KAZI ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA MAISHA YAKO
KAZI
ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA MAISHA YAKO
SIKU
YA PILI
Mwl.Peter
Francis Masanja
0679392829
Basi
nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
Wagalatia
5:1
Maana
yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye
apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.
Wagalatia
6:8
🍇
Roho Mtakatifu hutupa uwezo wa kuishinda
dhambi .
✍ Anampa mtu uwezo wa
kuitawala dhambi .
✍ Maisha ya mtu yakikaa
katika uongozi wa Roho Mtakatifu , mtu huyo atakuwa kielelezo mbele za Mungu na
wanadamu .
✍ Mruhusu Roho Mtakatifu
atawale maisha yako utaona mambo yako yanaenda vizuri sana
✍ Roho Mtakatifu
anamfanya mtu achukie dhambi , aondoe hali ya ukawaida .
✍ Kila aliye na uongozi
wa Roho Mtakatifu anaushuhuda mzuri katika maisha yake .
✍ Kila aongozwaye na
Roho Mtakatifu ni jasiri au ni shujaa wa imani
Anamamlaka
ya kuonya , kukaripia na kukemea bila woga .
✍ Hii ni kwasababu Roho Mtakatifu humtia nguvu na
mamlaka ya kumkemea shetani na kazi zake zote .
✍ Utauliza kwanini sasa baadhi ya wakristo
wameangukia kwenye maisha ya dhambi , ina maana hawaongozwi na Roho Mtakatifu
💉
Jibu ni kwamba hawakuomba uongozi wake na kuamua kuuruhusu mwili uwaongoze .
✍ Hii imewafanya vijana
wengi kuanguka katika zinaa na matokea yake ni uangamivu .
✍ Hakikisha unawekeza maisha yako kwa Roho Mtakatifu
ili umpendeze Mungu
✍ Huwezi kuishinda
dhambi kwa mwili , utaanguka tu .
Cha
kufanya tafta uongozi wa Roho Mtakatifu .
✍ Roho Mtakatifu anakupa
tahadhari juu ya uovu .Kuna wakati watu wanaoongozwa na Roho Mtakatifu
wakikosea wanaingia hukumuni mioyoni mwao na kujutia kwanini wamefanya hivyo ✍ Roho Mtakatifu
anakufundisha njia ikupasayo kuifuata ili uwe salama .
✍ Kunena kwako ,
kuwajibu watu kuwe kuzuri ,
Kinywa
chako kinene maneno ya hekima .
Ili
uwe na hekima na busara lazima utafte uongozi wa Roho Mtakatifu .
📖
Maneno
yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo
kumjibu kila mtu.
Wakolosai
4:6
✍ Huwezi kuwa na hekima
ya kiMungu kama huna uongozi wa Roho Mtakatifu.
Utajikuta
unawajibu watu vibaya .
✍ Kumbuka tunazungumzia
umuhimu wa Roho Mtakatifu katika kuishinda dhambi .
✍ Roho Mtakatifu anakupa uwezo wa kujitambua thamani
yako mbele za Mungu .
✍ Kwa sababu yeye ni
Mtakatifu basi na wewe inabidi ujitambue kuwa wewe ni mali yake .Kwahiyo
anakwambia usiuchafue mwili wako .
📖
19
Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu,
mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
1
Wakorintho 6:19
✍ Roho Mtakatifu anakupa
uwezo wa kujitambua wewe ni nani na unapaswa kufanya nini ili usimkose Mungu ❓
Kujitambua
hapa ni kujua kuwa mwili ulionao ni hekalu la Roho Mtakatifu na hupaswi
kuuchafua .
✍ Baada ya kutambua hilo
uishi sawasawa na neno la Mungu na kulitendea kazi .
✍ Anakupa akili ya
kupima kila jambo ufanyalo , je linamletea Mungu utukufu ❓
Kwahiyo
ni yeye anakuletea ufahamu wa kuyapima kila uyafanyayo kama yanamtukuza Mungu .
Huwezi kumwomba Mungu ukisema 🛐🛐
Ee
Mungu nakuomba nikanywe pombe au nikazini na mke wa mtu uniongoze kwa Roho wako
Mtakatifu 😨😨😨😨
Ukiona
jambo lolote huwezi kuomba uongozi wa Roho Mtakatifu ujue ni dhambi achana nalo
.
✍ Leo kaa jitafakari kwa makini sana kama ifuatavyo :
✍ Kama unaishi maisha ya
zinaa ,unazini na wake za watu , unazini na kila kijana , unanunua pombe ,
unatukana , unajisaga ,unapiga punyeto , unakaa barazani kupiga umbea , je una
Roho Mtakatifu ❓
Jibu
ni kwamba umekufa kiroho ni marehemu anayetembea .
Roho
Mtakatifu amekukimbia unaishi kimwili na siyo kiroho tena .
✍ Kama unaishi kwa
kuheshimu watu wa kila rika na wengi wanatamani waige maisha yako na tabia zako
njema tambua wewe unaongozwa na Roho Mtakatifu.
✍ Matendo yako yamfanye
Roho Mtakatifu afanye makao ndani yako .
Ukiishi
maisha ya kutenda machukizo Roho Mtakatifu hukimbia kabisa maana wewe siyo mtu
tena bali ni mwanadamu mwenye tabia za mnyama .
✍Kama vile mnyama asivyo
na Roho Mtakatifu vivyo hivyo na mtu akibeba uanadamu hufanya mambo kama mnyama
.
✍ Mtu anatabia za Rohoni
bali mwanadamu anatabia za mwilini ndiyo maana ni kawaida sana mtu akigeuka
kuwa mwanadamu kanisani utamwona anajiingiza kuchafua kanisa.
📖
14
Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake
huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya
rohoni.
1
Wakorintho 2:14
15
Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.
1
Wakorintho 2:15
✍ Jifikirie , je unauongozi wa Roho Mtakatifu ❓
💉
Kama unang'ang'ania umjue mchumba wako kabla ya ndoa je huko ni kuongozwa na
Roho Mtakatifu au mwili ❓
Na
kama ni mwili basi ni dhambi kwako wewe .
✍ Heshimu sana mambo
matamu kimwili lakini madhara yake kiroho ni makubwa sana .Wanaofanya zinaa
husema ni tamu sana ni raha lakini wakiugua magonjwa wanakuwa washauri wazuri
sana kwetu maana walipanda kwa mwili wamevuma mauti .
Asikudanganye
mtu eti utumike , utauziwa mbuzi kwenye gunia hutafanya vizuri ndani ya ndoa ,
jitenge na waovu .
Mpendeze
Mungu .
✍ Mheshimu Roho Mtakatifu akaaye ndani yako asije
akakukimbia ukafa kiroho na kimwili pia . ✍ Panda kwa roho uvune mema .
🍇
Mungu akubariki sana
Nakutakia
siku njema yenye baraka
Naitwa
: Mwl.Peter Francis Masanja
0679392829
📖
4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;
1
Wathesalonike 4:4
5
si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.
1
Wathesalonike 4:5
Maoni
Chapisha Maoni