NAJUTA KUMJUA


😭 NAJUTA KUMJUA 😭😭


Mwl.Peter Francis Masanja
0679392829


Ni ujumbe mzito uliojaa simanzi na kuchoma mioyo ya vijana .
Maadamu upo duniani wewe ni kijana kuna watu ulijuta kuwajua .
Unaona ni heri usingewajua kabisa ukawa na amani moyoni mwako .
Naam , hii ndiyo dunia tambua hujaja duniani kuishi bila kukutana na upinzani.
Unaona ni heri usingewajua kabisa ukawa na amani moyoni mwako .
Naam , hii ndiyo dunia tambua hujaja duniani kuishi bila kukutana na upinzani.
Kuna wakati Mungu alijuta kumweka Sauli awe mtawala mpaka akachukua maamuzi magumu ya kumng'oa kwenye ufalme na kumchagua Daudi atawale .
Wewe wajuta kuwajua baadhi ya watu , tambua kuna wakati Mungu anajuta pia kukuita wewe mwanaye .

📖 Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha.

1 Samweli 15:11

Kuna wakati kweli unajuta kuwajua baadhi ya watu kwa sababu wamekuingiza katika shida na tabu , maisha yako wameyaweka matatani yamekuwa magumu.

Lakini nakuambia usijutie hilo ni fundisho utafundisha na wengine wapate kujihadhari namna ya kuchagua marafiki wa kuambatana nao .
Mungu alijuta kwanini alimchagua Sauli atawale , mpaka akamtumbua madarakani kwa nguvu .
Inawezekana na wewe kijana Mungu anakuangalia na kujuta kwanini ulikiri kuacha dhambi siku unampokea Yesu ukisema ninamkataa shetani na kazi zake zote .
Lakini anakuangalia anakufananisha na Sauli .
Kuna wakati pia hata wewe unajuta kwanini uliolewa na yule au kwanini ulimuoa huyo , yaani anakusumbua na kuleta mawazo kwako kuna wakati unawaza ukimbie .🏃🏻‍♂🏃🏻‍♂
Majuto unayopitia Mungu ameyaona atayatatua , huhitaji kujuta omba Mungu akupe amani maana yeye ni Mfalme wa amani .

JEHOVAH SHALOM

Kuna wakati pia unajuta kumjua rafiki yako wa kiume yaani boyfriend alikupa ujauzito akakutelekeza .Akakuachisha masomo


Sikiliza  usijute binti , yupo Mungu amekuandalia mume wako wakati ukifika hutaona kujuta kwako .
Na sasa nakuambia acha kujuta .
Yupo Mungu mpaji anampa mtu apendavyo
JEHOVAH JIREH

📖 20 Tazama, nimepewa amri kubariki, Yeye amebariki, nami siwezi kulitangua.
Hesabu-Numbers 23:20

: Balaamu alitumwa akawalaani Israeli lakini akakutana na neno la Mungu limesimama kinyume chake .

Alipotaka kuweka laana akakuta zimewekwa baraka .
Adui yako ukimjua wewe sema na Mungu tu , huhitaji kujuta kumjua acha Mungu amshughulikie .
Aliyekusaliti usijute kumjua shukuru kumjua kwasababu ungeendelea naye angekuua , tambua Mungu kakuepusha na matatizo .
Cha kujutia duniani ni anguko yaani dhambi , yakupasa utubu na kuiacha kabisa maana inatoa uhusiano wako na Mungu .

📖 9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; Uzifute hatia zangu zote.
Zaburi 51:9

11 Usinitenge na uso wako, Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
Zaburi 51:11

Dhambi pekee inakuletea majuto kwa sababu inamwondoa Mungu kwako .
Adui ni mtaji na ni mtumwa wako wa baadae ,
Usijute kumjua anayekupiga vita
Vita vya maneno , na kukufanyisha kazi ngumu au kukudhihaki baada ya kukufanyia ubaya akaanza kukucheka 🤣
Ipo siku atakuja analia umsaidie .
Yusufu , aliuzwa Misri kwa Potifa kuwa mtumwa lakini alifanikisha nyumba ya Potifa mpaka akaambiwa vitu vyote aguse lakini mke asiguse.

Yusufu alipata kibali machoni mwa Mungu pamoja na majuto aliyopitia .
Hata wewe leo mtu aliyekuumiza ni sawa na mmisiri tu lakini ipo siku atakuona umeinuliwa na ataanza kushangaa
Na kuanza kusema Oooh huyu alikuwa rafiki yangu lakini saivi mmmmh kafanimiwa mno au kaolewa au kaoa.

📖 Kisha Bwana akawapa raha pande zote, sawasawa na hayo yote aliyokuwa amewaapia baba zao; wala katika adui zao wote hakusimama hata mtu mmoja miongoni mwao mbele zao; yeye Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Yoshua 21:44

: Mungu atakupa raha isiyokoma , na yule aliyekufanya ujute hutamkumbuka tena.
Historia ya aliyekuumiza nafsi yako , yaani aliyekuingiza kwenye tabu na dhiki utaisahau saa inakuja Mungu atakujaza furaha na mafanikio .
 Hupaswi kusema unajuta kumjua , cha kufanya muombee ipo siku atakuja kutambua kwamba alifanya makosa na atatubu .
Ipo siku atakukumbuka hupaswi kujuta .
Kuna wakati Mungu anamleta yule aliyekufanya ujute ili audhihirishe ukuu na uweza wake .Akutoe kwenye hiyo shida ili liwe fundisho kwa wengine wapate kumwamini kuwa yeye yupo .Na yote kwake yanawezekana .

📖 37 kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.
Luka 1:37

Unayejuta kumjua pia atakuja apate fundisho kupitia wewe .
Mungu anakuwazia mema kila wakati


Yeremia 29 :11

Asantee tutakutana siku nyingine kuendeleza somo hili .
Najuta kumjua
Ndiyo ujumbe wa leo ambao unazungumzia mambo yanayogusa mioyo ya watu na kujutia kuwa na marafiki wabaya
Lakini ni fundisho kwa uliyemjua na kwako pia ikifika saa ya kuinuliwa kwako .
Faida ya ujumbe huu ni kuwa

Marafiki waliokuumiza ni fursa ya kuinuliwa kwako .



Mungu akubariki sana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*