UWEZO WA DAMU YA YESU KATIKA KUSHUGHULIKIA NA KUONDOA MIUNGU INAYOTESA MAISHA YETU


UWEZO WA DAMU YA YESU KATIKA KUSHUGHULIKIA NA KUONDOA MIUNGU INAYOTESA MAISHA YETU
Semina
Day 2.   Mwl.Grace Elirehema

Ø  Unaposhughulika na miungu ya ukoo shughulika na majina ya ukoo.Kama unatoka koo za kifalme shughulikia miungu ya kifalme iachie maisha yako.Pia shughulika na miungu ya eneo (miungu ya kigeni).
Ø  Shughulikia miungu ya marafiki zako na miungu ya wapenzi wako uliozini nao.
Ø  Shughulika na miungu ya ndoa za wake wengi.
                    WAAMUZI 5:8
Walichagua miungu mipya ,Ndipo kulikuwa na vita malangoni………”
                KUTOKA 3:1-14
Ø  Kila unapoomba takasa hilo eneo kwa damu ya Yesu .
Ø  Misri inayozungumziwa hapa ni ardhi ambapo unaishi
Ø  Bwana ameyaona mateso,na maumivu.Maumivu yanawasimamizi.
Ø  Ombea malango ya mafanikio.
Mtu ana malango yake ya mafanikio.Hakikisha unapambana sana shetani asiyamiliki malango yako ya mafanikio.
Ø  Pambana na mikono ya adui zako ikuachie.
Mungu amekuahidi atakuingiza kwenye eneo zuri kabisa .
           KUTOKA 12:1-13
Mungu alikuwa anawasemesha juu ya sadaka.
Unapomwaga damu ya Yesu .Mungu anashuka kuharibu kila kitu kibaya kinachosumbua maisha yako ,kila roho za miungu na madhabahu zitaondolewa.
Kila mahali uingiapo weka damu ya Yesu na miili ya watu wako .
Ø  Achilia damu ya Yesu kwenye nguvu za miungu na kwenye ibada za miungu.
Ø  Uiachiliapo damu ya Yesu ,Mungu anapita katika eneo hilo
         KUTOKA 12:12-14
Ø  Kama adui amepita kwenye malango ,achilia damu ya Yesu ipite kuondoa kila roho chafu ( mapepo).
Ø  Damu ya Yesu inapomwagwa inafanya hukumu na kuondoa miungu ya makabila.
Ø  Damu ya Yesu ikipita huondoa
·         Maumivu
·         Mateso
·         Kilio
·         Watesi
Kuna wakati miungu hukaa kwenye vitovu vya watu.
            KUTOKA 12:23
Ø  miungu huwa inasababisha uharibifu katika maisha ya mtu kama vile urafiki,umoja,shule,mali n.k
Mharibifu hataharibu tena
             WAKOLOSAI 2:15
Damu ya Yesu ina nguvu za kupambana na enzi na mamlaka ya nguvu giza.
             1 WAKORINTHO 5:7
Kristo alijifunua katika agano la kale ,lakini hawakutambua,akaja kujifunua katika agano jipya.
              ZABURI 82:1,8
Katikati ya miungu atasimama na kuhukumu
Mwambie Mungu asimame kwenye ardhi aihukumu miungu .
              DANIELI 7:26-27
Mamlaka ya miungu itaondolewa milele.
               DANIELI 5:14
Ø  Unapoombea mtu au kujiombea mwenyewe ondoa:
·         miungu ya kabila
·         miungu ya ukoo
·         miungu ya familia
·         miungu ya waganga
·         miungu ya kigeni
·         miungu ya wapenzi( uliozini nao).
WAAMUZI 10:16
Ondoa hiyo miungu kwa damu ya Yesu.

MUNGU AKUBARIKI SANA




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*