ROHO MTAKATIFU
🍇 ROHO MTAKATIFU 🍇
SIKU
YA KWANZA
Mwl.Peter
Francis Masanja
0679392829
Bwana
Yesu asifiwe sana
✍ Karibu sana katika
ufunguzi wa semina yetu siku ya leo .
✍ Biblia imezungumza
habari za roho Mtakatifu tangu Agano la kale amezungumzwa sana lakini kwa namna
ambayo msomaji wa biblia anatakiwa kumfuatilia kwa kina .
✍ Roho Mtakatifu alijifunua kwa watumishi wa Mungu
ambao yeye aliwachagu
✍ Ametajwa katika kitabu
cha Isaya katika utatu mtakatifu .
📖 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake,
wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu , ni Bwana wa majeshi; dunia yote
imejaa utukufu wake.
Isaya
6:3
Katika Isaya 6:3 tunaona neno Mtakatifu
limetajwa mara tatu kudhihirisha jina la Mungu kwa namna ya utatu Mtakatifu .
Yaani
Mungu baba, Mwana na Roho Mtakatifu
Mtakatifu
, Mtakatifu , Mtakatifu .
Kwahiyo
kwa waombaji wanaoanza kuomba wakianza na neno Mtakatifu lazima wataje mara
tatu ili kumzunguzia Mungu katika utatu Mtakatifu .
✍ Roho Mtakatifu alifunuliwa kwa kinywa cha nabii
Isaya
📖 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa
sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma
ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa
habari za kufunguliwa kwao.
Isaya
61:1
✍ Nabii alifunuliwa
habari hizi na kazi Roho Mtakatifu moja wapo ikiwa kutia mafuta ( upako ) .Kazi
ya Roho Mtakatifu ni kumjaza mtu upako wa injili na nguvu za kiroho na mamlaka
juu ya nguvu za giza .
✍ Maana yake ni kwamba
Roho Mtakatifu akifanya makao ndani ya mtu , huyo mtu anakuwa na nguvu za
kiroho na atafungua wengi sana .
Roho Mtakatifu ni mtakatifu ( msafi , siyo
mchafu ) hii ndyo sifa yake kuu .
Anakaa
patakatifu
📖 Msimzimishe Roho;
1
Wathesalonike 5:19
✍ Hawezi kukaa ndani ya mtu anayejichafua kwa dhambi
.
✍ Biblia ya English
Revised Version
Inasema
tusiondoe kazi ya Roho Mtakatifu ndani yetu .
📖
Don’t stop the work of the Holy Spirit.
1
Thessalonians 5:9
ERV
✍ Tutaondoaje kazi ya
Roho Mtakatifu ndani yetu ❓
Ni
kwa kutenda dhambi
📖 You should know that your body is a temple
for the Holy Spirit that you received from God and that lives in you. You don’t
own yourselves.
1
Corinthians 6:19 ERV
✍ Miili yetu ni hekalu (
nyumba ) ya Roho Mtakatifu kwahiyo ili akae ndani lazima tuwe safi .
✍ Hatujimiliki wenyewe
tuliookoka miili yetu ni mali ya Roho Mtakatifu
📖 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la
Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu
wenyewe;
1
KOR. 6:19
🍇 MATUNDA(
KAZI) YA ROHO MTAKATIFU 🍇
✍ Roho Mtakatifu ana
matunda mengi sana katika maisha ya wokovu .
🍇 Roho Mtakatifu anabadilisha tabia za
mtu .
Anaondoa
tabia mbaya na kumjaza mtu mambo saba ambayo Mungu anayataka ayaone ndani ya
mtu .
Mambo
haya ni yafuatayo :
🍇 Roho ya BWANA
Inakusaidia
kudhirisha tabia za Mungu ndani yako .
Wakikuona
watu waone sura ya Mungu.
🍇 Kumcha Mungu
🍇
Hekima
🍇
Ushauri
Kushauri
watu kiroho.
🍇Ufahamu
Utakusaidia
kupinga au kuikataa dhambi .
🍇
Uweza
Nguvu
za Mungu
🍇 Maarifa
Yatakusaidia
kufanya maamuzi sahihi juu ya maisha yako ya kiroho na kimwili bila kumkosea
Mungu
📖
2
Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na
uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana;
Isaya
11:2
Roho
Mtakatifu anampa mtu uwezo wa kunena kwa lugha .
📖
1
Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
Matendo
ya Mitume 2:1
2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi,
ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
Matendo
ya Mitume 2:2
3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja
wao.
Matendo
ya Mitume 2:3
4
Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho
alivyowajalia kutamka.
Matendo
ya Mitume 2:4
✍ Kunena kwa lugha ni
moja ya kazi ya Roho Mtakatifu kwa aliyeokoka
.
📖
Nami
nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini zaidi sana mpate kuhutubu, maana
yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili
kusudi kanisa lipate kujengwa.
1
Wakorintho 14:5
✍ Kunena kwa lugha siyo
kazi ya kufundishwa na mtu unene ni kazi ya Roho Mtakatifu hiyo kukufundisha
wewe kunena , akikushukia utanena tu .
🍇
Roho Mtakatifu ni mwalimu .
📖
kwa
kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha saa ile ile yawapasayo kuyasema.
Luka
12:12
Lakini
huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu,
atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Yohana
14:26
✍ Anakufundisha ufanye
nini
✍ Unahitaji kumsikiliza
Roho Mtakatifu nini anakwambia ufanye ili ufanikiwe kiroho na kimwili.
✍ Unaweza ukapanga jambo
fulani ulifanye lakini akilikataa utaona matokeo yake katika ulimwengu wa roho
( ulimwengu usioonekana ).
✍ Mheshimu sana mwalimu
wako ( Roho Mtakatifu ) akisema fanya hiki fanya akikataa acha .
✍ Anatufundisha kuenenda
katika kwa adabu na hekima dunia hii ,
tusiwe na majibu mabaya kama watu wasiomjua Mungu .
Mungu
akubariki sana naomba niishie hapo katika siku ya ufunguzi wa semina hii
Maoni
Chapisha Maoni