MAOMBI YA TOBA JUU YA URITHI MBAYA


           MAOMBI YA TOBA JUU YA URITHI MBAYA

SEHEMU YA KWANZA
Mwl.Peter Francis Masanja
0679392829
0744056901

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Kutoka 20:5
Bwana Yesu asifiwe.
Karibu sana katika mwongozo wa maombi haya ambayo nimeyaandaa ili yaweze kukusaidia katika maisha yako na rafiki zako pia .
Roho wa Mungu amenigusa kuandika haya maombi ili yaweze kukufungua pale unapoona kuna shida lakini umeshindwa kujua namna ya kuingia katika toba.
Katika maombi haya nataka nikupe onyo kwanza kwamba maana ya toba ni kukubali kuachana kabisa ulichokuwa unakitenda na kuamua kukaa karibu na Mungu muumba mbingu na nchi,aliyeumba vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.
Nakusihi sana na narudia kukusisitiza kwamba unapotubu hakikisha hurudii tena hiyo dhambi.
Maishani mwako kuna mambo mengi sana ambayo yanamchukiza Mungu na mengine uliyafanya kwa makusudi ukisema kwamba utatubu tu bado upo kwenye neema.
Pia kuna mengine ambayo wewe hukuyafanya katika maisha yako lakini yalifanywa na ndugu zako au wazazi wako .Mungu akaachilia adhabu juu ya maisha yenu katika familia yenu au ukoo wenu.
Adhabu za kurithi ni pamoja na magonjwa na tabia ambazo ni aibu mbele za Mungu na mbele za watu kuzisimulia kabisa maana hazifai kuigwa hata na watoto wako au jamii inayokuzunguka.
Basi leo naomba tushirikiane kuomba kwa pamoja maombi haya ili upate kufunguliwa popote ulipo.
Nakuomba sana uyasome maombi haya ili uweze kufunguliwa kwenye shida na mitego mbalimbali ambayo shetani ameiweka juu yako ili akutese.
Nikukumbushe kwamba mateso mengi anayopitia mtu ni matokeo ya dhambi.Mfano kuna baadhi ya dhambi kama utoaji mimba na ukahaba huwa zina matokeo mabaya sana katika ukoo na ndiyo maana utakuta kuna ukoo watoto ni makahaba au wazinzi sana kuanzia kipindi wanapopevuka tu wanaanza kuwajua wanaume bila aibu kabisa.
Pia utaona jinsi gani watu wanaotoka kwenye hizo familia wengi mahusiano yao huwa hayadumu na ndoa zao huwa za tabu sana.
Kabla ya kuyatumia maombi haya hakikisha unamwimbia Mungu wimbo wa kuabudu.

MAMBO YA KUOMBEA TOBA
Ø  Zinaa
Ø  Kuabudu miungu mingine kama vile kwenda kwa waganga.
Ø  Ardhi ambapo unaishi kwa sasa.
Omba toba juu ya miungu inayoabudiwa mahali hapo kwa kujua au kutokujua.
Ø  Ardhi ya nyumbani ulipozaliwa.
Ø  Ardhi ya eneo unapofanyia kazi.
Ø  Ardhi ya Kanisa unapoabudia.
Ø  Tabia mbaya ulizorithi kutoka kwa wazazi
Kuna tabia za wazazi wetu kweli haziridhishi na hazifai kuigwa kabisa.

7 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.
Maombolezo 5:7

Ø  Majina ya kurithi.
Kuna baadhi ya majina ya kabila mtu anayopewa yanaambatana na miungu ya ukoo na roho za miungu kama vile uchawi na ushirikina ,ulevi,ukahaba,uzinzi,n.k
Hakikisha sana unaomba toba juu ya majina hayo na kuondoa kabisa uhusiano wa hayo majina na tabia chafu, uhusiano wa hayo majina na roho za miungu ,uhusiano wa hayo majina na roho za magonjwa na umaskini,n.k.
Kuna baadhi ya watu wamepewa majina ya wanyama ,hii imewafanya wawe na tabia kama wanyama hao na kujikuta wanafanya mambo ya kuchukiza yaani maovu.
Ø  Nafasi ya kazi uliyoirithi
Kuna nafasi nyingi za kazi mtu hurithi baada ya kutoka mtu aliyekuwa katika nafasi hiyo.Nafasi hizo huwa zinamatatizo kama mtu aliyetangulia alitenda dhambi na adhabu ikaja katika eneo hilo kuleta mateso.
Zipo ofisi na kampuni ambazo ma meneja huwa wakija baada ya miezi michache wanakimbia kazi au wanakufa kabisa ,hii ni kwasababu katika nafasi hiyo kuna roho ya uharibifu imemwagwa ili kila atakayeikalia apate mateso.Omba toba juu ya nafasi ya kazi ambayo umekuta mtu kahama au kafariki halafu wewe ukaenda kuichukua.Usiingie kienyeji ukakaa tu .Takasa ardhi ya hapo na kuondoa miungu iliyosimama mahali hapo kufanya vita na kiti ulichokikalia .
Angalia Daudi alipoichukua nafasi ya Sauli kutawala ,kulikuwa na njaa kubwa sana katika Izraeli kwa sababu ya Sauli.
Daudi aliona njaa inazidi kutesa utawala wake ikabidi amwulize Mungu .Ndipo akaambiwa ni kwasababu ya Sauli.

1 Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni.

2 Samweli 21:1
Usipuuzie matatizo unayoyaona yanajirudia katika nafasi unayoikalia,mwulize Mungu .


TWENDE TUINGIE KWENYE MAOMBI NAKUOMBA UYASOME UMAANISHE

1.Toba binafsi

Ee MUNGU baba ,nimekuja mbele ya kiti chako cha rehema ,nakushukuru kwa kuwa umenjalia uzima na afya .Ninakushukuru kwa kuwa wewe ni mwema,umenichagua hivi leo kuzungumza na wewe sawasawa na ISAYA 1:18-19

18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

Isaya 1:18

19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;
           
Isaya 1:19

Ninakuja mbele zako maana nimesikia habari zako kuwa wewe ni Mungu unayesamehe na kufuta makosa ya wakuitao.
Ninaomba toba juu ya dhambi zote nilizozitenda kwa kujua na kutokujua .Nakuomba unirehemu ,unioshe kabisa kwa damu ya Yesu .
Maana nimejua ya kwamba nimekukosea na hasira yako ikawaka juu yangu.
Ninakuomba ,kuanzia sasa,unisafishe ,unitakase,unioshe dhambi zote nilizozitenda ,katika jina la Yesu ,nakusihi Ee Mungu unisamehe kabisa sawasawa na ZABURI 51:1-10 kama ilivyoandikwa:


1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.

Zaburi 51:1

2 Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu.

Zaburi 51:2

3 Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima.

Zaburi 51:3

4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu.

Zaburi 51:4

7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji

Zaburi 51:7

8 Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi.

Zaburi 51:8

9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; Uzifute hatia zangu zote.

Zaburi 51:9

10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu

Zaburi 51:10

Nakuomba Mungu unisamehe juu ya dhambi zote kupitia damu ya Yesu nafuta dhambi za kutumikia miungu, kutokusamehe,n.k( TAJA MAMBO YOTE ULIYOYAFANYA MWENYEWE AMBAYO YANAMCHUKIZA MUNGU) katika jina la Yesu nakuomba usikie kuomba kwangu.Amen

2.Toba juu wazazi na mambo yote waliyoyafanya ukayarithi.

Katika jina lipitalo majina yote ,jina lenye nguvu kupita majina yote la BWANA Yesu Kristo.
Mungu mwenye rehema ,ninakuja mbele zako nikiomba toba juu ya wazazi wangu ,inawezekana kuna maovu walikutenda na hasira yako ikashuka juu yao na juu yangu.
Nakuomba sasa uwasamehe na kuwaponya na kila roho ya mauti ,inayofuatilia maisha yao ,roho ya magonjwa,roho ya kukataliwa,roho ya umaskini,roho ya zinaa,roho ya miungu n.k kwa damu ya Yesu ninafuta kila roho chafu nilizozirithi kutoka kwa wazazi wangu,katka ukoo wa baba na ukoo wa mama yangu ,maana neno lako Mungu linasema:
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu  mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Kutoka 20:5
Ninafuta dhambi zote walizozitenda ,zikatesa maisha yangu ,ninazifuta kuanzia kizazi cha kwanza ,na cha pili ,na cha tatu na cha nne na kuendelea katika maisha yangu  kwa damu ya Yesu ,kila dhambi za urithi nazifuta sawasawa na neno la Mungu linavyosema katika Waebrania 9:22-23
22 Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo.
Waebrania 9:22
23 Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo.
Waebrania 9:23
Ninafuta kila urithi wa mabaya kutoka kwa wazazi wangu kwa damu Yesu ,ninajitoa          huko mwili wangu,nafsi yangu,na moyo wangu kila kitu kinachohusu maisha yangu natoka huko kwa damu ya Yesu.
Kila asili na historia mbaya ya kurithi kutoka kwanza wazazi wangu naifuta kwa damu ya Yesu sawaswa na Ezekieli 16:3-6,9
 3 useme, Bwana MUNGU auambia Yerusalemu hivi; Asili yako na kuzaliwa kwako kwatoka katika nchi ya Mkanaani; Mwamori alikuwa baba yako, na mama yako alikuwa Mhiti.
Ezekieli 16:3
4 Na katika habari za kuzaliwa kwako, siku ile uliyozaliwa, kitovu chako hakikukatwa, wala hukuoshwa kwa maji usafishwe; hukutiwa chumvi hata kidogo, wala hukutiwa katika nguo kabisa.
Ezekieli 16:4
5 Hapana jicho lililokuhurumia, ili kukutendea lo lote la mambo hayo kwa kukuhurumia; lakini ulitupwa nje uwandani, kwa kuwa nafsi yako ilichukiwa, katika siku ile uliyozaliwa.
Ezekieli 16:5
6 Nami nilipopita karibu nawe, nikakuona ukigaagaa katika damu yako, nalikuambia, Ujapokuwa katika damu yako, uwe hai; naam, nalikuambia, Ujapokuwa katika damu yako, uwe hai.
Ezekieli 16:6
9 Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nalikuosha kabisa damu yako, nikakupaka mafuta;
Ezekieli 16:9
Kwa damu ya Yesu ,nafuta kila asili mbaya inayotesa maisha yangu,katika jina la Yesu ,Ee Mungu usikie kuomba kwangu ,maana wewe ni kimbilio langu na mwamba wa wokovu wangu na wewe pekee ndye msaada wangu ,nifunike kuanzia sasa na hata milele.Amen.

MUNGU AKUBARIKI SANA
Nakuomba uendelee kufuatilia somo la maombi haya
Pia waweza kunipigia simu kwa ushauri na maombi
0744056901/0679392829










Maoni

  1. Nimebarikiwa sana na maombi haya,Mungu wa Mbinguni azidi kukuinua zaidi na zaidi Mtumishi

    JibuFuta
  2. Amina mtumishi kwenye maombi haya ukoo wangu kuna mambo ya kurithi yanatuumiza hasa wanawake ukiolewa ni matatizo kila kukicha. Ukifika miaka arobaini ndoa zinavunjika

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*