SILAHA ZA KIROHO

✍🏻 SILAHA ZA KIROHO πŸ–Š

πŸ“–SOMO LA KWANZA πŸ“–


Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829


πŸ“– 11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

Waefeso 6 :11


πŸ–Š Bwana Yesu Kristo asifiwe


πŸ–Š Tukivitafakari vita vya rohoni tunaona kuna falme mbili yaani ufalme wa Mungu na ufalme wa shetani .


πŸ–Š Lakini ufalme wa Mungu ni mkuu na unanguvu kuliko ufalme wa shetani .


πŸ–Š Pia tunaona kuwa kuna mamlaka mbili za kiroho

πŸ–ŠMamlaka ( Authority ) ni nguvu ya kuamua/kuamuru jambo litokee au lifanyike .


πŸ–Š Zitazame hizi mamlaka

1⃣ Mamlaka ya Mungu .

πŸ–Š Mamlaka hii ni kuu kuliko mamlaka zote .Hakuna mamlaka iwezayo kuishinda mamlaka ya Mungu .


2⃣ Mamlaka ya shetani

πŸ–Š Hii ni mamlaka itendayo kazi hapa duniani kwa lengo la kuiba , kuua na kuangamiza .Mamlaka hii imejaa uongo na na ni dhaifu hainauwezo wa kuishinda mamlaka ya Mungu .

πŸ–ŠPia kuna wakuu wawili naam

1⃣ Mungu ni mkuu sana

πŸ–Š Mungu ni mkuu kwa watu wake na huwapa watu kushinda na amewapa watu mamlaka ya kutamka jambo likawa .


2⃣ Shetani mkuu wa dunia na baba wa uongo ndiye awanasaye watu kufuata tamaa zake .

πŸ–Š Huyu hutenda kazi pamoja na wachawi , waganga , na waabudu sanamu na waabuduo wafu pamoja na wafuatao tamaa zake na wapinga Kristo

πŸ–Š Katika ulimwengu wa roho wewe umchaye Mungu tambua anakutumia akijua wewe ni silaha yake ya vita .

πŸ“– 20 Wewe u rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;

Yeremia 51 :20

21 na kwa wewe nitamvunja-vunja farasi, na yeye ampandaye; na kwa wewe nitalivunja-vunja gari la vita, na yeye achukuliwaye ndani yake;

Yeremia 51 :21

22 na kwa wewe nitawavunja-vunja mwanamume na mwanamke; na kwa wewe nitawavunja-vunja mzee na mtoto; na kwa wewe nitawavunja-vunja kijana mwanamume na kijana mwanamke;

Yeremia 51 :22

23 na kwa wewe nitamvunja-vunja mchungaji na kundi lake; na kwa wewe nitamvunja-vunja mkulima na jozi yake ya ng'ombe; na kwa wewe nitawavunja-vunja maliwali na maakida.

Yeremia 51 :23

πŸ–Š Katika ulimwengu wa roho wewe umchaye Mungu umepewa nguvu ndani yako kwa sababu uliyembeba ndani yako yaani Yesu  ni mkuu kuliko mkuu wa dunia ( shetani ,ibilisi, Lusifa , nyoka wa zamani , mwizi , na baba wa uongo).

Sikia neno la BWANA
πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

πŸ“– 4 Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.

1 Yohana 4 :4

πŸ–Š Katika ulimwengu wa roho tuna pigana na falme , mamlaka, wakuu wa giza , na majeshi ya pepo wa wabaya .

Neno la Mungu linasema πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

πŸ“– 12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 6 :12

πŸ–Š Nataka nikwambie kwamba hakuna pepo wazuri kama ambavyo baadhi ya dini hufuga majini au mapepo ya utajiri na umaarufu wakiyaita ni pepo au jini wazuri .

Katika ufalme wa Mungu hatufugi pepo .❌❌❌❌❌❌❌

 πŸ–Š ZIFUATAZO NI SILAHA ZA KIROHO πŸ–Š

Nataka nikwambie kwamba watu wengi walioamini na kubatizwa wanapepetwa kama ngano na ibilisi kwa sababu ya kutotumia vizuri silaha ambazo Mungu kawaachia .


πŸ–Š Tuziangalie silaha hizi

πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

1⃣ IMANI

πŸ–Š Biblia inasema hivi πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

πŸ“– 16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Waefeso 6 :16


πŸ–Š Mwana wa Mungu anatakiwa awe na nguvu ya imani ili aweze kushinda nguvu za shetani .

πŸ–Š Unapoomba amini kwamba Mungu yupo na atakushindia vita uliyonayo .

πŸ–Š Waangalie wa kina Daniel alipotupiwa kwenye tundu la simba aliamini Mungu atamuokoa .

πŸ–Š Shadrak , Meshack na Abedinego nao waliokolewa kwa imani hawakuungua ndani ya tanuri la moto .
Hawakuungua kwa sababu waliamini Mungu yupo mweza wa mambo yote atawaokoa .


πŸ–Š Mkumbuke na Samsoni , kwa imani alijitwalia kisasi kwa Wafilisti


Sikia neno la BWANA
πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

πŸ“– 32 Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii;
Waebrania 11 :32

33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,
Waebrania 11 :33

34 walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.

Waebrania 11 :34


πŸ–ŠIlinde sana imani na uitumie kumwaibisha shetani .Maana wengi wamemfuata shetani kwa kushindwa kuitetea imani ?

πŸ–Š Imani ni silaha kuu sana ya kumshinda shetani na kumwaibisha .


2⃣ JINA LA YESU

πŸ“– 9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Wafilipi 2 :9

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Wafilipi 2 :10

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Wafilipi 2 :11


πŸ–Š Jina la Yesu Kristo pekee likitajwa pepo hutoka .

Hakuna awezaye kutoa pepo kwa jina tofauti na jina la Yesu Kristo.

πŸ–Š Hili jina likitajwa linanguvu na uweza na mamlaka ya kuharibu , kung'oa ,kubomoa , kuangusha na kuangamiza kazi zote za ibilisi .

Imeandikwa hivi πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

πŸ“– Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.

1 Yohana 3:8b


πŸ–Š Uponyaji wote na nguvu ya kutoa pepo umebebwa na jina la Yesu Kristo .

πŸ“–
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
Marko 16 :17

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Marko 16 :18


πŸ–Š Jina la Yesu ni silaha ya kiroho mtu akilitaja kwa imani atamshinda shetani .
3⃣ NENO LA MUNGU


πŸ–Š Wewe uliyeokoka tambua kuwa neno ni silaha ya kiroho .

πŸ–Š Unashauriwa sana ulijue neno la Mungu ili ibilisi asikunase na mitego ya dhambi .

πŸ“– 11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

Zaburi 119 :11


πŸ–Š Bila neno shetani atakutumikisha dhambini .

πŸ–Š Hakikisha unalitumia neno la Mungu ili kumshinda shetani .

Neno la Mungu ni upaga wa Roho

πŸ“– 12 Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

Waebrania 4 :12



πŸ–Š Unatakiwa uwe na neno la Mungu ili kushinda vita vya kiroho .


4⃣ DAMU YA YESU


πŸ–Š Damu ya Yesu Kristo inamwondolea shetani uhalali wa kumiliki na kutawala .

πŸ–Š Damu hii ndiyo imefanya upatanisho kati ya Mungu na wanadamu .

πŸ–Š Damu hii ndiyo sadaka ya ukombozi ilimwagika maramoja tu pale msalabani tukaponywa magonjwa na tukanunuliwa na Mungu kutoka kwenye mikono ya ibilisi .

Sikia neno la Mungu

πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»

πŸ“– 9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,

Ufunuo wa Yohana 5 :9

10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.

Ufunuo wa Yohana 5 :10


πŸ–Š Halleluyaaaaa.Nataka nikwambie kwamba ulipomwamini Yesu Kristo ukabatizwa ulikiwa mikononi mwa ibilisi .Mungu alitumia damu ya Yesu Kristo kukutoa mikononi mwa ibilisi   ,maana yake alimnyang'anya shetani uhalali wa kukumiliki akakupa na mamlaka ya kutawala hapa duniani .

πŸ–Š Ushindi huu ulioupata ni mkuu sana yaani umekombolewa kwa damu ya Yesu Kristo .

πŸ–Š Mshinde shetani kwa damu ya Yesu Kristo


πŸ“– 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

Ufunuo wa Yohana 12 :11


πŸ–Š Kila kitu kinachokuhusu kufunike kwa damu ya Yesu ,yaani familia yako na mali zako zote zifunike kwa damu ya Yesu Kristo.

πŸ–Š Palipo na damu ya Yesu Kristo , shetani hukosa makao na kutoweka kabisa .Damu ya Yesu ni moto ulao ikiwepo mahali mapepo hutoweka .

πŸ–Š Itumie damu ya Yesu Kristo katika maombi maana ni silaha ya kiroho .


πŸ–Š Napendanikwambie kwamba hakuna kupeleka sadaka ya ukombozi kwa mtumishi fulani , itumie damu ya Yesu Kristo ndyo sadaka ya ukombozi .


Mungu akubariki sana

Karibu katika mwendelezo wa somo hili ili uzione silaha zingine kumi za kiroho


Ni mimi

Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829

Baptist Church Mtwara

πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’πŸ’’

Unakaribishwa kwa maswali ,maoni  n.k

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*