓*





✍🏻 Anza na kumsifu Mungu kwanza maana kusifu kunawafukuza maadui .



✍🏻 Mshukuru Mungu kwa kukupa afya na uzima na kukupatia kibali cha kuomba .



✍🏻 Mwabudu katika roho na kweli .

( omba toba na reheme )



✍🏻 Msifu Mungu



✍🏻 Soma neno la kusimamia maombi yako .



✍🏻 Mkaribishe Roho Mtakatifu akufundishe kuomba na damu ya YESU ikufunike
Pia ita jeshi la malaika kutoka mbinguni likuzingire nikulinde .


✍🏻 Hakikisha unalitakasa eneo unapofanyia maombi ili asiwepo adui na mpelelezi yeyote wa kiroho .


✍🏻 Eneo unalofanyia maombi lazima liwe salama kiroho .


Maana kuna maeneo mengine yameugua yanaroho chafu .


📙 2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;

Kumbukumbu la Torati 12:2

3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.

Kumbukumbu la Torati 12:3



✍🏻 Hakisha unaorodhesha mahitaji yako ya kuombea hii itakufanya uombe kwa mda mrefu .


Kila hitaji mbele za Mungu lina ushahidi kutoka kwenye biblia yaani neno .


✍🏻 Kila hitaji lina neno la kusimamia .


Zingatia mifano ya mahitaji yafuatayo :



📙 KUOMBEA UCHUMI ( BIASHARA ) .



💻 11 Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.

Isaya 60:11





📙 KUOMBEA WAGONJWA



💻 1 Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
Mathayo 10:1



💻 17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

Marko 16:17

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

Marko 16:18




📙 KUOMBEA AMANI


💻 Kautakieni amani mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake mji huo ninyi mtapata amani.

Yeremia 29:7




📙 KUOMBEA HUDUMA KANISANI


💻 Ee Bwana, nimesikia habari zako, nami naogopa; Ee Bwana, fufua kazi yako katikati ya miaka; Katikati ya miaka tangaza habari yake; Katika ghadhabu kumbuka rehema.

Habakuki 3:2




📙. KUOMBA ULINZI

💻 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;

Isaya 62:6




Mwambie Mungu yeye anasema , kupitia maneno hayo mwambie afanye sawasawa na maneno hayo .


Neno linanguvu sana katika hitaji umwombalo Mungu .

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*