ITUMIE MAMLAKA YA JINA LA YESU KUSHINDA NGUVU ZA GIZA

🍇 ITUMIE MAMLAKA YA JINA LA YESU KUSHINDA NGUVU ZA GIZA 🔥

Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829



📖 9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;


Wafilipi 2:9

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;


Wafilipi 2:10

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.


Wafilipi 2:11


🔥 Tumia jina la Yesu kuangusha ufalme wa giza .


🔥 Tumia jina la Yesu kuwafunga midomo wanaokunenea mabaya .


🔥 Tumia jina la Yesu kuomba chochote kile utakacho Mungu akutendee .


📖 14 Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.

Yohana 14:14


🛐 Kila uombalo omba kupitia jina la Yesu .


✍ Shetani hana mamlaka ya kukizuia kile ulichokiomba kupitia jina la Yesu .

✍ Jina la Yesu lina mamlaka ya upokeaji ( kupokea kile ulichokiomba ).



🔥 Unapolitaja jina la Yesu tambua kuwa unalitaja jina lenye nguvu kupita majina yote .

🔥 Jina hilo linapita majina yote .Lina mamlaka kupita majina yote.

🔥 Litumie kuteka na kuangusha ufalme wa giza .



🍇 Unalichukuliaje jina la Yesu maishani mwako ?

📖 14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.


Mathayo 16:14

15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

Mathayo 16:15

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

Mathayo 16:16



✍ Yesu ni mwana wa Mungu aliye hai

✍ Kama yeye ni mwana wa Mungu aliye hai tambua kuwa ndani ya jina lake kuna uzima yaani kuna uponyaji .Ukilitumia jina lake mambo yote yaliyoharibika yatachipuka upya .


📖 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.


Yohana 17:12



✍ Jina la Yesu ni ulinzi .

Huhitaji kuomba waganga watambike kwako liite jina la Yesu pekee .🔥🔥🔥🔥

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*