MAFANIKIO YA KIUCHUMI

*πŸ”°MAFANIKIO YA KIUCHUMI πŸ”°*


SOMO LA PILI


Mwl Peter Francis Masanja

0679392829

https://peterfrancismasanja.blogspot.com




πŸ”° 20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae;

Mwanzo 28 :20

21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu.

Mwanzo 28 :21

22 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.

Mwanzo 28 :22


πŸ–Š Katika somo la kwanza nilifundisha somo la malango yako ya kiuchumi na mambo ya kushughulikia kwenye malango yako .


πŸ–ŠLeo nakukaribisha katika somo hili la pili tujifunze jambo moja kwa ufupi.


πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

✍🏻 *MAFANIKIO YA KIUCHUMI NI AGANO*


πŸ–Š Kila aliyefanikiwa kiuchumi alifanya agano kati ya uchumi wake na kile anachokiabudu .


πŸ–Š Inawezekana ikawa kafanya agano na mashetani akapokea masharti fulani ayafuate ili apate kujitanua kiuchumi kama vile kutoa kafara za damu ya ndugu zake ,mke wake , watoto wake, wazazi wake ,au wafanya kazi wake .Pia anaweza kupatana watu waugue magonjwa tu ya ajabu kama vile magonjwa ya akili n.k.Aidha , anaweza pia akaweka agano na kuzimu la kuoa na kuacha wake au kutokusaidia ndugu zake .


πŸ–Š Vivyo hivyo na mafanikio ya watu wa Mungu aliyehai mafanikio yao yapo kwenye agano na Mungu wao .


πŸ–Š Mungu akitaka kumfanikisha mtu anazingatia sana agano kati ya huyo mtu na uchumi wake ambalo kamwekea Mungu .


πŸ–Š Tunamwona Yakobo aliagana na Mungu kabla ya kwenda kutafta na alimfanikisha sana .


*πŸ”° 20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae;*

Mwanzo 28 :20

*21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu.*

Mwanzo 28 :21



πŸ–Š Yakobo aliweka nadhiri kwa Mungu kuhusu mafanikio yake ya uchumi .

πŸ‘‰Nadhiri ni ahadi ya kutimiza jambo fulani kwa kile ulichofanyiwa au unachotarajia kukifanya au kufanyiwa .


πŸ–Š Nadhiri kwa maana nyingine ni makubaliano au mapatano .

πŸ–ŠHakuna nadhiri bila kuwa na makubaliano

πŸ–Š Na hakuna agano bila kuwa na makubaliano au mapatano .

πŸ–Š Jambo la muhimu sana Mungu analitumia kumfanikisha mtu ni kuagana naye kwamba huyo mtu atafanya nini kwa ajili ya Mungu endapo atamfanikisha .


πŸ–Š Mungu ni mwaminifu sana katika agano au patano .Agano ni mkataba kwahiyo mtu wa Mungu anatakiwa aheshimu asitoke nje ya huo mkataba .

πŸ–Š  unapofanya agano la kiuchumi ujue mpaka wana wa wanao watanufaika na huo uchumi .

πŸ–Š Katika  Somo linalofuata tutaona matokeo ya kufanya agano na Mungu kiuchumi

Karibu sana .

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAIDA YA KUJAA ROHO MTAKATIFU

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA

πŸ”° MBINU ZA KUFUNGA NA KUOMBA πŸ›*