TAHADHARI KWA BINTI ZETU


TAHADHARI KWA BINTI ZETU

Kutoka kwa MWL.Peter Francis Masanja


Vashti alikuwa mwanamke mrembo , yaani mzuri sana wa kuvutia
Uzuri wake ulimfanya amdharau mumewe
Mfalme  Ahasuero
 Tupo katika dunia hii ambayo mwanamke akisifiwa mzuri na kila mtu anaweza akamdharau mumewe akisema hata mkiachana yeye hatachelewa kupata bwana .

Uzuri na mvuto wa mwanamke hauifanyi ndoa idumu bali tabia njema ndyo uimara wa ndoa .
  Esta , alikuwa mwanamke mrembo mzuri sana na kila mtu alimtaka naye alijua kabisa kuwa ni mzuri
Lakini Esta alikuwa mwombaji na mwombolezaji ( mcha Mungu ) ,  mpole ,mnyenyekevu , mtiifu, na mwenye kumsikiliza mumewe na watu wote .
Ahasuero akamuoa mrembo Esta akaachana na Vashti .
Uzuri wa mwanamke bila kujitoa kwa Mungu haunafaida kabisa na huambulia kuwa pango la wazinzi na waasherati.
 📖 11 wamlete Vashti, malkia, mbele ya mfalme, amevaa taji ya kifalme; ili kuwaonyesha watu na maakida uzuri wake, maana alikuwa mzuri wa uso.
Esta 1:11
12 Bali Vashti, malkia, alikataa kuja kwa amri ya mfalme kwa mkono wa wasimamizi-wa-nyumba; kwa hiyo mfalme akaghadhibika sana, na hasira yake ikawaka ndani yake.

Esta 1:12
 Vashti alika alimdharau mumewe
 Hii ni kwa sababu alijiinua sana huyu Vashti

Lakini Esta, mwanamke aliyejaa upendo , huruma , upole , utii, na ucha Mungu na uzuri wake alisifika sana na akawa mkombozi wa watu .
 📖 7 Naye alikuwa amemlea Hadasa, yaani, Esta, binti wa mjomba wake, kwa kuwa hana baba wala mama. Naye msichana huyu alikuwa wa umbo mzuri na uso mwema ; nao walipokufa baba yake na mama yake, yule Mordekai alimtwaa kuwa binti yake yeye.
Esta 2:7
8 Basi ikawa, wakati iliposikiwa amri ya mfalme na mbiu yake, wasichana wengi wakakusanyika huko Shushani ngomeni mikononi mwa Hegai; Esta naye aliingizwa katika nyumba ya mfalme, mikononi mwa Hegai mwenye kuwalinda wanawake.
Esta 2:8
9 Yule mwanamwali akampendeza, akapokea fadhili kwake; naye akampa upesi vifaa vya utakaso, pamoja na posho zake, na vijakazi saba walio haki yake, wa nyumbani mwa mfalme. Pia akamhamisha yeye na vijakazi wake akawaweka mahali pazuri katika nyumba ya wanawake.

Esta 2:9
15 Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, yeye hakutaka kitu, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake . Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona .

Esta 2:15
16 Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero,…

MUNGU AKUBARIKI SANA




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*