ALAMA BARABARANI
ALAMA
BARABARANI
Mwl.Peter Francis Masanja
0679392829
Maisha ya mwanadamu yapo kwenye barabara ambayo
imejaa sheria , kanuni na taratibu amabazo zinatakiwa zifuatwe.
Mungu ameweka alama katika barabara yako ya kiroho.
Zipo alama nyingi sana ambazo zinayaendesha maisha
ya mwanadamu na kujua matumizi ya barabara yake ya kiroho .
Maisha yako ya kiroho ni barabara ambayo Mungu
ameweka alama uzifuate ili uweze kufika salama uendako .
ZIFUATAZO
NI ALAMA ZA KUZINGATIA NA KUZIFUATA KATIKA BARABARA YAKO YA KIROHO
✍ Mtu wa Mungu
unatakiwa kufuata alama hizi ili ufanikiwe kufika katika safari yako ya kiroho(
wokovu ).
1. Utakatifu
Utakatifu ni
alama nzuri sana katika barabara yako ya kiroho. Bila utakatifu barabara yako
ya kiroho itakuwa chafu na itaangamia yaani utapata ajali ya kiroho yaani
anguko .
Nanyi
mtakuwa watakatifu kwangu mimi; kwa kuwa mimi Bwana ni mtakatifu nami
nimewatenga ninyi na mataifa, ili kwamba mwe wangu.
Mambo ya Walawi 20:26
Utakatifu ni alama ya Mkristo aliyehai katika
barabara yake ya kiroho
Japo wakristo wengi huikana hii alama kuwa hawana
katika barabara yao ya kiroho.
Sikiliza nikueleze mtu wa Mungu.
Duniani kuna watakatifu ambaye wa kwanza ni mimi na
wewe hapo Mungu anatuhitaji sana
bali
kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika
mwenendo wenu wote;
1
Petro 1:15
kwa
maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
1
Petro 1:16
Mungu ni Mtakatifu na wanaomwabudu inawapasa wawe
watakatifu yaani wajitakase watubu dhambi zao na kuziacha kabisa .
Kwahiyo alama hii lazima iwepo kwenye barabara yako
ya kiroho.
Kuna baadhi ya wakristo husema hakuna mtakatifu
duniani hasa wanapoonywa kuwa barabara yao ya kiroho imechafuka inabidi
waisafishe.
Maswali haya wanauliza
Inamaana wewe ni mtakatifu ?
Wewe ni nani unanihukumu ?
✍Mpendwa
huhukumiwi unatakiwa ushukuru na kutengeneza njia zako ukaishi maisha
matakatifu .
✍ Tupo katika
dunia ambayo kila mtu anadai anajua neno vizuri anakataa maonyo .
Mtu
akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua.
1
Wakorintho 8:2
✍Katika alama hii
ya utakatifu ni ya muhimu sana kuijua kwa upana zaidi maana vijana wengi
huchafua barabara zao za kiroho kumpa nafasi shetani awamiliki wakisema hakuna
mtakatifu duniani .Kitu ambacho siyo kweli
Watakatifu
waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Zaburi
16:3
Ufalme wa Mungu haumilimiwi na watu ambao hawana
utakatifu .
Lakini
watakatifu wake Aliye juu wataupokea ufalme, na kuumiliki huo ufalme milele,
naam hata milele na milele.
Danieli
7:18
✍ Ufalme wa Mungu
utatekwa na watakatifu , yaani wataumiliki wao .
: Izingatie alama hii ya utakatifu lazima iwepo
katika barabara yako ya kiroho.
2.Neno na
nguvu .
Hii ni alama nyingine katika barabara yako ya
kiroho.
✍ Neno ni alama
nyingine ambayo inatakiwa ionekane katika barabara yako ya kiroho.
✍ Neno
litakufanya ung'are ukilisoma ukalielewa na ukaishi sawasawa na linavyosema.
✍ Alama hii
vijana wanatakiwa waitafte kwa bidii sana na kuhakikisha isifutike mioyoni mwao
.✍ Alama hii ndyo imebeba
nguvu za kiroho na nguvu za ushindi.
Alama hii pia imebeba nguvu ya kukua kiroho na
kuimarika sana .
.... Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna
nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
1
Yohana 2:14
✍ Kijana usalama
wa barabara yako ya kiroho upo ndani ya neno pekee na hilo neno lazima
libadilishe mfumo wa maisha yako .
Maisha yako ya imani , yapo ndani ya neno
Neno ni alama
ambayo inafanya barabara yako ya kiroho iwe safi kabisa na kila mtu atatamani
maisha yako .
11
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Zaburi
119:11
15
Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako.
Zaburi
119:15
16
Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.
Zaburi
119:16
Neno ndyo alama pekee ya Mkristo inayomfanya ashinde
dhambi.
11
Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
Waefeso
6:11
17
Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
Waefeso
6:17
SOMO
LITAENDELEA
Mungu akubariki sana
✍ Mungu
anakuwazia mema
Mungu anataka ulishike neno lake na kulitii na
kuliishi
Maoni
Chapisha Maoni