UHUSIANO ULIOPO KATI YA ARDHI ,MBINGU NA MAISHA YA MTU KIROHO NA KIMWILI


UHUSIANO ULIOPO KATI YA ARDHI ,MBINGU NA MAISHA YA MTU KIROHO NA KIMWILI


Mwl.Peter Francis Masanja
0744056901 

Mungu akubariki sana wewe uliyepata kibali cha kujifunza somo hili .
Karibu tuendelee .

Tuombe 

Mtakatifu 🛐Mtakatifu 🛐Mtakatifu 🛐
Baba wa mbinguni , tunakushukuru kwasababu ya kibali ulichotupa cha kujifunza somo hili  , tunakuomba ufungue macho yetu ya kiroho ,masikio yetu ya kiroho , fahamu zetu na mioyo yetu tukapate kusikia neno lako katika jina la Yesu .Amen
Inawezekana umeomba mda mrefu sana lakini bado unaendelea kukutana na vita kali sana katika maisha yako .

Hii ni kwasababu hujawahi kumwambia Mungu juu ya ardhi na mbingu mahali unapoishi .
: Naomba tuiangalie ardhi inasifa gani ambazo zinaweza kuathiri maisha yako ya kimwili na kiroho .📖


                   📖 SIFA AU TABIA ZA ARDHI KIROHO 📖
Ardhi katika biblia imeandikwa kwa jina la nchi

Kwahiyo hakuna tofauti kati ya nchi na ardhi .
Nchi ni ardhi yenye mipaka halali ya umiliki .

ARDHI INAMASIKIO


Ardhi inasikia kila kitu ambacho itaambiwa na kukitekeleza kabisa .
Ardhi inaposikia neno inaliandika na kulitekeleza .


 1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitanena; Na nchi isikie maneno ya kinywa changu.
Kumbukumbu la Torati 32:1
: Mungu alipoiumba ardhi aliumba na mbingu akazifanya pamoja haziachani .

Zote zinasikia na akiziita zinamtii
13 Naam, mkono wangu umeuweka msingi wa dunia, na mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo husimama pamoja.
Isaya 48:13
Palipo na ardhi kuna mbingu na ukinena neno juu ya ardhi na mbingu husikia pia kwa maana zipo sawa na pande mbili kwenye  sarafu .
29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.
Yeremia 22:29
30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.

Yeremia 22:30
Ardhi imepewa masikio katika ulimwengu wa roho .
ARDHI INA KINYWA
Ardhi inauwezo wa kumeza na kutapika .
Inauwezo wa kufungua kinywa chake na kuhifadhi mambo mazuri au mabaya .
11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika
ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
Mwanzo 4:11
12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
Mwanzo 4:12

📙 ARDHI INA MACHO

Ardhi ina macho na ni shahidi ya mambo yote ayatendayo mtu na kuyanena , mema na mabaya .
📖 Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;

Kumbukumbu la Torati 30:19
📙 ARDHI NI KITABU CHA KUHIFADHIA MAMBO YANAYOMHUSU MTU , MEMA NA MABAYA

Inaandika na kuhifadhi mema au mabaya .

📖 29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.
Yeremia 22:29
30 Bwana asema hivi,  Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.
Yeremia 22:30
Kuna Wakristo walipohamia maeneo fulani walienda kupata tabu sana katika maisha yao kwasababu ya kuenda kuishi kienyeji bila kumwuliza Mungu ardhi waliyoihamia imebeba nini .
Kuna ardhi zimeandika habari chafu , zimenenewa kwa kila atakayekuja kuikalia lazima apate mateso .
Tafta sana kufahamu siri iliyopo kwenye ardhi utakayohamia kwenda kuanza maisha juu yake .

Hii itakusaidia kujua vita juu ya eneo hilo iko wapi .
Ardhi ikiambiwa kila mtu atakayoikalia augue magonjwa au asifanikiwe au ndoa yake ivunjike au awe mzinzi au awe mlevi au kahaba , au asizae , au watoto wake wasioe wala kuolewa inatekeleza kabisa .
Unaweza ukashangaa kwenda tu kuikalia yakaibuka matatizo maishani mwako .
Maarifa ya kiroho yanahitajika sana ili kung'oa hizo roho chafu ambazo zinasimamia mabaya juu ya ardhi .
Kuna ardhi zingine ukiikanyaga tu , inaanza kukupa ishara kuwa imeugua , ina magonjwa inahitaji tiba .
 ARDHI HUUGUA

Ardhi ikifanyiwa maovu mfano , uganga, uchawi , kupitia tambiko na mazindiko inaugua kabisa na inakuwa na roho za mauti .
: 📖 14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, NA KUIPONYA NCHI YAO.

2 Mambo ya Nyakati 7:14
Pigia mstari neno " na kuiponya nchi yao "
Maovu yakitendeka juu ya ardhi ardhi huugua na kuwa ya tofauti sana
Ardhi iliyougua inawafanya watu wanaoikaa kulala usingizi mgumu

Unalala unamka asbuhi unapiga miayo na uchovu juu yako , unaamka unaenda kazini lakini uchovu unausikia .
Kwahiyo unatakiwa kuwa mtu makini sana katika ardhi unayohamia kwenda kuishi , hata kwenye nyumba ya kupanga .

Angalia maisha ya kiroho ya watu wanaokuzunguka , angalia maendeleo yao ya kiafya , na kiuchumi .

Angalia tabia zao na za watoto wao zikiwa ni mbaya ujue kabisa kunashida kwenye ardhi .
  Kisha ingia kwenye maombi ya toba juu ya ardhi hiyo .
📖 14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.

2 Mambo ya Nyakati 7:14
15 Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.
2 Mambo ya Nyakati 7:15

16 Maana sasa nimeichagua nyumba hii na kuitakasa, ili kwamba jina langu lipate kuwako huko milele; yatakuwako na macho yangu, na moyo wangu daima.
2 Mambo ya Nyakati 7:16
17 Nawe, ukienda mbele yangu kama alivyokwenda Daudi baba yako, ufanye sawasawa na yote niliyokuamuru, na kuzishika sheria zangu na hukumu zangu;
2 Mambo ya Nyakati 7:17

18 ndipo nitakithibitisha kiti cha enzi cha ufalme wako, kama nilivyoagana na Daudi baba yako, nikisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kutawala katika Israeli.
2 Mambo ya Nyakati 7:18
Vunja ile madhabahu iliyosimama juu ya ardhi kusimamia mabaya .

📖 2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;

Kumbukumbu la Torati 12:2

3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.
Kumbukumbu la Torati 12:3
Futa maneno yote na habari zote mbaya zilizoandikwa juu ya ardhi hiyo .


Futa kwa damu ya Yesu .


 7 Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa.

Isaya 7:7

 Mwambie Mungu aitakase hiyo ardhi kwa damu ya Yesu .
22 Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo.
Waebrania 9:22
Damu ya Yesu inamamlaka ya kuitakasa ardhi iliyonenewa mabaya

Maoni

  1. Nimebarikiwa sana na mafundisho kuhusu ardhi mbingu na jinsi mahusiano haya yaniadhirivyo.

    JibuFuta
  2. Nimebarikiwa na mafundisho

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*