TAFTA KUJUA NI KITU ULICHONACHO AMBACHO ADUI ANAKIWINDA
TAFTA KUJUA NI KITU ULICHONACHO AMBACHO
ADUI ANAKIWINDA
MWL.Peter Francis Masanja
0744056901
BWANA YESU ASIFIWE
Ø Unaweza
ukawa unaombea jambo fulani kumbe adui hakitafti hicho anatafuta kingine kabisa
.
Ø Unaweza
ukawa unaombea uchumi wako kumbe adui anawinda uhai wako .
Nao
wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya;
Na kufikiri hila mchana kutwa.
Zaburi
38:12
Ø Tafta
kujua nini adui anakiwinda kwako ,
Ø Mwulize
Mungu atakujulisha ni nini adui anawinda kwako .
Ø Mtu
wa Mungu , lazima ujue je anawinda nini huyo adui .
v Inawezekana Anawinda:
·
Watoto wako .
·
Afya yako
·
Ndoa yako
·
Uchumba wako .
·
Huduma yako ( utumishi wako aiue )
Ø Halafu
wewe ukajikuta unaombea uchumi tu ambao hawindi kabisa .
Ø Baada ya kujua anachowinda tafta kujua
anatumia mbinu gani na silaha gani .
Ø Adui
anaweza akaja kwa kujifanya rafiki kwako lakini anakuvizia akumalize .
Ø Adui anaweza kuleta mtu asiyesahihi , mchumba
, mke asiye sahihi kwako ili aue huduma yako .
Ø Baadhi ya vijana wamejikuta wanakimbia huduma
na kumwacha Mungu kwa sababu ya maneno yaani kukosolewa katika kila walifanyalo
.
Kijana tambua
kuwa ukiona unasemwa sana na kupigwa vita vya maneno hiyo inamaanisha kuwa adui
anapambana na huduma yako anataka kuiua
kwa kukutia roho ya kukata tamaa.
Ni jukumu lako kuombea huduma yako sasa .
Kabla ya
kuingia kwenye maombi lazima ujue unaombea jambo gani na ni kwanini ❓
Umeona kuna
hitilafu gani mpaka hitaji hilo uliweke kwenye maombi .
Kama hujaona
hitilafu ombea ulinzi na kibali cha Mungu kitawale juu ya eneo hilo .
Baada ya
kujua anachokiwinda adui hakikisha Mungu yupo upande wako .
Unaweza
ukaanza kupambana na adui kumbe Mungu hayupo upande wako ( hayupo pamoja na
wewe) ukajikuta unashindwa kumpiga adui wewe anakupiga .
Ndipo adui
zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande
wangu;
Zaburi 56:9
Maombi ya
kupambana na adui ( maombi ya vita ) yanahitaji ukaribu na Mungu zaidi .
Lazima
umkaribie Mungu ili awe pamoja na wewe katika vita uliyonayo .
Lakini Bwana
yu pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea
watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawakutenda kwa
akili, wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe.
Yeremia 20:11
UFANYE NINI BASI ILI KUHAKIKISHA KATIKA
VITA YA KIROHO ULIYONAYO BWANA AWE UPANDE WAKO ?
Ø Tenda
mema ili Mungu asikuache katika vita ya kiroho uliyonayo .
Ukitenda mema
hakuna wa kukudhuru maana utakuwa unalindwa na Mungu .
Naye
ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?
1
Petro 3:13
Ø Uwe
na desturi ya kuomba toba ( kujitakasa ) mbele za BWANA.
Rejea ZABURI 51
Ø Epuka
maisha ya dhambi , dhambi inakutenga mbali na Mungu , dhambi inamfanya Mungu
akuache na kupigwa na adui .
Ø Israeli walipofanya dhambi Mungu akawaacha ,
wakapigwa sana na kuwa watumwa .
Adui anaweza kukupiga kwa sababu ya maisha ya dhambi
.
Kisha
wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana; Bwana akawatia
mikononi mwa Midiani muda wa miaka saba
Waamuzi
6:1
Ø Kuna
vita mtu inaweza ikamwandama na kuteswa kwa sababu ya mfumo wa maisha fulani
ambao unamzuia Mungu kuwa pamoja naye na kisha adui kuwa na uhalali wa kuleta
mateso .
Ø Maombi
ya vita yanahitaji kujisafisha ( kusafisha njia zako ) .
Hii itamfanya Mungu awaaibishe adui zako .
Mungu
akubariki sana
Karibu katika mwendelezo wa somo hili siku nyingine
Maoni
Chapisha Maoni