THAMANI YA UBIKIRA WAKO


                                       🍇 THAMANI YA UBIKIRA WAKO 🍇


Mwl.Peter Francis Masanja
0679392829
📖 Basi watumishi wa mfalme waliomhudumu walimwambia, Mfalme na atafutiwe mabikira vijana wazuri;
Esta 2:2
🍇 Ijue thamani ya ubikira wako ,
Jitunze , subiri ndoa .
📖 Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.
Mithali 22:3
📖 10 Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, Wewe usikubali.
Mithali 1:10

🍇 Epuka makundi yapotoshayo ili utunze ubikira wako .Epuka kujichafua
📖 Hawa ndio wasiotiwa unajisi pamoja na wanawake, kwa maana ni bikira. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
Ufunuo wa Yohana 14:4



                                  
                  


                🍇 SABABU ZA KUPOTEZA UBIKIRA 🍇

Pointi 1;Kukosa hofu ya Mungu .
Uongo wa wanaume.
Pointi 2.Tamaa
Point 3: Makundi ya marafiki wabaya .
 Pointi 4 . Utandawazi
Pointi 5: Ubakaji
Pointi 6: Malezi mabaya toka kwa wazazi
Pointi 7:Wanawake kukubali kutolewa
Kutaka kujaribu wajione nao wamekua .
Pointi 8: Malezi hafifu ya kiroho .
Pointi 9: Ni mpango uliosukwa na shetani kuvuruga ndoa za watu .
Pointi 10: Kuingia kwa mafundisho ya mashetani .
Pointi 11: Umaskini ( maisha magumu ).
🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻
 🍇 Leo nitazungumzia mambo yanayosababisha mabikira kupungua hapa duniani
Katika darasa la jioni hii tutaangalia sababu hizi ili vijana na wazazi pia watambue
Kamwe hakuna apendaye kununua bidhaa iliyotumika ili akaifanyie marekebisho .
Kila mtu mume au mke anapenda ampate mwenzi aliyejitunza na hili ndiyo kusudi kuu la Mungu .
Kwa maana hii Mungu anauthamini sana ubikira kuliko unavyofikiria .
Kwenye biblia tukiangalia katika agano la kale tunaona kwamba
Mwanaume akimtoa binti ubikira sharti amuoe kwasababu amemtia unajisi ( thamani ya usichana wake imepotea tena ).

Na atakuwa amewaletea aibu wazazi wake kwenye jamii
📖 13 Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,
Kumbukumbu la Torati 22:13
14 kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;
Kumbukumbu la Torati 22:14
15 ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;
Kumbukumbu la Torati 22:15

16 na baba yake yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye amchukia;
Kumbukumbu la Torati 22:16
17 angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.
Kumbukumbu la Torati 22:17
18 Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu mume na kumrudi,
Kumbukumbu la Torati 22:18

  Ubikira ukitolewa thamani ya binti inakuwa haipo tena , ndyo maana enzi za Musa kijana akimtoa ubikira binti lazima amuoe
. Bikira ilithaminiwa mno hapo zamani na ndoa zilikuwa hazina migogoro mingi na mababu zetu walizeekea kwenye ndoa .Lakini leo miaka miwili tu mikwaruzo .
📖 Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso wake, bikira, wala mwanamume hajamjua bado; akashuka kisimani, akajaza mtungi wake, akapanda.
Mwanzo 24:16
Raheli mke wa Yakobo alimuoa bikira ✍✍✍✍✍✍✍

Ubikira unaambatana na malezi mazuri , ukikuta familia mabinti bikira hiyo familia inaheshimika sana.
Binti kutolewa bikira ni ishara ya malezi feki na wazazi kukosa utii mbele za Mungu .
📖 Hawa ndio wasiotiwa unajisi pamoja na wanawake, kwa maana ni bikira. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
Ufunuo wa Yohana 14:4
Ubikira wa kiroho yaani kutokutumikia miungu mingine baada ya kuzaliwa mara ya pili unathamani sana kwa Mungu
Huu unafananishwa na ubikira wa mwili thamani yake kutokutiwa unajisi .
Mungu mwenyewe anasema mbinguni wataingia mabikira ( wasiotiwa unajisi kwa kuabudu sanamu au kumtumikia shetani yaani wasio na chapa ya ibilisi )hawa wasio na chapa ya shetani ( maovu ) ni mabikira mbele za Mungu .
Kwahiyo Ubikira lazima utunzwe sana .Usiguswe na mwanaume yeyote subiri uolewe kabisa , mwili wako ni kwaajili ya mume wako .
Nawewe mwanaume usiguse binti yeyote subiri uoe maana mwili wako ni kwaajili ya mkeo tu .
📖 2 Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.
2 Wakorintho 11:2
3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.
2 Wakorintho 11:3
Mungu anataka kuona watu wakioana mabikira
Kwahiyo thamani ya ubikira inatambuliwa na Mungu pia kuwa ni usafi
Kipindi kijacho tutaangalia hasara za kutolewa ubikira wako .✍✍✍✍✍✍✍✍
Mungu akubariki sana


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

🔰 MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA 🛐*