OKOKA KATIKA MAMBO YOTE
📖OKOKA KATIKA MAMBO
YOTE 📖
Mwl.Peter
Francis Masanja
0679392829
Kuokoka
ni kukataa ubaya .
Kuokoka
ni kukataa uvionavyo vizuri lakini ni machukizo kwa Mungu.
Kuokoka
ni kuishi maisha matakatifu.
Kuokoka
ni kuishi kama Kristo alivyoishi .
Kuokoka
ni kusoma neno na kulifanyia kazi na kuliishi.
Kuokoka
ni kutubu na kuacha dhambi usirudie tena .
Kuokoka
ni kufunga na kuomba .Kama hufungi na kuomba bado hujaokoka .
Kuokoka
ni kuachana na marafiki waovu na kutafta marafiki watakao kufanya ukue kiroho.
Kuokoka
ni kuacha kuabudu miungu na kuamua kumwabudu Mungu aliye hai , Muumba mbingu na
nchi .
Kuokoka
ni kumpenda Mungu
📖
15
Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia,
kumpenda Baba hakumo ndani yake.
1
Yohana 2:15
16
Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na
kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
1
Yohana 2:16
✍Kinywa
chako kiokoke .
Epuka
matukano na matusi wewe umeokoka acha .
Epuka
mizaha .
✍ Moyo wako uokoke
Epuka
hasira na chuki na kinyongo
Acha
wewe umeokoka .
📖
15 Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia,
kumpenda Baba hakumo ndani yake.
1
Yohana 2:15
16
Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na
kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
1
Yohana 2:16
✍Epuka
mazungumzo mabaya
📖 Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu
tabia njema.
1
Wakorintho 15:33
✍Epuka
mavazi yaaibu ni dhambi
Acha
kabisa ,
✍Mwili
wako uokoke
Wapo
watu wanaangalia uvaaji wako ili wamkubali Yesu , vaa vizuri usiwazuilia kuja
kwa Yesu .
Mungu
akubariki sana
Maoni
Chapisha Maoni