KUHUSU MARAFIKI

*PUNGUZA MZIGO, PUNGUZA MARAFIKI FEKI PUNGUZA KABISA TENA WAPUNGUZE SANA TU;WAPUNGUZE ILI UWE MWEPESI*

*Punguza marafiki ambao ukiwaambia unataka kufanya kitu wanakujibu "utawezaaa?" Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao kutwa wanataka mchafue meza bar. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao umeongea nao kitu mkiwa wawili mwisho wa siku unakikuta kimeenea sehemu nyingine. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao wako right kila siku wenyewe hawataki kuambiwa wamekosea. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao wakija kwako wao urafiki unahamia kwa mumeo au mkeo aliyekaa sebuleni wakati wewe kakuacha nje. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao wanakuwa na urafiki na maadui zako kwa ukaribu zaidi. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki wa kwenye raha tu ukiwa na shida unajikuta peke yako. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki wanaokusifu huku wakijua umekosea. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao kila ukiwapigia simu na wao utawasikia yaani nilitaka kukupigia sasa hivi. Punguzaaaa!*

*PUNGUZA MIZIGO ISIYOKUWA NA UMUHIMU*

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*