JIHADHARI NA MAJUTO YA NDOA


                        JIHADHARI NA MAJUTO YA NDOA
Mwl.Peter Francis Masanja
0744056901


UKIPANDA KWA MWILI UTAVUNA UANGAMIVU
 HISIA ZA MAPENZI ZINAKUFANYA UKOSEE KUOA AU KUOLEWA .
Acha vijisababu visivyokuwa na mashiko katika kufanya maamuzi ya kuoa au kuolewa .
📖 Siwezi kumwacha kwa sababu tumetoka mbali sana
Mungu akikataa amekataa wewe ng'ang'ana utavuna ndoa ya majuto .
📖 Siwezi kumwacha kwa sababu nimegharamia mno acha nimuoe tu 🙆🏻‍♂
gharama unayoiona inakusukuma umuoe mtu ambaye si sahihi ni sawa na kumlipa pesa jambazi aje akukate mapanga .
📖 Nampenda mno lazima nimuoe au anioe
Badilisha maamuzi unaweza ukampenda mtu lakini kama Mungu amemkataa acha kabisa itakuwa ni majuto kwako .
📖 Sipati usingizi kwa sababu yake .
Wewe ndye unajikosesha usingizi kwa jambo ambalo Mungu kalikataa unalazimisha kwa hisia za mwili wako
Acha utavuna ndoa ya majuto .
📖 Namwona yeye tu sioni mwingine .
Acha uongo , hisia zisikutawale msikilize Mungu nini anasema juu yako .
Epuka ndoa ya majuto .
📖 Nimenfia
Usiseme umemfia mtu ambaye siye sahihi utakufa ndani ya ndoa .
📖 Namsikia akitembea moyoni mwangu .
Acha uongo subiri mume au mke ambaye Mungu kamwandaa kwaajili yako , mwili wako usikuendeshe.
 📖 Nitaolewa na aliye nizalisha .
Kuzalishwa siyo kigezo cha kuwa huyo ni wako ambaye Mungu alikupangia , tambua hata ulipozalishwa ulimkosea Mungu .
Tulia subiri Mume wako toka kwa Mungu .
📖 Hakuna kijana aliye mwaminifu siku hizi
Kauli hii ukiishika itakuletea ndoa ya majuto , utamtilia mashaka mwenzi wako .
🖊 KWANINI VIJANA WENGI WANACHAFUANA KABLA YA NDOA
Kuchafuana kunaleta ndoa ya majuto .
Ø  ZIPO SABABU ZA KIMWILI AMBAZO VIJANA WENGI HUDHANIA NI FAHARI KUMBE NI MAJUTO BAADA YA KUINGIA KWENYE NDOA .
1.      Wanaimarisha mahusiano ( urafiki wao )
2.       Kujamiana ndiyo uhakika wa kwamba unampenda mwenzako .
3.       Kujamiana kabla ya ndoa ni kumfanya mwenzako atulie kwako asiende kwa wengine .Eti umfanye awe wako tu .
4.      Baadhi ya wasichana huona ndiyo njia ya kumfanya kijana wa kiume amkubali lakini mwisho wake anaishia kuachika .
5.       Wasichana hujamiana ili wapate mimba na mwishowe wang'ang'anie kuolewa na mwanaume kwa kisingizio cha mimba .






🖊 MADHARA YAKE




📖 Baadhi ya wasichana wanadharauliwa na kuachika na kuachwa na maumivu makali hata mimba pia.
📖 Kukosa hofu ya Mungu .

Wanamkosa Mungu
Mwanzo 39:9

Zinaa ni dhambi inayomtoa Mungu kwa mtu na kumwacha peke yake .
📖 Kuondoa akili ( ufahamu mzuri ) .
Mithali 6:32_33
📖 Hata wakiingia kwenye ndoa bila toba ndoa yao Mungu ataitapika kwa sababu hawajautubia uasherati wao .
Waebrania 13:4
📖Wakizaa watoto katika hali hiyo , watoto wao watakamatwa na roho ya uzinzi /uasherati , na matokeo yake utaona binti zao wanazalia nyumbani bila kuolewa .
Zaburi 51:5

Unapoona mwanao kazalia nyumbani jihoji wewe kabla ya ndoa hukuwa mwasherati na je ulitubu

Kama hukutubu umehatarisha maisha ya wanao kwenye eneo la ndoa .
📖 Haya yote ukiyaepuka utakuwa na ndoa isiyo na majuto .
Utasikia binti anaambiwa Usipo nipa sikuoi nakuacha maana naona umenibania 🤣🤣🤣🤣
Mwambie kwamba nashukuru kwa sababu Mungu kanidhihirishia kwa maono kuwa wewe hunifai nenda kwa makahaba watakubali unavyotaka ,mimi namsubiri mume wangu toka kwa BWANA.

NITAMJUAJE KAMA NDIYE WANGU KUTOKA KWA MUNGU

Swali hili ni zuri sana na ni rahisi sana kwa kulijibu

📖 18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanzo 2:18
Vijana wengi hukosea ramani kuisoma hasa wanapotaka wenzi wa ndoa .
[ Kumpata mwenzi sahihi lazima ufuate kanuni kama mtu asomavyo ramani , kuna ufunguo ( kiongozi ) ambaye ni Mungu

Kazi yake ni kukuonyesha yule unayemkusudia amebeba nini kiroho , amebeba tabia zipi na vipaumbele gani katika maisha yake .

Je hivyo vitu vinaelekeana na vyako
3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?
Amosi 3:3
Mungu hajaahidi kukuletea mtu asiyefanana na wewe lakini akili zako na macho yako ( mwili) ukiufuata unaweza ukakuletea mtu asiyesahihi kabisa na kujutia kuoa au kuolewa.
Aliye sahihi mtaendana interest ( vitu mvipendavyo ) siyo huyu anapenda miziki ya kidunia halafu wewe unapiga kwaya hiyo ndoa itakuwa ya kisiasa , chama tawala na chama pinzani .
Huyu haamini kuwa zinaa inashindwa halafu wewe unaamini na unaipiga vita , hapo ujue kabisa huna mtu  jifariji ujuavyo .
Wewe unafunga na kuomba yeye hizo habari anazipinga hawezi kujitesa , hapo pia ujue unaoa au unaolewa na mtu asiye na maono mda wowote utalia .
Wewe ukiongelea mambo ya kiroho anakuingizia mambo ya kidunia kubishana na wewe , huyo siyo wa kufanana na wewe .
: Aliye sahihi mtania mamoja , mtaombea mahusiano yenu , atakushauri mambo ya kiroho na kukuambia piga injili mpaka dunia ishangae .Atakushirikisha ratiba na mambo ya kiroho anayojifunza .

Mtacheka 🤣🤣mtafrahi , mtaimba Zaburi .
Kila mtu atamkumbuka mwenzake na kumwona wa thamani sana na ni zawadi toka kwa Mungu





Siyo unakuwa na mtu anajifanya kaisari mpaka na shetani anamshangaa amezidi viwango
Baada ya wiki kaingiza gia ya kwazo mpaka utajuta kumjua .
USIVAE SHELA BILA KUTUBIA ZINAA

Kama mmejuana kabla ya ndoa msivae shela harusini Mungu ataiadhibu ndoa yenu .
Tubuni ndiyo mvae hiyo shela ili ndoa yenu isiwe ya majuto .
Kwanini shela isivaliwe na watu ambao wamejuana kabla ya ndoa
Kwasababu tafsiri ya kuvaa shela ni ubikra , je unapoivaa halafu hujatubia zinaa humdhihaki Mungu


Hapo ndiyo maana ya kwamba usivae shela kama mmejua kabla ya ndoa, tubu ili uvae usipotubu ndoa inaweza ikapigwa .
Mungu akubariki sana nitaendelea siku nyingine kwa ufafanuzi zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*