LAZIMA UJUE TOFAUTI KATI MTU NA MWANADAMU
🍇 LAZIMA
UJUE TOFAUTI KATI MTU NA MWANADAMU 🍇
Mwl.Peter
Francis Masanja
0679392829
✍
Mtu anatabia ya kimungu ndani yake .Amebeba utu ( matendo ya haki ).
✍
Mwanadamu amebeba tabia za mnyama ( anatenda mambo kama mnyama ) .Kila kitu
kwake kufanya ni sawa tu .
✍ Mwanadamu anaroho ya
uasi ndani yake na anafanya uadui na Mungu .
📖
26
Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki
wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye
kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mwanzo
1:26
✍
Mtu anasura na mfano wa Mungu yaani utendaji wake ndani yake .
✍
Mwanadamu yeye anaunyama ndani yake
Akijisikia
aoe wake wengi anaoa , akijisikia akalewe au akanunue makahaba anaenda tu
kwasababu anasifa kama mnyama .
📖 1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa
nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo
6:1
2
wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia
wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo
6:2
3
Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye
ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
Mwanzo
6:3
✍ Katika kitabu cha
Mwanzo 6:1_3 , Mungu anawazungumzia wanadamu kwa tabia ya kinyama na siyo tabia
ya utu ( kutenda kama Mungu atakavyo ) .
Hajasema
kwamba hatashindana na mtu au watu
Amesema
hatashindana na mwanadamu ( wanadamu ) .
✍
Mungu pia anasema watu wake wanaangamia kwa kukosa maarifa hajasema wanadamu
wanaangamia kwa kukosa maarifa .
📖 6 Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa
maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe
kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami
nitawasahau watoto wako.
Hosea
4:6
✍
Alizungumzia watu akimaanisha wanaofuata sheria zake ( watakatifu ) .
✍
Ndyo maana leo pia tunaona makanisani kuna wanadamu wamejiingiza huko kuleta
roho ya uasi .
✍
Ndyo maana leo tunaona mtu anachumbiwa na mwanadamu na siyo mtu 🤣🤣🤣🤣
✍
Hakikisha marafiki zako ni watu na siyo wanadamu ,wanadamu hawana utu
✍
Hakikisha mchumba wako awe mtu asiwe mwanadamu
Akiwa
mwanadamu atatenda kama mnyama na haoni aibu kukufanya mke wa pili .
🙏Somo
limeishia hapo 🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
Maoni
Chapisha Maoni