📖 JINA ULILOPEWA LINA MAANA GANI KIROHO ❓
📖 JINA ULILOPEWA LINA MAANA GANI KIROHO ❓
Mwl.Peter
Francis Masanja
0679392829
📖
Nilipokuwapo
pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana
mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
Yohana
17:12
✍ Yesu alipewa jina kubwa sana kiroho na jina lenye
nguvu za kuokoa litajwapo mashetani hutetemeka.
✍ Jina la Yesu lina mamlaka na nguvu za kushinda
ufalme wa giza.
📖
Wala
mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba
mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi
tulivyo.
Yohana
17:11
Jina ulilopewa yaani jina la ukoo lina maana
gani ❓
✍ Kuna majina ya ukoo yanaambatana na miungu ya ukoo
✍ Jina ulilopewa nyumbani yaani jina la asili
linaweza likawa limebeba tabia mbaya na roho za miungu zitakazo sumbua maisha
yako.
✍ Jina la ukoo lina tabia , fuatilia kujua tabia
zake,✍ Unaweza kupewa jina la
babu yako aliyekuwa mganga , mchawi, mlevi , mzinzi , mgomvi n.k halafu hizo
tabia zikajitokeza kwako pia .
✍ Shughulikia tabia chafu za jina ulilopewa
📖 9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha
mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Wafilipi
2:9
10
ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani,
na vya chini ya nchi;
Wafilipi
2:10
✍ Yesu alipewa hilo jina likiwa na maana kubwa sana
na nguvu za kuokoa
✍ Jina lipitalo kila jina
✍ Jina lenye nguvu kupita majina yote .
Ombea jina lako ulilopewa na ukoo wako
inawezekana kunashida inakutesa kwa sababu ya jina ulilopewa.
Kuna
watu wanaitwa Shida , mateso , na wengine majina ya wanyama wamejikuta wanapata
ugumu katika maisha yao .
Tumia jina la Yesu kufuta tabia chafu za jina
ulilorithi
Kuna wengine walinunua majina ya watu kusomea
, futa tabia chafu za hilo jina .
Haiwezekani
usomee jina la mtu bila kujua tabia zake ,
Aliachaje
shule na kwanini aliacha
Usije
ukaanza kupata misukosuko katika masomo kama yake .
Kumbuka
wengine waliacha masomo kwa sababu waliugua sana mara kwa mara .
Unaweza
ukalirithi hilo jina ukawa wa kuugua mara kwa mara .
Nakutakia asbh njema .
Maoni
Chapisha Maoni