Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

*KUMKOMBOA ALIYEFUNGWA NA MIUNGU YA UKOO*

🔥 * KUMKOMBOA ALIYEFUNGWA NA MIUNGU YA UKOO* 🔥 Sehemu ya Kwanza 💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒💒 10 Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma, Zaburi 107 :10 👉 Mtu alinayetumikishwa na miungu ya ukoo yupo kwenye taabu sana Amefungwa hafurukuti na ana asilimia chache sana za kumjua Mungu Hivyo basi anahitaji kufunguliwa huko alikoshikwa kupitia matambiko na matamko ya ukoo 2 Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako, Mithali 6 :2 👉Maneno yanakamata maisha ya mtu Hivyo jina lako likiingizwa kwenye orodha ya majina ya ukoo kupitia matambiko utahangaika sana 👉 Unaweza ukashangaa tena baadhi ya familia wanafunga mbuzi wenye mabaka meusi na meupe na wale mbuzi weusi kengele shingoni ili kupitia hao mbuzi wakiomba jambo lolote watalipata Cha ajabu zaidi hao mbuzi wanapewa majina ya mababu waliokwisha kufariki tayari na kuwafanya miungu yao 👉 sasa utakuta unapewa jin

ONYO KWA WA KINA DADA

*ONYO KWA KINA DADA AMBAO HAWAJAOLEWA * 🔥 DADA AKILALA NA MWANAUME KABLA YA NDOA ANAUWEZEKANO MKUBWA WA KUACHIKA MARA TU WANAPOMALIZA UCHAFU WAO ANAKOSA THAMANI KWA HUYO MWANAUME ANAMLINGANISHA NA FULANI WA AWALI 8 Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma. Maombolezo 1 :8 9 Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza. Maombolezo 1 :9 10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako. Maombolezo 1 :10 11 Watu wake wote hupiga kite, Wanatafuta chakula; Wameyatoa matamaniko yao wapate chakula Cha kuihuisha nafsi; Ee Bwana, tazama, uangalie; Kwa maana

SHAUKU YA MATAIFA

Shauku ya mataifa /The disire of agecy Mwanadamu anakimbizana wakitaka kutafuta shauku,na Huku wanadamu wakitaka kutafuta shauku wao wenyewe,kwa kweli hawataweza,.Kristo huyu ndiye mwenye kuwezesha shauku hii.  Luke 2;8-14. Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku. 9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang?aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. 10 Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; 11 maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana. 12 Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng?ombe. 13 Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, 14 Atukuzwe Mungu juu mbinguni,Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.huyu ndiye injili hasa,na Kama ni injili basi ni mkombozi wa mw

DHAMBI YA USHOGA

Picha
🔥 *DHAMBI YA USHOGA  🔥 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 1 Wakorintho 6:9 🔥Tangu enzi za sodoma na Gomora mpaka sasa tunauona ushoga na ufiraji unakua kwa kasi sana duniani . 🔥 Kipindi cha Nuhu ,Mungu alipoona wanadamu wanazidi  maovu aliwaangamiza kwa gharika. 5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. Mwanzo 6 :5 🔥Hata Sodoma na Gomora aliiangamiza kwa moto kutokana na maovu kuzidi na moja wapo ni hili la ushoga na ufiraji 15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. Mwanzo 19 :15 24 Ndipo Bwana akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa Bwana. Mwanzo 19 :24 🔥Nakukumbusha tena kwa msi

DHAMBI YA USHOGA NA UFIRAJI* 🔥

Picha
🔥 * DHAMBI YA USHOGA NA UFIRAJI* 🔥 💒Peter Francis💒 0679392829 0744056901 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 1 Wakorintho 6:9 🔥Tangu enzi za sodoma na Gomora mpaka sasa tunauona ushoga na ufiraji unakua kwa kasi sana duniani . 🔥 Kipindi cha Nuhu ,Mungu alipoona wanadamu wanazidi  maovu aliwaangamiza kwa gharika. 5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. Mwanzo 6 :5 🔥Hata Sodoma na Gomora aliiangamiza kwa moto kutokana na maovu kuzidi na moja wapo ni hili la ushoga na ufiraji 15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. Mwanzo 19 :15 24 Ndipo Bwana akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa

CHUNGA UVAAJI WAKO WEWE MWANAMKE* 💒 .

Picha
💒 * CHUNGA UVAAJI WAKO WEWE MWANAMKE* 💒 . Peter Francis 0679392829(what's App) 0744056901 Facebook: Peter Francis Masanja francispeter424@gmail.com 🚶🏻‍♀MIILI YA WADADA LEO IMEKUWA SILAHA YA KUWAUA WANAUME HII TUNASEMA NI DHAMBI YA KUWASABABISHA WEBGINE WATENDE DHAMBI KWA KUTENGENEZA VISHAWISHI 👉 kutembea nusu uchi ni dhambi ya ukoseshaji 👉kutembea ukionyesha matamanio kama vile mapaja, kitovu, kiuno , maziwa , na nguo za kukubana na kukuchora umbo na nguo zinazoonesha nguo za ndani ni dhambi ya kukosesha watu wanaokuona . Ole ni wa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha! Maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha; lakini ole wake mtu yule aliletaye jambo la kukosesha! Mathayo 18:7 👉 mnawafanya wanaune wazini kwa kuwaza maana hata kuwaza kufanya ngono na mtu fulani ni dhambi Tena ndiye aliyefanya mahali pa juu milimani pa Yuda, na kuwaendesha katika uasherati wenyeji wa Yerusalemu, na kuwakosesha Yuda. 2 Mambo ya Ny

VUNJA MADHABAHU YA UKOO INAYOFANYA MATAMBIKO NA MAZINDIKO KUPITIA MIZUMU

Picha
🔥 VUNJA MADHABAHU YA UKOO INAYOFANYA MATAMBIKO NA MAZINDIKO KUPITIA MIZUMU  2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; Kumbukumbu la Torati 12 :2 3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo. Kumbukumbu la t 12 :3 👉 Angalia jinsi mizimu inavyoongea na watu wanapoenda kuabudu makaburini 4 Nawe utashushwa, nawe utanena toka chini ya nchi, na maneno yako yatakuwa chini toka mavumbini; na sauti yako itakuwa kama sauti ya mtu mwenye pepo, ikitoka katika nchi, na matamko yako yatanong'ona toka mavumbini. Isaya 29 :4 Ingia kwenye Maombi sambaratisha , vunja ,bomoa , na kuichoma moto ile madhabahu ya ukoo wanapoitumikia miungu mingine . 1 Ole wa watoto waasi; asema Bwana; watakao mashauri lakini

MAJIBU YA MAOMBI YAKO YANATEGEMEA IMANI ULIYONAYO*

Picha
* MAJIBU YA MAOMBI YAKO YANATEGEMEA IMANI ULIYONAYO* 👉 Ukiamini kupokea vidogo utapokea vidogo 👉Mungu atakujibu kulingana na unachoamini 👉Yule mwanamke aliyetokwa damu mda wa miaka 12 aliamini akigusa vazi la Yesu atapona .Ndyivyo ilivyokuwa akapona 25 Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, Marko 5 :25 26 na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya Marko 5 :26 27 aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; Marko 5 :27 28 maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona. Marko 5 :28 👉Wengine waliamini katika kuwekewa mikono na Yesu wakapona na ndivyo ilivyokuwa 22 Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake, Marko 5 :22 23 akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate k

MITANDAO NA UFALME WA MBINGUNI*

👑 *MITANDAO NA UFALME WA MBINGUNI* 👑 12 Ingawa uovu una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;  Ayubu 20 :12 👑 Kuna watu wanaitumia mitandao kwa maneno yao matamu kurubuni watu . 🔥 Mitandao itawapeleka motoni kwa kutumia ndimi zenu mnanena udanganyifu   *MITANDAO* 🔥 Mitandao imerahisisha dhambi leo hii watu wanatumiana picha za uchi na kufanya uasherati na uzinzi  48 Hivyo nitaukomesha uasherati katika nchi hii, ili wanawake wote wafundishwe, wasifanye mambo ya uasherati wenu.  Ezekieli 23 :48 49 Nao watawalipa ninyi malipo ya uasherati wenu, nanyi mtachukua dhambi za vinyago vyenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.  Ezekieli 23 :49 👉🏻mbingu na ardhi zimeandika uovu wa mitandao na kila utakapoenda huwezi fanikiwa umefungwa kupitia ardhi  27 Mbingu zitafunua wazi uovu wake, Nayo nchi itainuka kinyume chake.  Ayubu 20 :27 KAMA TAJIRI ILIVYO NGUMU KUURITHI UFALME WA MUNGU  NDVYO ILIVYO NA MTU ATUMIAYE MI

*MAOMBI YA UPONYAJI

Picha
*MAOMBI YA UPONYAJI * 🔥 BWANA Yesu asifiwe sana 👉inawezekana umeomba miaka mingi lakini bado unahangaika na tatzo 👉 siyo kwamba hujii kuomba lakini kuna roho ya mauti imefunga maisha yako bila wewe kujua . 👉 Umefungwa wapi sasa ❓ Tuone hapa 🔥 kila mchumba anayekuja kwako anakuacha ujue umefungwa 🔥 kila unapoanzisha biashara inakufa au unataka kuanzisha unaogopa utapata hasara hyo ni mauti iloyofunga uchumi wako . 🔥 Kila unapotaka kusoma neno la Mungu unapata usingizi ,ukiona hali hyo ujue kuna mauti imeshikilia maisha yako usimjue Mungu zaidi  *Tuombe* Baba katika jina la Yesu ,ninakuja kinyume dhidi ya nguvu zote za giza zilizoshikilia maisha ya watu wako ninasambaratisha nguvu za kaburi na kila roho za mauti zilizoshikilia maisha ya watu wako kwenye afya ,kwenye uchumi,kwenye,ndoa,na kwenye elimu katika jina la Yesu  .Kama ilivyoandikwa katika HOSEA 13:14 kusema 14 Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi

NDIYE MKE AU MUME BORA ?

Picha
MCHUMBA YUPI NI MKE / MUME BORA ? Mithali 19 : 14 Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana. Hebu soma tofauti hizi za uchaguzi wa wachumba kulingana na kundi la mtu anayechagua. =*Kijana wa kiume asiyemcha MUNGU akihitaji mchumba hutaka sifa zifuatazo zote au baadhi ya sifa hizi*.* 1. Umbo zuri linalosifiwa na marafiki zake. 2. Sura nzuri inayowafanya marafiki zake wamsifie kwamba amepata kifaa. 3. Msomi kama yeye. 4. Anatoka familia nzuri. 5. Anamjua MUNGU japokua yeye muoaji ni mpagani. 6. Tabia nzuri japokua yeye muoaji hana tabia nzuri hata moja. 7. Atembee nae kwanza ili aone kama anafaafaa kumbe ni dhambi na hatari sana ya kuuvunja uchumba kabla hata ya ndoa. Mithali 31:10 ''Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani. '' =Binti asiyemcha MUNGU akihitaji mchumba hutaka sifa zifuatazo zote au baadhi ya sifa hizi. 1. Awe na pesa za kutosha zitakazomtosha ka

YESU NDIYE VYOTE KATIKA VYOTE

Wakolosai 1;15-20 15naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. 18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. 19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae; 20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni

NITAMJUAJE KAMA NI YEYE

Picha
🌹🌹 * NITAMJUAJE KAMA NI MCHUMBA SAHIHI WA NDOA * 🌹🌹             Mtu utamjua huyu ndye mchumba akiwa anapenda upendavyo wewewewe Asiyependa dunia kuliko kumpenda Mungu . Kama wewe umeokoka mpime mtu wako kwa vitu vya dunia ujue mapema Ikiwa anayajua ya dunia kuliko hata Mungu huyo hakufai Na kama akitaka ngono kabla ya ndoa huyo hakufai kabsa mkimbie 🏃 Angalia marafiki zake pia ,kama anamarafiki wengi sanaa wasiofaa kimaadili ujue hapo kunajambo Mwangalie  kama wewe unamtukuza Mungu kweli jihadhari sana utaangushwa kiimani na mtu mzembe wa neno la Mungu Mwangalie atakufanya imani yako istawi zaidi au idumae zaidi Huwezi ukawa mchungaji halafu umeoa mwanamke mbishi mwenye kiburi hutatamani hata kufundisha masuala ya ndoa . Mpime mchumba wako kwenye ukweli na uwazi Kama akikudanganya jambo Fulani na ukaja kufuatilia ukaona ni uongo jua huyo hakufai Mchumba wa kukufaa ni yule anayekuwa na malengo na wewe ya kuwa mtaishije mkioana Pete

FAIDA YA KUOMBEA TAIFA

Picha
AYUBU 22:21 👉 *_Taifa ni nini_* ❓ Taifa ni watu wanaoishi katika eneo fulani waliounganishwa na lugha moja kama njia ya mawasiliano yao ya kila siku . 💒 Katika taifa lolote kuna mfumo wa utawala unaoongoza watu waweze kufikia malengo yao ya kimaisha ili wapate kuifurahia nchi yao waikaayo . 👉 Taifa lolote linahitaji kuendesha kwa misingi na kanuni za Mungu ili kila kitakachofanyika kipate kibali kwa Mungu ili watu wakaao katika nchi hiyo wabarikiwe .  🇹🇿_Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. Mwanzo 11:6 🇹🇿 _ 🇹🇿 *Nchi ni nini* ❓ Nchi ni ardhi yenye mipaka halali ya umiliki . 👉 Tanzania ni nchi yenye mipaka halali ya umiliki , ndyo maana kaskazini imepakana na Kenya na Uganda , Mashariki imepakana na bahari ya Hindi , Kusini imepakana na Msumbiji na Zambia , na Magharibi imepakana na Congo .  _Nchi hii inamilikiwa na watu wa kabi